• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RC AKABIDHI MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 142 KWA VIKUNDI 29 VYA MANISPAA YA TABORA

Posted on: December 2nd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Phillemon Sengati amekabidhi hundi yenye thamani shilingi milioni 142 kwa vikundi 29 vya wanawake na vijana wa Manispaa ya Tabora.

Mikopo hiyo imetolewa kwa vikundi hivyo ikiwa ni sehemu ya Manispaa ya Tabora kutimiza takwa la Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa ya mwaka 2019 inayoitaka kila Halmashauri  kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake, vijana na walemavu.

Dkt. Sengati amekabidhi mikopo hiyo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ukumbi wa jengo la Manispaa lilipo Viwanja vya Nane Nane maarufu kwa jina VIwanja vya Fatuma Mwasa.

Akikabidhi mfano wa hundi hiyo, Dkt. Sengati alivitaka vikundi vilivyopata mkopo kutumia fedha hizo katika miradi na malengo waliyoombea mikopo na sio katika shughuli nyingine zisizokuwa za maendeleo.

“Nendeni mkazitumie pesa mlizozipata leo kwenye miradi, malengo na makusudio ya mikopo yenu kama ambavyo amliomba na wala msiende kuzitumia kinyume na kusudio la shughuli zisizokuwa za kimaendeleo, ili ifike wakati muweze kusafirisha biashara zenu nje ya Mkoa na hata mpaka nje ya Nchi,” alisema Dkt. Sengati.

Aidha Dkt. Sengati aliutaka Uongozi wa Manispaa kuandaa mpango wa kutoa elimu ya Usimamizi wa Fedha na kufikiri kimkakati kwa wajasiriamali kabla ya kuwapa mikopo ili waweze kutumia fedha hizo kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao wenyewe, na Taifa kwa ujumla.

Sanjari na hayo, Dkt Sengati aliutaka uongozi wa Manispaa ya Tabora kutoa mikopo kwa uwazi bila ucheleweshaji na kuepuka rushwa kwa vikundi vinavyoomba na kwamba ifike wakati sasa uongozi wa Manispaa utoe fedha nyingi na vifaa kwa vikundi ili matokeo yake yaweze kuleta tija kwao wenyewe na Mkoa kwa ujumla.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Christina Bunini alisema katika mwaka wa fedha unaoendelea wametenga kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 445 kwa ajili mikopo ya vikundi kama sheria inavyotaka.

Alisema kati ya fedha hizo wamepanga kutoa kiasi cha shilingi milioni 178 kwa wanawake, milioni 178 kwa vijana na milioni 89 kwa watu wenye ulemavu.

Bunini aliongeza hadi hivi wameshapokea maombi mengi zaidi ya fedha ya fedha iliyotengwa katika bajeti.

Alisema toka Julai hadi Oktoba mwaka huu wameshapokea maombi ya mikopo kwa vikundi 79 ambayo thamani yake ni sawa na shilingi milioni 566.5.

Bunini alisema kati ya fedha hizo vikundi 61 vya wanawake vimeomba kiasi cha shilingi milioni 463, vijana 12 vimeomba shilingi 76 na watu wenye ulemavu 6 vimeomba shilingi milioni 27.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Tabora Tumaini Mgaya alisema hadi hivi sasa Manispaa ya Tabora imekwisha kutoa kiasi cha shilingi milioni 211 kwa vikundi 41.

Alisema kuwa pamoja na jitihada hizo kuna baadhi ya vikundi vimekuwa havirejeshi mikopo kwa wakati na kusababisha wanavikundi wengine wanaohitaji kuchelewa kupata fedha.

Alisema miongoni mwa vikundi ambavyo vinadaiwa ni vya vijana na watu wenye ulemavu na kuna baadhi ya vikundi vimekuwa vikianzisha miradi tofauti na ile waliyombea mikopo

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2020 January 15, 2021
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA (PSLE) 2020 November 21, 2020
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 MANISPAA YA TABORA December 18, 2020
  • Usafi wa Mazingira kwa Wananchi Wote, Jumamosi ya mwisho kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI MANISPA YA TABORA LAPITISHA MAPENDEKEZO YA BAJETI YA BILIONI 50.7 KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022

    February 13, 2021
  • DC KOMANYA AZINDUA SHUGHURI ZA UHAMASISHAJI WA BIMA YA AFYA YA JAMII (CHF ILIYOBORESHWA) MANISPAA YA TABORA

    January 19, 2021
  • MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI KIFUA KIKUU NA UKOMA WADHAMIRIA KUZIFIKIA KATA ZOTE TABORA MANISPAA

    December 18, 2020
  • MSTAHIKI MEYA TABORA MANISPAA AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA VILEO

    December 17, 2020
  • Angalia Zote

Video

MSTAHIKI MEYA BW. RAMADHAN KAPELA - UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NA UWEKEZAJI KATIKA MANISPAA YA TABORA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA
  • Taarifa Mbalimbali
  • Fomu ya maombi ya Leseni
  • Jarida 2020
  • Taarifa kwa Umma
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Manispaa Tabora - Barabara ya Boma

    Anwani ya Posta: S.L.P 174 Tabora

    Simu ya Ofisi: 026-2604315/6088

    Simu ya Mkononi: 0786820518

    Barua Pepe: md@taboramc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.