• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Fursa za Uwekezaji


1.0 UTANGULIZI:

Chimbuko la  Mji wa Tabora ulianzishwa katika nusu ya kwanza ya karne ya 19 na wafanyabiashara wa-Kiarabu na wa-Kiswahili kutoka Zanzibar. Waliutumia mji huu kama kituo cha njia ya biashara kati ya Pwani na Ziwa Tanganyika. Biashara kuu ilikuwa ni ya Pembe za Ndovu na Utumwa.

Mji   wa Tabora ni moja ya miji inayokuwa kwa kasi katika Tanzania, Tabora ipo katikati ya ukanda wa Magharibi na hivyo kuufanya mji huu kuwa na uwezekano wa kuuza bidhaa zake katika Mikoa ya Kigoma, Rukwa, Singida, na Shinyanga, hivyo mji wa Tabora  ni kitovu cha uchumi katika kanda ya Magharibi. Aidha kuwepo kwa station kubwa ya reli kutoka Mwanza, Kigoma, Mpanda na Dar es salaam ambayo iko sambamba na barabara  zinazounganisha mji huu na Miji ya Kigoma, Mpanda, Dodoma, Shinyanga na Mbeya kunadhihirisha kuwa Tabora iliwekwa ili kuwa kitovu cha biashara katika Kanda ya Magharibi na kuwa kiunganishi kati ya Kanda ya juu kusini kunakolimwa mazao ya chakula kwa wingi na Kanda ya ziwa ukanda wa wafugaji.

Hata hivyo, Serikali ya Jamuhuri ya Mungano ya Tanzania imetambua umuhimu wa Mji wa Tabora, kwa kuwa tayari imeweka  mipango yake mikubwa katika Mkoa kwa kuboresha miundombinu ya barabara na uwanja wa ndege pamoja na kukubali kuanzisha vyuo vya elimu ya juu  na ya Kati, vitu vyote hivi vinaufanya mji wa  Tabora kuwa ni sehemu bora ya kuwekeza katika ukanda huu wa Magharibi mwa Tanzania

Kuwepo kwa wawekezaji wa viwanda katika Mji wa Tabora kutaongeza ajira, kutakuza viwanda vidogo vya kusindika na kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa katika mkoa wa Tabora na Mikoa jirani. Aidha, kutakuza soko la mazao yanayozalishwa katika Vijiji vya Mkoa huu na hatimaye kupunguza umaskini uliokithiri.


2.0 FURSA ZILIZOPO KATIKA MJI WA TABORA

  • Fursa  ya kuweka viwanda vya kusindika asali na Nta (Honey and beeswax  processing). 

Mji wa Tabora  ni Makao Makuu ya Mkoa wa Tabora na upo katikati ya Wilaya nyingine. Mkoa una zaidi ya mizinga milliom 3 ambayo inazalisha 50% ya asali yote inayozalishwa Tanzania, lakini hakuna kiwanda kikubwa cha kusinda asali na nta.

Kwa kuwa mji wa Tabora ni kitovu cha uchumi na biashara katika Mkoa kuna fursa kubwa ya kuwekeza viwanda vya kusindika asali na anta ili kuongeza thamani ya asali na kipato cha wafugaji. Kwa takwimu zilizopo Mkoa una uwezo wa kuzalisha tani 21,000 kwa mwaka.

Aidha, asali kutoka Tabora inauzwa Dar es salaam, Arusha na Nairobi ambako kuna viwanda na hivyo kuwakosesha wananchi wa Tabora ajira na kipato.


  • Fursa ya kuweka viwanda vya kusindika mafuta ya Alizeti na karanga

Mafuta ya alizeti na karanga ya napendwa sana na watumiaji kwa sababu  hayana kiasi kikubwa cha chorestrol. Mji wa Tabora tunaagiza mafuta ya kula kwa asilimia 50% ya mahitaji kutoka katika Mikoa ya  Dar es Salaam, Arusha, Singida na Mwanza. Ambapo mahitaji yetu kwa mujibu wa takwimu kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO) kwa  mwaka ni  tani 15,000.

Aidha, Tabora ina ardhi nzuri ambayo inafaa kwa kuzalisha karanga na alizeti. Hivyo, kuna fursa kubwa ya kuwekeza kwenye kilimo cha alizeti na karanga na   kuanzisha viwanda vya kusindika mafuta ya alizeti.


  • Fursa ya kuweka viwanda vya kusindika nyama, ngozi na maziwa

Tabora ni Mkoa wa tatu kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo , lakini cha kusikitisha  kuna kiwanda kimoja cha kusindika maziwa ambacho kinafanya kazi chini ya uwezo wake. Hii inatokana na mitambo kuchoka, pia hakuna kiwanda cha kusindika nyama na ngozi inagawa vitu hivi vinahitajika kwa wingi.


  • Fursa ya kuwekeza katika sekta ya utali

Tabora ni mji wa kihistoria ambao umebahatika kuwa na vivutio vingi vya utalii lakini havijatangazwa ili kujua Tabora kuna vitu gani kama miji mingine. Vivutio hivi ni kama ugalla game reserve, kigozi game reserve, kituo cha makumbusho cha Dr. Livingstone –Kazehil, Kabuli la Mtemi Milambo,  njia ya watumwa, hospitali ya kwanza Tanzania, Boma ambalo lina handaki linalounganisha Boma na Station. Vivutio hivi vinatoa fursa za kujenga hotel za kitalii pamoja na camping lodges.


  • Fursa ya kuwekeza katika viwanda vya kusindika matunda (embe na matunda pori)

Tabora  ni mojawapo ya Mikoa mitano inayozalisha maembe kwa wingi, maembe yanasafirishwa kwenda Dar es salaam, mengi yanaharibika njiani, hivyo kuna umuhimu wa kuwa na kiwanda cha kusindika maembe katika mji wa Tabora.

Hata hivyo kwa kuwa Tabora ipo kwenye ukanda wa misitu ya miombo, kuna matunda mengi yanayozalishwa kwenye misitu ya miombo kama vile ntalali na ntonga ambayo yanatumika kutengenezea wine.


  • Fursa ya kuwekeza katika ujenzi wa supermarket/shopping malls 

Mji wa Tabora ni miongoni mwa miji inayokua kwa kasi kubwa kutokana na kuwepo kwa taasisi mbalimbali. Kwa kipindi cha miaka michache iliyopita idadi ya watu imeongezeka kwa kasi kubwa ya 5% kwa mwaka (Census report, 2012). Sambamba na ongezeko hili la watu pia mahitaji ya vitu muhimu yameongezeka kwa kasi, lakini katika Mji wa Tabora hakuna supermarket kubwa/ shopping mall ambayo inaweza kuwa ni kimbilio la watu wengi.  Hivyo kuna fursa kubwa ya kuwekeza supermarket ndani ya mji wa Tabora.


  • Fursa ya uanzishwaji wa Bandari ya nchi Kavu (Dry port) na Ukanda Maalumu wa Uwekezaji (EPZ and SEZ). 

Mji wa Tabora ni moja ya miji inayokuwa kwa kasi katika Tanzania, Tabora ipo katikati ya ukanda wa Magharibi na hivyo kuufanya mji huu kuwa na uwezekano wa kuuza bidhaa zake katika Mikoa ya Kigoma, Rukwa, Singida, Shinyanga na nchi jirani za Uganda, Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC),Zambia na Malawi. Hivyo mji wa Tabora ni kitovu cha uchumi katika kanda ya Magharibi. Aidha kuwepo kwa station kubwa ya reli kutoka Mwanza, Kigoma, Mpanda na Dar es salaam ambayo iko sambamba na barabara zinazounganisha mji huu na Miji ya Kigoma, Mpanda, Dodoma, Shinyanga na Mbeya kunadhihirisha kuwa Tabora iliwekwa ili kuwa kitovu cha biashara katika Kanda ya Magharibi na kuwa kiunganishi kati ya Kanda ya juu kusini kunakolimwa mazao ya chakula kwa wingi na Kanda ya ziwa ukanda wa wafugaji.Kutokana na hali hiyo kuna mahitaji makubwa ya kuanzisha Bandari ya nchi Kavu na ukanda maalumu wa uwekezaji {Export Processing Zone (EPZ) na Special Economic Zone(SEZ)}

Eneo linalopendekezwa kwa ajili ya Bandari ya nchi Kavu, EPZ na SEZ lipo katika Kata ya Ndevelwa karibu na uwanja wa ndege kandokando ya reli ya kati itokayo Dar es Salaam na kuelekea mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Kigoma na Katavi. Katika eneo hili kutakuwa na eneo la uunganishaji (assembling) wa mitambo mbalimbali ya zana za Kilimo (Matrekta), magari na mashine zingine ili kuondokana na dhana ya Uchumi tegemezi  

                                                                                                                                             

  • Fursa ya kuwekeza katika sekta ya  elimu na afya

Ili kuboresha mazingira mazuri ya uwekezaji, pia tunahitaji kuboresha huduma za jamii. Kuna fursa ya kuwekeza katika sekta ya afya, mbali na Hospitali ya Mkoa hakuna hospitali nyingine ndani ya mji  wa Tabora ambayo inaweza kuwa kimbilio kwa wawekezaji.  Hata hivyo bado kuna fursa kubwa ya kuwekeza kwenye sekta ya elimu hasa katika vyuo vya ufundi na shule za sekondari yenye hadhi ya kimataifa ili kuvutia wawekezaji wakubwa.


  • Fursa ya kuwekeza katika usafiri wa ndani (public transport)

Mji wa Tabora ni miongoni mwa miji mikongwe na na unakua kwa kasi kubwa kutokana na kuwepo kwa taasisi mbalimbali. Kwa kipindi cha miaka michache iliyopita idadi ya watu imeongezeka kwa kasi kubwa ya 5% kwa mwaka (Census report, 2012). Sambamba na ongezeko hili la watu pia mahitaji ya usafari wa daladala yameongezeka kwa kasi. Halmashauri ya Manispaa kwa kushirikiana na SUMATRA wameanzisha njia 12 kwa ajili ya kutoa huduma ya usafiri ndani ya Manispaa ya Tabora. Njia hizi zote hazina magari ya kutoa huduma ya usafiri, badala yake watu wanatumia baiskeli na pikipiki. Hivyo kuna soko kubwa la uhitaji wa usafiri wa daladala ndani ya mji wa Tabora.


  • Fursa ya kuwekeza kiwanda cha kusindika Tumbaku

Tabora ni Mkoa wa kwanza kwa uzalishaji wa zao la tumbaku Tanzania. Zao hili linachangia zaidi ya 50% ya pato la Mkoa. Tumbaku yote inayozalishwa Tabora inapelekwa Morogoro kusindikwa  na hivyo kukosesha mapato na ajira kwa wananchi wa Tabora. Hivyo, katika Mji wa Tabora kuna fursa kubwa ya kuwekeza kiwanda cha kusindika tumbaku ili kuongeza thamani ya zao la tumbaku na kuongeza ajira. Eneo lililopendekezwa kujengwa kiwanda hiki ni nyuma ya milima ya Hardas kata ya Malolo lina ukubwa wa ekari 50.


  • Fursa ya kuwekeza katika ujenzi wa nyumba (real estate development)

Mji wa Tabora ni miongoni mwa miji inayokua kwa kasi kubwa kutokana na kuwepo kwa taasisi mbalimbali. Kwa kipindi cha miaka michache iliyopita idadi ya watu imeongezeka kwa kasi kubwa ya 5% kwa mwaka (Census report, 2012). Sambamba na ongezeko hili la watu pia mahitaji ya nyumba za makazi, biashara na taasisi mbalimbali yameongezeka kwa kasi. Hivyo kuna soko kubwa la uhitaji wa nyumba ndani ya mji wa Tabora.


3.0 MAENEO YALIYOTENGWA KWA AJILI YA UWEKEZAJI

Katika Manispaa ya Tabora kuna maeneo ya aina tatu ya uwekezaji ambayo ni:-

Maeneo ambayo yalitengwa kwa ajili ya viwanda tangu zamani, maeneo haya yapo katika eneo la Kiloleni. Katika eneo hili kuna viwanja ambavyo bado havijaendelezwa na pia kuna viwanda ambavyo mitambo yake ni mibovu. Wamiliki wa viwanda  na viwanja hivi wapo tayari kwa kuingia ubia na wawekezaji wengine. Mfano Tabora Misitu na Tabora Dairies. Eneo hili lina miundombinu yote (umeme, maji, Barabara na reli)

Maeneo mapya yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda na hoteli.

Katika Manispaa ya Tabora maeneo haya yametengwa katika sehemu zifuatazo:


  • Eneo la Viwanda Malolo:

Eneo hili limeandaliwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda vya kati, lina jumla ya viwanja  40 vya wastani wa ekari 3 kwa kila kiwanja.  Katika eneo hili kuna miundombinu ya barabara kuu, Reli na umeme.

Katika eneo hili upimaji bado haujafanyika kwa sababu fidia kwa wananchi wenye mashamba ya asili bado haijatolewa.

Aidha, katika eneo hili tayari kuna mwekezaji mmoja (MIHAN GAS LTD) ambae aligharimia fidia na akapimiwa viwanja  na ameshaanza ujenzi wa kiwanda cha kuchakata gas.


  • Eneo la viwanda Cheyo:

Katika eneo hili limepangwa kwa ajili ya viwanda vya kawaida (Light Industry) na lina ukubwa wa ekari 200, kwa ajili ya kuchakata mazao ya kilimo na mifugo. Katika eneo hili kuna reli na barabara.

Eneo hili bado halijapimwa kwa sababu fidia bado haijatolewa kwa wananchi wenye mashamba ya asili.


  • Eneo la Mjini Kati (Central Area Redevelopment)

Katika eneo hili kuna fursa ya kujenga majengo ya vitega uchumi mfano ofisi, shopping malls, hotel, kwa kushirikiana na wamiliki wa viwanja na majengo yalipo katika eneo hilo. Eneo la mjini kati linaundwa na Kata nne ambazo ni Kanyenye, Chemchem, Gongoni na sehemu ya Kata ya Mbugani.

Hii ni kwa sababu katika eneo hili linatakiwa kujengwa ghorofa 4- 6 ambayo ni fursa kwa taasisi kubwa za uendelezaji majengo kama vile NHC, PSPF, TBA na LAPF. Aidha, Halmashauri kupitia kongamano la uwekezaji katika Mkoa wa Tabora, wananchi wenye viwanja katika eneo la Mjini kati tayari wameshaelimishwa na wapo tayari kuingia ubia na wawekezaji.

Aidha, Manispaa ya Tabora imeainisha eneo linguine kandokando ya Barabara kuu ya Itigi kwa ajili ya kujenga mji wa kisasa wa kibiashara lenye ukubwa wa ekari 100 katika eneo la Inala

.

MAENEO YALIYOTENGWA KWA AJILI YA UWEKEZAJI

No.
ENEO LILILOTENGWA
UKUBWA
MIUNDOMBINU
HALI HALISI
1.
Eneo la viwanda Malolo
Ekari 120
Umeme, barabara na reli
Eneo halijalipwa fidia na kupimwa
2.
Eneo la Viwanda Cheyo
Ekari 200
Barabara na reli
Eneo halijalipwa fidia na kupimwa
3.
Eneo la Viwanda Kiloleni

Maji, Umeme, Barabara na reli
Eneo limepimwa na linamilikiwa na wananchi ambao wapo tayari kuingia ubia na mwekezaji
4.
Eneo la Bandari ya Nchi kavu (Dry Port) na EPZA
Ekari 400
Barabara, reli, Umeme na Uwanja wa ndege
Eneo  halijalipwa fidia na kupimwa
5.
Eneo la Mjini Kati – Mji mkongwe – (Central Business District)
Kata ya Kanyenye, Gongoni na Chemchem
Barabara, Maji, Umeme, na simu
Eneo limepimwa kwa matumizi ya biashara na Taasisi na linamilikiwa na wananchi wako tayari kuingia ubia na wawekezaji
6.
Eneo la Kilimo Mjini (urban agriculture) Ndevelwa
Hekta 131
barabara
Eneo  halijalipwa fidia na kupimwa
7.
Eneo kwa ajili ya Hotel za kisasa – Mawiti na Kidatu na Itetemia
Hekta 25
barabara
Eneo  halijalipwa fidia na kupimwa





8.
Maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya Viwanda vidogo vidogo/Informal Sector

Ipuli Block D
Ipuli Block F
Usule Block C
Mawiti Block A
Maeneo haya yamepimwa.



4.0 HATUA ZINAZOFANYWA NA SERIKALI KUVUTIA WAWEKEZAJI TABORA.

Halmashauri kwa kushirikiana na Serikali kuu imefanya jitihada zifuatazo ili kuboresha mazingira ya uwekezaji Tabora kama ifuatavyo:-

Kukamilisha ujenzi wa barabara za lami zinazounganisha Mji wa Tabora na Mikoa jirani

Kukamilisha ujenzi wa uwanja wa ndege

Umbembuzi yakinifu na Usanifu wa kina unaendelea ili kufikisha maji ya ziwa Victoria Mkoani Tabora.

Ukarabati wa mfumo wa maji ya bomba wa zamani ili kuongeza uzalishaji wake.

Kuweka mkongo wa Taifa wa mawasiliano ili kurahizisha mtandao wa mawasiliano

Kuandaa Mwongozo wa uwekezaji katika Mkoa wa Tabora na umekamilika

Kutangaza  fursa za uwekezaji  zilizopo kupitia kongamano la uwekezaji  ambalo lilifanyika Dar es salaam tarehe 19/07/2013 na kufuatiwa na kongamano la uwekezaji (Economic Forum) la tarehe 19/08/2015 ambalo lilifanyika Tabora.


Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2022 January 29, 2023
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA TULI KATA YA IFUCHA - INALA July 25, 2022
  • TANGAZO KWA WANANCHI NA TAASISI WALIOOMBA VIWANJA KATIKA ENEO LA INALA - TULI August 17, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023 - HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA December 14, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA LAAC YAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UJENZI WA MIRADI MIZURI NA UTOAJI WA MIKOPO YA 10% YENYE TIJA

    March 17, 2023
  • DC BURA AWAAGIZA WATENDAJI KATA KUONGEZA NGUVU NA HAMASA KATIKA KUSIMAMIA VIASHIRIA VYA LISHE

    February 15, 2023
  • MANISPAA YA TABORA YATOA MIKOPO YA FEDHA KIASI CHA MILIONI 437,300,000/= KWA VIKUNDI VYA VIJANA , KINA MAMA NA NA WATU WENYE ULEMAVU

    February 14, 2023
  • WALIMU 1680 WA MANISPAA YA TABORA WAPATA VISHIKWAMBI

    January 24, 2023
  • Angalia Zote

Video

TAARIFA YA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AGOSTI 14, 2022 TABORA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.