• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

Posted on: May 20th, 2025

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela ameeleza kuwa, kila mfanyabiashara awe mkubwa, wa kati na mdogo katika Manispaa ya Tabora anao wajibu wa kulipa ushuru, kodi na tozo mbalimbali zilizopo kwa mujibu wa sheria mama ya Nchi na sheria ndogo ya Halmashauri.

Mhe. Kapela ametoa rai hii leo mei 20, 2025 wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2024/2025, kikao ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora.

Mhe. Kapela ametoa maelezo haya kufuatia baadhi ya wafanyabiashara waliopisha ujenzi wa soko kuu na kuhamishiwa eneo la nyuma ya stendi mpya kugoma kulipa kodi ya pango ya Tsh.50,000/= kwa kibanda na kudai kuwa wao wapo tayari kulipa Tsh.20,000/= kwa kibanda. Mhe. Kapela amefafanua kuwa, kodi ya pango hupangwa kulingana na bei ya soko na kiasi cha elfu hamsini wanachotakiwa kulipa ni kidogo sana ukilinganisha na bei ya soko ya eneo hilo.

Aidha, Mhe. Kapela ameeleza kuwa, Manispaa ya Tabora imepata mwekezaji ambae ameonesha nia ya kuwekeza kiwanda cha mbolea na yuko katika mazungumzo na Serikali na ameongeza kuwa, kuna mwekezaji mwingine anaetaka kuwekeza kwenye kiwanda cha kusindika viazi vitamu, hivyo Manispaa ya Tabora itapiga hatua kubwa sana kwa uwekezaji huu.

Kadhalika katika Baraza hili, wajumbe na waalikwa wamepata fursa ya kupata elimu ya BIMA YA AFYA KWA WOTE kutoka kwa Meneja wa NHIF Mkoa wa Tabora Ndugu Salum Adamu.

Ndugu Adam ameeleza kuwa, Serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha kuwa Watanzania wote wanapata haki ya kupata matibabu, imekuja na mpango thabiti wa utekelezaji wa ajenda hiyo, ambao ni BIMA YA AFYA KWA WOTE.

Ameeleza kuwa bima hii inatolewa kwa kaya ambapo Baba, Mama na watoto wanne watapata bima hii kwa kiasi cha Tsh. 150,000.00 kwa mwaka mzima, na mtu mwenye bima hii ana nafasi ya kitibiwa kwenye vituo vyote vya kutolea huduma vya umma na binafsi, tena kwa ngazi zote kwa maana ya ngazi ya kituo cha afya hadi Hospitali ya rufaa ya Taifa.

Ndugu Adam ameeleza kuwa, kwa sasa wakazi wa Mkoa wa Tabora bado wanachangamoto ya kukata bima pindi wanapata shida ya kuumwa, jambo linalokwenda kinyume na sera ya bima ambayo inataka Wananchi wote wakate bima, ili iwe rahisi kumhudumia mwenye uhitaji kwa urahisi na haraka.

 Ndugu Elias Kayandabila, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora ameeleza kupokea maelekezo na ushauri wa wajumbe wa Baraza la Madiwani, lakini pia ameungana na Meneja wa NHIF Mkoa wa Tabora kuwataka Wakazi wa Manispaa ya Tabora kukata bima hii “BIMA YA AFYA KWA WOTE”, kwani maradhi yanamkuta mtu mwenye kipato hata cha chini, tena akiwa hajajipanga, hivyo bima hii ni mkombozi wa wanyonge

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.