• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

CHIFU FUNDIKIRA AONGOZA MAMIA YA WAKAZI WA TABORA KUMUOMBEA DUA RAIS SAMIA

Posted on: July 12th, 2025

Na Alex Siriyako:

Chifu Msagata Fundikira, Mtemi wa Unyanyembe ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Machifu Tanzania ameongoza mamia ya wakazi wa Manispaa ya Tabora kumuombea Dua maalumu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan.

Dua hii maalumu imesomwa leo Julai 12, katika viwanja vya Ikulu ya Unyanyembe na kuhudhuriwa na viongozi wa madhehebu mbalimbali, viongozi wa Chama, Machifu wa Mkoa wa Tabora, Viongozi wa makundi maalumu, pamoja na Wakazi wa Manispaa ya Tabora.

Chifu Fundikira ameeleza kuwa, Tanzania ni Nchi yenye amani, na amani hii inadumishwa na Wananchi kwa kushirikiana na Viongozi wetu, hivyo kwa kutambua kuwa tunaelekea kwenye chaguzi za kuwapata viongozi wetu ifikapo Oktoba mwaka huu, Rais wetu kama kiongozi Mkuu wa Nchi anakabiliwa na jukumu kubwa, na hivyo kuna haja ya kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ampe afya njema, hekima na busara, ili aweze kutuvusha salama katika kipindi hiki.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Dkt.John Mboya, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Ndugu Paul Chacha, amemshukuru sana Chifu Fundikira kwa kuandaa Dua maalumu ya kumuombea Kiongozi wetu Mkuu wa Nchi, kwani mzigo alionao ni mkubwa sana, kama Watanzania tuna wajibu wa kumuombea kwa Mwenyezi Mungu.

Aidha, Dkt.Mboya amewaasa Watanzania kudumisha amani na upendo hasa kwenye nyakati hizi za uchaguzi, na ameongeza kuwa madhara yatokanayo na uvunjifu wa amani sio lazima yafundishwe shuleni, tunaweza kujifunza kwa Nchi jirani ambazo amani imetoweka.

Vilevile Dkt.Mboya amewaomba Wananchi wajitokeze kwa wingi kupiga kura ifikapo Oktoba mwaka huu, watumie haki zao za kikatiba kuwachagua viongozi wanaowapenda kwa ngazi za Rais, Wabunge na Madiwani.

Dkt.Mboya ametanabaisha vilevile kazi kubwa ya kuleta maendeleo kwa Wananchi ambayo imefanywa na Serikali ya awamu ya sita katika sekta za afya, elimu, kilimo,mifugo, pamoja na miundombinu ya barabara na maji.

Katika kuhitimisha ujumbe wake, Dkt.Mboya ameahidi kufikisha ombi la wakazi wa Tabora kwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibari Mhe.Hussein Mwinyi, ombi la kuukarabati uwanja wa Ali-Hassan Mwinyi, ikiwa ni ishara ya kuendelea kumuenzi Hayati Ali-Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya pili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Aidha, Dkt.John Pima, Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kwa upande wake ameungana na viongozi wengine kuishukuru familia ya Chifu Fundikira kwa kuandaa Dua hii maalumu, na ametumia fursa hiyo kuwaomba viongozi na Wananchi wa Tabora wampe ushirikiano, ili kwa pamoja waweze kuendelea kuchagiza maendeleo ya Tabora na Tanzania kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 30, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA ZA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 July 03, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • DC WELLA AWATUNUKU VYETI WALIMU WALIOFANYA VIZURI KITAIFA

    July 26, 2025
  • CHIFU FUNDIKIRA AONGOZA MAMIA YA WAKAZI WA TABORA KUMUOMBEA DUA RAIS SAMIA

    July 12, 2025
  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.