• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

UBORESHAJI WA MAJARIBIO (PILOT) WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KWA KUTUMIA TEKNOLOJIA YA ‘BIOMETRIC VOTER’S REGISTRATION (BVR) KUANZIA TAREHE 24/11/2023 HADI 30/11/2023 KATIKA KATA YA NG’AMBO

20 November 2023

Tume ya Taifa ya Uchaguzi inawatangazia wananchi wote wa Kata ya Ng’ambo iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mkoa wa Tabora kuwa, Uboreshaji wa Majaribio (PILOT) wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utafanyika kwa siku saba kwa kila kituo.

Uboreshaji wa majaribio utaanza siku ya Ijumaa tarehe 24 hadi Alhamisi tarehe 30 Novemba, 2023 katika vituo vitakavyoainishwa na Tume.  Vituo hivyo vitafunguliwa kuanzia saa mbili kamili (02:00) asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili kamili (12:00) jioni.

UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA UTAHUSISHA MAMBO YAFUATAYO:-

Kuandikisha wapiga kura wapya waliotimiza umri wa Miaka 18   ambao ni raia wa Tanzania kwa mujibu wa sheria.

Kuandikisha wapiga kura ambao watakuwa wametimiza umri wa miaka 18 ifikapo uchaguzi Mkuu 2025.

Kuandikisha wale ambao wanazo sifa lakini hawakujiandikisha hapo awali.

Kuboresha taarifa za wapiga kura waliohama Kata au Majimbo yao ya Uchaguzi au ambao taarifa zao zilikosewa hapo awali Mf. Majina.

Kwa wale wapiga kura wanaotaka kuboresha taarifa binafsi na wanaohama vituo au vyote viwili kwa wakati mmoja wanaweza pia kuanzisha mchakato wa kuboresha taarifa zao kwa kwa njia ya mfumo wa mtandao ‘online’.  Mfumo huu wa kuboresha taarifa za mpiga kura unapatikana katika mtandao wa Tume - www.nec.go.tz kwa kutumia kompyuta au simu janja kisha atabonyeza kiunganishi (link) iliyoandikwa Boresha Taarifa za Mpiga Kura au atatumia anuani ya ovrs.nec.go.tz itakayompeleka moja kwa moja kuanzisha mchakato huo. Katika mfumo huu, wapiga kura wanatakiwa kuingiza namba ya kitambulisho cha taifa (NIN), namba ya kadi ya mpiga kura, namba ya simu anayotumia kwa sasa na jina la kata kisha watapata ujumbe wenye namba ya utambulisho (token namber) ambayo wataenda nayo kituoni ili kukamilisha taratibu za kupata kadi ya mpiga kura.

Kutoa kadi mpya kwa wapiga kura waliopoteza kadi zao au kuharibika.

Kuondoa wapiga kura waliokosa sifa za kuendelea kuwemo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Mfano waliofariki n.k.

 

MAMBO YA KUZINGATIA

  • Mwananchi anatakiwa kupanga mstari akiwa kituoni na kusubiri hadi zamu yake ya jiandikisha itakapowadia. Watu wenye mahitaji maalumu kama vile wazee, wagonjwa, watu wenye ulemavu, wajawazito na akina mama wenye watoto wachanga watakaokuwa nao kituoni watapewa kipaumbele.
  • Mwananchi atakapofika kituoni atachukuliwa alama ya vidole vyote kumi vya mikono yote miwili na kupigwa picha na kisha kupewa kadi yake mpya hapo hapo kituoni.

Zoezi hili la uboreshaji wa majaribio litafanyika pia katika Kata ya Ikoma iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Rorya mkoani Mara.

  • Kwa Mpiga Kura aliyeboresha taarifa zake mtandaoni ni muhimu akahifadhi vyema namba ya kumbukumbu (token) ili iweze kumsaidia kupata kadi yake anapokwenda katika kituo cha kujiandikisha.

 

Tumia haki yako ya msingi kwa kwenda kujiandikisha.


Tangazo Hili Limetolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi S. L. P 358, DODOMA

Tel. +255 26 2323201 - 7. Nukushi: . +255 26 2323208. Barua Pepe: info@nec.go.tz, uchaguzi@nec.go.tz. 

Tovuti: www.nec.go.tz. NEC ONLINE TV- TANZANIA,                                                                                                                                 

Facebook  - https://www.facebook.com/nec.tanzania.39 ,                                                                      

 Instagram - https://www.instagram.com/tumeyauchaguzi_tanzania/,                                                           

Twitter     - https://www.twitter.com/tumeyauchaguzi_tanzania,                                                                   

NEC APP - http://mobileapp.nec.go.tz, 

NEC BLOG - www.blog.nec.go.tz.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.