• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

Posted on: January 9th, 2025

Na. Alex Siriyako:

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tabora ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu Mohamed Katete imeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ikiwa ni sambamba na ubora wa miradi hii katika Wilaya ya Tabora.

Kamati hii ya siasa imefanya ziara leo Januari 9, 2025 ya kutembelea na kukagua ubora  wa miradi ya kimkakati katika sekta mtambuka Wilayani hapa, ambapo miradi kama Ujenzi wa Reli ya mwendokasi (SGR) kipande cha Makutupola, Singida hadi Tabora, Hospitali ya Manispaa ya Tabora, Ujenzi wa Uzio , Jengo la abiria na Maegesho ya magari katika Uwanja wa ndege Tabora, Shule ya Sekondari Malolo pamoja na Ujenzi wa Bwawa la Iyombo kijiji cha Tumbi.

Ndugu Katete kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Tabora amemshukuru sana Mwenyekiti wa chama hicho Taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi sana kwenye miradi ya maendeleo hasa sekta za Elimu, Afya ,Kilimo, pamoja na miundombinu ya barabara na Reli, ambapo wananchi wamesogezewa huduma pamoja na fursa za ajira kuongezeka.

Ndugu Katete amewaomba Wakazi wa Manispaa ya Tabora kuacha kwenda kupanga foleni Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora ( Kitete) kwani Dkt.Samia ameshatujengea Hospitali ya Manispaa ya Tabora ambayo inatoa huduma nyingi sana karibia na huduma zinazotolewa na Kitete,kwani utofauti wake ni mdogo sana, na amemshukuru sana Rais kwa kutenga fedha nyingi kujenga Hospitali hii pamoja na kununua vifaa tiba.

Kwa upande wake katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Tabora Ndugu Daniel Muhina, ameeleza kufurahishwa na ujenzi wa shule ya Sekondari Malolo sambamba na shule zingine za Sekondari Wilayani hapa kama Ifucha na Ntalikwa, aidha amesisitiza kwa niaba ya chama cha Mapinduzi kuwa fedha zilizoletwa kutekeleza miradi hii zitoshe kwa ubora uliokusudiwa, na miradi ikamilike huku wazabuni wote wakiwa wamelipwa.

Aidha wajumbe wa kamati hii wameridhishwa na kasi na ubora wa ujenzi wa uzio, jengo la abiria pamoja na maegesho ya magari katika uwanja wa ndege wa Tabora, ambapo ujenzi wa mradi huu uko mbioni kukamilika.

Kwa niaba ya Serikali, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Deusdedith Katwale, ameeleza kupokea ushauri na maelekezo ya Chama cha Mapinduzi, na ameahidi kupitia taasisi zilizopo chini yake kuwa watahakikisha ushauri huo na maelekezo ya chama yanatekelezwa kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.