• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

Posted on: January 4th, 2025

Na.  Alex SIRIYAKO:

Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imetoa mikopo ya vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu yenye thamani ya Tsh.1,632,818,500/= katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025.

Mikopo hii imetolewa leo Januari 4, 2025 katika viwanja vya Manispaa ya Tabora, ambapo Mgeni rasmi katika Hafla hii alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora Ndugu Deusdedith Katwale ambaye amewakilishwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora Bi. Asha Churu. Hafla hii imehudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwemo Madiwani wa Manispaa ya Tabora, Wakuu wa Divisheni na Vitengo pamoja na wanufaika wa mikopo.

Awali, akitoa taarifa ya uratibu wa mikopo hii, Mkuu wa Divisheni ya Maendeleo ya Jamii katika Manispaa ya Tabora Bi. Tumaini Mgaya ameeleza kuwa, Manispaa ya Tabora ilitenga kiasi cha Tsh.1,632,818,500/= kwa ajili ya mikopo hii ya asilimia kumi kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka wa fedha 2024/2025, fedha ambazo zimekopeshwa kwa jumla ya vikundi mia moja arobaini na nane (148), sawa na asilimia nne (4%) kwa vikundi vya vijana, asilimia nne (4%) kwa vikundi vya wanawake na asilimia mbili (2%) kwa vikundi vya  watu wenye ulemavu.

Aidha, Bi. Tumaini ameongeza kuwa, jumla ya vikundi vilivyoomba mikopo hii vilikuwa 235, ambapo viliomba mikopo yenye thamani ya Tsh. 5,448,487,472/= na kulingana na fedha iliyotegwa kuwa haitoshelezi mahitaji ya vikundi vyote, vikundi vingine vyenye sifa na vile ambavyo havikuwa na sifa vimekosa mkopo huo kwa awamu hii.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora Bi. Asha Churu akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Deusdedith Katwale amewataka wanufaika wa mikopo hii kwenda kuitumia vyema mikopo hii ili iweze kuwainua kutoka hatua waliyonayo sasa na kwenda hatua nyingine ya kiuchumi.

Aidha, Bi. Churu amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kibali cha mikopo hii kutolewa, kwani bila idhini yake vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wa vikundi hivi 148 wasingeweza kupata fedha hizi.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela kwa upande wake amewasisitiza wanufaika wa mikopo hii kuwa mikopo hiyo sio zawadi ama hisani kwao, amefafanua kuwa mikopo hiyo ni mikopo kama ilivyo mikopo ya benki, tofauti yake ni kwamba mikopo hii haina riba na dhamana yake ni nafuu ila urejeshwaji wake ni wa lazima ili vikundi vingine vipate fursa ya kunufaika na mkopo huo.

Ndugu Ramadhani Nassoro ni mlemavu wa ngozi, ambaye amenufaika na mkopo wa milioni 80, ambazo pamoja na mambo mengine, amenunua lori la kubebea madini ujenzi aina ya FUSO FIGHTER, kwa upande wake pia amemshukuru sana Rais Samia kwa kuwapatia mikopo hii na ameahidi kuwa kwa upande wake binafsi anakwenda kupiga kazi na atarejesha mkopo huo kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.