• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

Posted on: April 10th, 2025

Na Alex Siriyako:

Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Bukoba wamekoshwa na mandhari nzuri, iliyopendezeshwa na miti kando kando ya kila barabara, mtandao mkubwa wa barabara za rami, na hali ya usafi katika mji wa Tabora.

Madiwani hawa wa Bukoba wamekiri haya leo Aprili 10, 2025 ambapo wametembelea kwa nia ya kujifunza katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba Mhe. Godson Gypson, Mbunge wa jimbo la Bukoba Mjini Mhe. Steven Byabato pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Erasto Y. Sima.

Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Bukoba wamepata wasaa wa kujifunza namna Manispaa ya Tabora inauweka mji wake katika hali ya usafi, namna Manispaa ya Tabora inakusanya mapato yake ya ndani, na ni mbinu zipi Manispaa ya Tabora inatumia kusimamia miradi yake ya kimkakati hasa miradi ya TACTIC.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Mhe. Byabato amewataka Wataalamu wa Manispaa ya Bukoba kunakili vizuri kila walichojifunza katika Manispaa hii ya Tabora na kueleza kuwa hayo ni maazimio ya ziara hii, na atahakikisha kwamba kila walichojifunza kinafanyiwa kazi.

Kdhalika Meya wa Manispaa ya Bukoba, Mhe. Godson Gypson, amewashukuru Manispaa ya Tabora kwa kukubali kuwapokea na kuwapa uzoefu wa namna wanavyopambana kukusanya mapato yao ya ndani na jinsi wanavyosimamia miradi yao ya TACTIC, aidha amewaomba Madiwani wa Bukoba wawe tayari kuungana na Wataalamu kukusanya mapato saiti bila kudai posho kama madiwani wa Tabora wanavyofanya.

 Baada ya majumuisho ya ziara hii, Naibu Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Idd A. Kalonga, kwa niaba ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhan Kapela, amewashukuru na kuwapongeza Madiwani hawa wa Bukoba kwa kuichagua Tabora kuwa sehemu ya kuja kujifunza, na amewaomba sasa kile walichojifunza waende wakakifanyie kazi na watapata matokeo chanya kama walivyokusudia.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.