• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

Dkt. BATILDA BURIANI AWAASA KINA MAMA KUCHUKUA FOMU NA KUGOMBEA NAFASI YEYOTE YA UONGOZI KATIKA CHAGUZI ZINAZOKUJA HIVI KARIBUNI

Posted on: March 8th, 2024

Na Alex Siriyako:

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Batilda Buriani amewaasa kina mama na vijana wa kike kuchukua fomu za kugombea nafasi yeyote ya uongozi katika chaguzi za Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu, chaguzi zinazotarajiwa kufanyika mwaka huu wa 2024 na 2025.Katika kuwahimiza kwenye hilo,amewakumbusha kuwa toka harakati za uhuru wanawake kama Bibi Titi Mohamed walikuwa mstari wa mbele, hivyo historia inaonesha kuwa wanawake ni viongozi toka kwenye harakati za uhuru.

Dkt.Batilda ametoa nasaha hizi leo Machi 8, 2024 katika viwanja vya majimaji, Wilayani Igunga, Mkoani Tabora wakati akihutubia Wananchi waliofurika viwanja hivyo kuadhimisha siku ya Mwanamke Duniani, maadhimisho ambayo kimkoa yamefanyika wilaya ya Igunga.

Amefafanua kuwa, Tanzania ni miongoni mwa Nchi chache Duniani ambazo zimepiga hatua kubwa ya usawa wa kijinsia, na kuongeza kuwa Tanzania ina Rais Mwanamke, Mawaziri, Viongozi mbalimbali kila sekta, hatua ambayo kuna Nchi nyingi zenye uchumi mkubwa na bado hazijafika hapa Tanzania ilipo.

Aidha Dkt.Batilda ametanabaisha kuwa uchumi wa mwanamke unastawi mahala penye amani, hivyo kama Watanzania hatuna budi kuilinda tunu ya amani tuliyonayo ili tuweze kufanya kazi zetu za kiuchumi vizuri. Ameongeza kuwa Rais Samia anapambana kuimarisha uchumi kwa ngazi zote kwa vitendo, na kwa kinamama na vijana wa Tabora Rais ameahidi kuleta kiwanda cha kutengeneza mizinga ya nyuki ili kupunguza gharama ya sasa ya utengenezaji wa mizinga hiyo kutoka Tsh.120,000/=  hadi Tsh.40,000/= kwa mzinga mmoja.

Katika hotuba yake, Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa Rais Samia katika kuunga mkono uwekezaji  kwa mwanamke na Jmii kwa ujumla, ametoa zaidi ya milioni mia mbili kwaajili ya mafunzo kwa vijana 23 wa Mkoa wa Tabora ili wapate ujuzi wa kuchakata mazao ya pamba na hatimae waweze kutengeneza bidhaa mbalimbali kama nguo na bidhaa zinginezo.

Historia ya Siku ya Mwanamke Duniani  ilianzia mjini New York-Marekani, ambapo wanawake takribani 15,000  waliandamana kudai haki ya ujira mzuri, wapunguziwe muda wa kufanya kazi pamoja na haki ya kupiga kura.  Mwaka 1910 Mwanamama Clara Zetkin  akatoa wazo la kuadhimisha siku hii kuwa ya Kimataifa, na hatimae mwaka 1911 kwa mara ya kwanza, siku hii ya Mwanamke iliadhimishwa Kimataifa kwa mara ya kwanza.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.