• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RC TABORA AWATAKA WATAALAMU KUSAIDIA WALENGWA WA TASAF KUTUMIA FEDHA ZAO KUIBUA MIRADI

Posted on: July 6th, 2021

Na Paul Kasembo-TMC

MKUU  wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Buriani amewaagiza Wataalamu kusaidia katika utoaji wa elimu ya matumizi sahihi ya fedha wanazopatiwa Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (TASAF) ili waweze kuanzisha miradi itakatowaendeleza wenyewe.

Dkt Batilda aliota kauli hiyo wakati wa Kikao kazi cha kujenga uelewa kuhusu kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF na kutoa mwongozo wa utambuzi na uandikishaji wa kaya za walengwa katika eneo la Utekelezaji kwenye Manispaa ya Tabora.

Alisema fedha wanazopata walengwa wanaweza kuzitumia katika shughuli mbalimbali ikiwemo ufugaji wa nyuki, kuku na mifugo mingine ambayo itawakomboa na kuwafanya wapande daraja na kuacha kutegemea ruzuku ya Serikali.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kupitia TASAF kaya zaidi milioni 1 zimenufaika na kufanyakazi za ujasiriamali na kuweza kuendesha maisha yao kwa unafuu ukilinganisha na awali.

Balozi Dkt. Batilda alisema Mkoa wa Tabora unazofursa nyingi kama vile mistu mikubwa , ardhi ya kutoa na mifugo mingi ambapo walengwa wanaweza nao kutumia nafasi hizo kusonga mbele kimaisha.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa aliagiza kufungwa kwa Kamera za ulinzi (CCTV  Camera ) katika maeneo makubwa ya biashara ikiwemo minadani masokoni, na stendi ili kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali yaliyopo Tabora Manispaa.

Alisema sanjari na hilo ni vema Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ikaimarishwa ili kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Balozi Dkt. Batilda alisema katika maeneo ambayo yamefungwa mifumo ya TEHAMA imeonyesha mafanikio makubwa ambapo mapato ya Serikali yapanda mara tatu ya awali.

Awali Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) Emmanuel Macha alisema utambuzi wa awamu utafanywa kwa makini na wahusika watakula kiapo ili kuepuka kuingiza majina ya watu wasiostahi. Halmashauri ya Manispaa ya Tabora itapata nafasi ya kuibua na kuandiskisha walengwa wa Kaya Masikini sana wapya ambao hawakupa nafasi klwenye Tasaf iliyopita

Na MKUU wa Wilaya ya Tabora Dkt.Yahya Nawanda ambaye pia alihudhuria kikao hicho amesema hatasita kuwachukulia hatua za kisheria kwa watu ambao hawana sifa ya kupokea fedha kwa ajili walengwa wa mpango wa kunusuru kaya Maskini (TASAF)

DC Dkt. Nawanda aliota kauli hiyo  wakati wa Kikao kazi cha kujenga uelewa kuhusu kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF na kutoa mwongozo wa utambuzi na uandikishaji wa kaya za walengwa katika eneo la Utekelezaji kwenye Manispaa ya Tabora.

Alisema fedha hizo zinatolewa na Serikali kwa ajili ya kuziwezesha Kaya Maskini ziweze kujikimu katika mahitaji muhimu ikiwemo upatikanaji wa huduma za chakula, elimu , afya ili ziliweze kushiriki vizuri katika shughuli nyingine za maendeleo.

Dkt. Nawanda aliwataka TASAF kushirikiana na Madiwani wa Manispaa ya Tabora wakati wa utambuzi na uandikishaji wa Kaya Maskini ili kuepuka kuwaacha walengwa.

Alisema kitendo cha kuwaacha walengwa kinaweza kusababisha lawama na malalamiko kwa Madiwani ambao ni wawakilishi wa wananchi na wako karibu na wanatambua hali halisi za watu wao.

“Tumieni mbinu shirikishi kuwabaini walengwa ili malalamiko yalipo kwa baadhi ya kaya maskini yasiweze kujirudia tena” Dkt Nawanda alisisitiza.

Kwa upande wa Afisa Mfuatiliaji Manispaa ya Tabora Nisalile Mwaipasi alisema kwamba madiwani wanawajibu mkubwa kuhakikisha wanashirikina ili kuweze kutimiza lengo la serikali ya kutambua kaya masikini .

‘’sisi wote tunajenga nyumba moja hakuna haja ya kugombea fito jambo ambalo litarudisha nyumba malengo ya serikali ‘’alisema Mwaipasi.

 

Mwisho

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.