• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI MKUU AMPONGEZA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TABORA

Posted on: September 8th, 2022

Waziri Mkuu  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Dkt. Peter M. Nyanja kwa usimamizi mzuri wa fedha za miradi ya Serikali.

Mhe. Majaliwa ametoa pongezi hizo katika ziara yake ya  kikazi ya siku mbili Mkoani Tabora ambapo  ambapo alitembelea na kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwamo jingo la Utawala la Manispaa ya Tabora

Aidha Mhe. Majaliwa katika kikao na Viongozi pamoja na Watendaji wa Mkoa wa Tabora amepokea Salamu za Mkoa wa Tabora kutoka kwa Mkuu wa Mkoa Dkt. Batilda Burian  ambapo pamoja na mambo mengine amemshukuru sana Mama yetu Samia Suluhu Hassan kwa upendeleo wake mkubwa kwa Mkoa wa Tabora.

Kwani zaidi ya Bilioni mia moja na kumi (110) zimetumika kwenye miradi ya maendeleo Mkoani Tabora kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na kwa upande wa Manispaa ya Tabora ikipata zaidi ya Bilioni nane (8) kwenye miradi yake maendeleo.

Katika Manispaa ya Tabora Mhe. Majaliwa amepata fursa ya kuongea na Wananchi na Watendaji wa Serikali na kueleza namna gani Serikali ya awamu ya sita imejipanga kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Na baadae amekagua mradi wa Jengo Jipya la Utawala linalojengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu, Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi imara wa Mama Samia Suluhu Hassan jingo ambalo kwa sasa liko hatua ya umaliziaji.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Tabora kuwekeza kwenye miradi yenye tija, ya kimkakati na yenye kuleta matokeo chanya kwa mapato yao ya ndani,kwani miradi mingi inayotekelezwa ni midogomidogo na haina tija sana kwa Halmashauri husika.

Mhe.Kassim Majaliwa amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuongeza tija, ubunifu na mbinu za kukusanya mapato ya ndani ili waweze kutoa huduma bora kwa Wananchi. Vilevile amewataka kufuata sheria na taratibu za matumizi ya fedha hizo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha zinapelekwa kwanza benki ndio zirudi kufanya matumizi.

Aidha katika kipengele cha mapato amesisitiza mawakala wapewe mikataba na ikiwa ni baada ya kufanya tathimini ya kina kwenye vyanzo husika, hii ikiwa ni kuleta ufanisi wa ukusanyaji wa mapato.

Aidha katika hotuba yake Mhe.Kassim Majaliwa amemtaka Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora kuhakikisha fedha zote ambazo hazijaingia kwenye akaunti husika benki katika Halmashauri zote za Mkoa wa Tabora zinapelekwa haraka iwezekanavyo na vinginevyo achukue hatua muhimu ikiwa ni pamoja na kushirikisha vyombo vingine vya Serikali ikiwamo TAKUKURU.

Katika hatua nyingine  Mhe. Majaliwa amemuagiza Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Dkt. John Mbowe kufanya msawazo wa watumishi ndani ya Mkoa wa Tabora ikiwa ni kupambana na uhaba wa Watumishi kwani kuna Halmashauri zingine zinakuwa na watumishi wengi katika kada flani huku Halmashauri nyingine zikiwa na uhaba mkubwa wa watumishi wa kada kam hiyo hiyo.

Waziri Mkuu amewaagiza Meya na Wenyeviti wa Halmashauri wawe wakali kwenye matumizi ya fedha za Halmashauri na wahakikishe taratibu na kanuni zinafuatwa ambapo  ameeleza kwamba Baraza la Madiwani linawajibu wa kuhakikisha kwamba kila shilingi inatumika kulingana na bajeti iliyopangwa na sio vinginevyo, na kuhakikisha kwamba sheria na taratibu zote zinafuatwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Dkt Peter Maiga Nyanja wakati akielezea utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa jingo la utawala amesema  kwamba mpaka sasa jengo linahitaji zaidi ya Bilioni mbili ili kuweza kukamilika kabisa, ambapo Mhe. Majaliwa ameahidi Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaipatia Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Bilioni moja kwa mwaka wa fedha 2022/2023 ili kuendelea kukamilisha jengo hilo kwa sababu Mkurugenzi na Manispaa ameweza kusimamia vyema matumizi ya fedha za awali.

Mwisho kabisa Mhe.Kassim Majaliwa amewashukuru Wananchi wa Tabora kwa mwitikio wao mkubwa kwenye zoezi la Sensa ya Watu na Makazi lakini vilevile kwa ukarimu wao na mapokezi makubwa wakati alipokuja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe. Samia Suluhu Hassan na kusisitiza kwamba upendo wa watu wa Tabora unawapa nguvu wao kama Viongozi wa Serikali.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.