• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WAZIRI JAFO AKAGUA NA KURIDHISHWA NA UJENZI WA BARABARA ZA LAMI KM 21.3 TABORA MANISPAA

Posted on: June 6th, 2020

Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemeni Jafo (MB) ametembelea na kukagua ujenzi wa barabara za Lami zenye urefu wa KM 21.3

Katika ziara hiyo Mhe Waziri alikuwa ameongozana na Mwenyekiti wa Bodi ya TARURA TANZANIA, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri, Mbunge wa Tabora Mjini Mhe Adamson Mwakasaka, Viongozi mbali mbali wa Manispaa ya Tabora ambapo walitembelea na kukagua ujenzi wa mtandao wa barabara kwa kiwango cha Lami na kuridhishwa kwa namna ambavyo ujenzi huo ulivyofanyika na viwango vyake.

''Nimekuwa ziarani kwa siku sita sasa, nimetembelea na kukagua miradi yote ambayo ipo chini ya Wizara yangu ya TAMISEMI kwa mikoa saba ikiwemo na Tabora kwenye Manispaa yenu ya Tabora ambapo nimekagua na kuridhishwa sana na mradi huu wa ujenzi wa barabara KM 21.3 kwa kiwango cha Lami, huu ni moja ya mradi uliotumia fedha nyingi sana chini ya Mradi wa Kimkakati wa Uimarishaji Halmashauri za Miji na Manispaa (ULGSP) hakika nimeridhishwa HONGERENI SANA MANISPAA YA TABORA,'' alisema Mhe Jafo.

Waziri Jafo alisema kuwa yote hayo ni matokeo na matunda ya kazi kubwa inayofanywa na Mhe John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Tanzania kwa wananchi wake, na kwamba hawakukosea kumchagua Mhe Rais, kwa msingi huo kuna kila sababu ya kumshukuru Mhe Rais wetu.

Aidha katika hatua nyingine Mhe Jafo aliwaambia wananchi wa Manispaa ya Tabora waliokuwa wakimsikiliza kwenye mkutano huo wa hadhara kwamba, kupitia Mbunge wa Tabora Mjini Mhe Mwakasaka na baadhi ya Waheshimiwa Madiwani walienda kumfuata Ofisini kwake Dodoma na kumuomba fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambapo aliwaahidi kuwapatia kiasi cha Shilingi Bilioni Moja.

Kwa upande wa Elimu, Mhe Jafo aliwaeleza wananchi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ilitoa kiasi cha Bilioni 89 kwa ajili ya ukarabati wa shule kongwe Nchi nzima zikiwemo na shule za Tabora Wavulana, Milambo Wavulana na Kazima Sekondari zote hizi zipo hapa Tabora Manispaa.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa ULGSP, Meneja wa TARURA Tabora Manispaa Mhandisi Edwin Kabwoto alimueleza kuwa Mradi huo wa Ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha Lami nene umejengwa kwa awamu tatu tofauti (Three phases).

Ambapo awamu ya kwanza (LOT 1 sawa KM 6.1 ujenzi) ulifanyika chini ya ya Mkandarasi M/S SALUM MOTORS TRANSPORT Co LTD na ANAM ROAD WORKS Co Ltd, awamu yapili (LOT 2  sawa na KM 9.23) Mkandarasi alikuwa M/S SALUM MOTORS Co LTD na ANAM ROAD WORKS Co Ltd na awamu ya tatu (LOT 3 sawa na KM 6.02) Mkandarasi alikuwa ni CHONQING International Construction Corporation (CICO) na hivyo kukamilisha ujenzi wa barabara yenye urefu wa KM 21.3

 Kukamilika kwa mradi huu katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kumeongeza tija katika uzalishaji, usafirishaji wa bidhaa na abiria kutoka eneo moja kwenda lingine pia umesaidia kuboresha muonekano wa Mji na kuongezeka kwa thamani ya maeneo yaliyokaribu na barabara hizo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.