• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WANANCHI WA KATA ZA UYUI NA TUMBI MANISPAA YA TABORA KUNUFAIKA NA UJENZI WA MADARASA YA KIDATO CHA TANO NA SITA

Posted on: September 25th, 2019


Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini Komanya Kitwala leo tarehe 25/9/2019 amefanya ziara kwenye shule za Sekondari za NKUMBA iliyopo Kata ya Uyui na Sekondari ya CHANG’A iliyopo Kata ya Tumbi kwa ajili ya kukagua maeneo yatakayo jengwa madarasa ya kidato cha tano na sita ifakapo 2020.

 Akizungumza wakati wa ziara hiyo kwenye Shule ya Sekondari NKUMBA  aliwaambia walimu, wajumbe wa bodi ya shule pamoja na wataalamu wa Elimu aliokuwa ameongozana nao kuwa, amekwenda kuangalia na kujiridhisha eneo litakalojengwa madarasa kwa ajili ya kidato cha tano na sita na mabweni mawili kwa ajili ya watoto wa kike.

 ‘’Ninao mpango mkubwa wa kufanya mapinduzi makubwa ya kielimu kwa Manispaa ya Tabora ikiwa ni sehemu ya ahadi yangu tangu nilipofika hapa Manispaa ya Tabora kwamba nitahakikisha naanzisha kidato cha tano na sita Shule mbili za NKUMBA na CHANG’A  chini ya usimamizi wangu kama Mkuu wa Wilaya ili niweze kumsaidia Mhe Rais Dk John Pombe Magufuli kwenye adhima yake ya kuinua Elimu nchini kama alivyoahidi akiinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi 2015/2020, kwahiyo Shule ya Sekondari NKUMBA ndiyo naanza nayo’’ alisema Komanya.

 Aidha Komanya alitumia fulsa hiyo kuwaagiza Wakuu wa Shule zote zilizopo Manispaa ya Tabora kuhakikisha wanapanda miti kwenye maeneo yote ya shule zao kuonyesha mipaka ya shule, kwa kufanya hivyo kutasiadia sana kuzuia wavamizi wa maeneo ya shule na kuepuka migogoro ya ardhi isiyokuwa ya lazima.

 Pia akamugiza Afisa Elimu Sekondari Manispaa ndugu Chatta Luleka kuhakikisha anapeleka wataalamu wa ardhi ili wapime na kuainisha ukubwa halisi wa maeneo ya shule hizo mbili kabla ya kuanza kujengwa hayo madarasa.

 Kwa upande wake Chatta Luleka amabae ndiye Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Tabora, alimshukuru sana Mkuu wa Wilaya kwa namna ambavyo amekuwa na maono yenye tija na afya sana kwa wakazi wa Manispaa ya Tabora hasa kwakuwa amekuwa mbunifu na msimamizi mzuri sana kwenye kuinua Elimu kwa Manispaa ya Tabora. Na akamuahidi kutekeleza maagizo yote anayoyatoa ili kuifanya Manispaa ya Tabora inakuwa bora zaidi kuliko wakati wowote.

 Kuanzishwa kwa kidato cha tano na sita katika shule hizo za NKUMBA na CHANG’A kutakuwa ni mkombozi sana kielimu kwakuwa hapakuwahi kuwa na High School tangu kuazishwa kwa shule hizo. Ambapo Shule ya Sekondari Chang’a kutakuwa na michepuo  miwili ya HGL na HKL, wakati Shule ya Sekondari Nkumba itakuwa na michepuo ya PCB na CBG, na ukizingatia kuwa wanafunzi wamekuwa wakienda umbali mrefu kufuata elimu hasa ya kidato cha tano na sita.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.