• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

BARAZA LA MADIWANI LAISISITIZA MENEJIMENTI KUSIMAMIA NA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO KWA WAKATI NA KUZINGATIA MAELEKEZO YANAYOTOLEWA ILI KUPANDISHA MAPATO YA HALMASHAURI

Posted on: November 13th, 2019

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora wameisisitiza Menejimenti ya Manispaa ya Tabora kuhakikisha kuwa wanatekeleza miradi ya maendeleo iliyowekwa kwenye Halmashauri ili iweze kuongeza mapato ya Halmashauri.

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani kwa robo ya kwanza Julai -Septemba kwa mwaka wa fedha 2019/ 2020 waheshimiwa Madiwani walisema ya kwamba, kumekuwa na utekelezaji wa kusua sua kwenye miradi ya maendeleo hasa ambayo inalengo la kuongeza mapato ya Halmashauri. Jmabo ambalo halikubaliki na kwamba halina afya kwa mustakabali wa mapato ya  Halamashauri kwa ujumla.

Sambamba na hilo, baraza pia lilisisitiza ya kwamba Menejimenti iwe inapkea, zingatia na kutekeleza maelekzo na maagizo yote yanayotolewa ili kuepuka kurudia rudia jambo mara kwa mara kwakuwa hali hiyo inawafanya Waheshimiwa madiwani kukosa imani na Menejimenti kwakuwa kila wanachokuwa wanaagiza na kukubaliana hakitekelezwi kwa wakati unaotakiwa.

Katika mkutano huo wa tarehe 12-13/11/2019  ambao pia ulihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini Komanya Kitwala, pamoja na baadhi ya waalikwa wengine akiwemo Meneja TARURA Manispaa ya Tabora Mhandisi Edwin Kabwoto, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Tabora Mhandisi Seraphine Lyimo, Kamishna Mwandamizi wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Tabora Mabusi Peter wao pia walipata nafasi ya kuelezea kazi zao na mwisho Mkuu wa Wilaya ya Tabora aliongea na baraza la madiwani.

Akiongea kwenye wakati wa mkutano huo wa baraza la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala aliwataka watumishi wa Manispaa ya Tabora kuwa waadlifu, watangulize uzalendo kwanza kwenye kazi zao za kila siku ili waisaidie Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania.

‘’Kumekuwa na sabotage(hujuma) kwa baadhi ya watumishi wasiokuwa waaminifu wa Manispaa ya Tabora ambao wamekuwa wakihujumu juhudi zote zinazofanywa kwa ajili ya kuiletea maendeleo Manispaa, nakuagiza Mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha unakaa na Menejimenti yako yote na kuwaita wale wote wanaosemwa semwa vibaya uzngumze nao na wale wasiostahili uwaondoe kwnye maeneo hayo wanayo lalamikiwa ili wawekwe wengine, alisema Komanya.’’

Komanya alitumia fulsa hiyo pia kumtaka Meneja wa TARURA Manispaa ya Tabora kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora juu ya matumizi sahihi ya barabara hizi za mijini kwakuwa wengi wao hawana uelewa sahihi juu ya namna ya kuzitumia. Pia akamtaka kuwepo na namna nzuri ya ukusanyaji wa mapato yao hasa yale yanayotokana na faini za kuegeshaji mbaya wa gari katikati ya mji, na kuwe na faini ya kufanana siyo mwananchi mwingine atozwe 20,000/ na mwingine atozwe 50,000/ wakati kosa ni la kufanana.

Na kwamba atapaswa kuwa anahudhuria mikutano ya baraza la madiwani kwa ajili ya kwenda kusoma mpango kazi wake wa kila robo ya mwaka. Katika maelekezo yake pia kwa upande wa Waheshimiwa Mdiwani aliwataka kuwa kitu kimoja na kutanguliza uzalendo na maslahi mapana hasa ya linapokuwa limetokea suala linalohusu Manispaa ya Tabora.  

Awali kwa siku ya kwanza Baraza la Madiwani lilipokea na kujadili taarifa mbali mbali za robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2019/2020 zikiwemo za utekelezaji wa Julai – Septemba 2019/2020, ambapo siku ya pili baraza lilipokea na kujadili taarifa mbali mbali za utekelezaji kwa Julai – Septemba 2019/2020   kutoka kwenye Kamati za kudumu za Waheshimiwa Madiwani.

Pamoja na mambo mengine mazuri yanayofanywa na Hamlashauri ya Manispaa ya Tabora, lakini pia Menejimenti iliweza kuibua miradi kadhaa ikiwemo ya ujenzi wa vyumba 24 vya maduka eneo la stendi ya basi, kuweka geti kwenye eneo la kuingilia na kutoka kwa gari ndani ya stendi ya basi, soko jipya la kuteremshia matunda, mazao na mizigo ya jumla eneo la Tambukareli, eneo la kuuzia mbao, furnitures (samani kama vile sofa n.k)  ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza mapato kwa Manispaa ya Tabora.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.