• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WAHESHIMIWA MADIWANI WA MANISPAA YA TABORA WAKAMILISHA ZIARA KATIKA MANISPAA YA SHINYANGA

Posted on: February 5th, 2022

Na Paul Kasembo-Shinyanga.

Ziara ya siku mbili kwa Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Tabora imekamilika leo katika Halmasahuri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kutembea na kuiifunza katika shuguri za uendeshaji wa miradi midogo na ya kati iliyopo katika eneo la Viwandani, uanzishwaji na utunzaji wa dampo lililopo Kazimzumbi Kilomita 6 kutoka Mjini kati, uanzishwaji na uendeshwaji wa machinjio ya kisasa Ndembezi ilyopo Kilomita 5 kutoka Mjini kati.

Akitoa salamu na ujumbe kutoka Manispaa ya Tabora, kaimu Mkurugenzi wan dg Gudu Malulu aliwaeleza wenyeji kuwa lengo la kusafiri kwenda Shinyanga ni kujifunza namna ambavyo wamefanikiwa mambo mbalimbali ka,a yalivyotajwa hapo juu.

”Kwa dhati kabisa tumedhamiria kuja kujiunza na kuchukua yale yote yenye tija kubwa yatokanayo na ziara hii ili yaende kuwa msaada mkubwa kwa Mnaispaa yetu ya Tabora kwa muktadha wa kuipaisha Kiuchumi, kuboresha huduma za jamii, kuongeza na kuimarisha mapato na kimaendel;eo kwa ujumla ili kufikia malengo ambayo Manispaa imejiwekea hasa kwa kip9ndi cha mwaka wa fedha 2022/2023”, alisema Malulu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Ndg Jomaary Satura alisema kuwa ni faraja sana kwa Wana Shinyanga kwa kutembelewa na ugeni kama huo muhimu ja bora zaidi wenye lengo la kuja kujifunza mambo ambayo wameyaona ni mema kwao na yanapatika katika Manispaa ya Sahinyana, na kwamba aliwaahidi ushirikiano wa kutosha zaidi ili waridhike na wapate walichokusudia na kiende kuwa na ,matokeo chanya kwa wananchi wao.

Satura alisema kwamba Shinyanga siyo bora zaidi kukiko Halmashauri zingine, lakini kitendo cha Manispaa ya Tabora kuichagua Shinyanga ni jambo jema na lenye kuketa faraja kubwa sana, na kwamba Manispaa ya Shinyanga itakwenda kujinza pia mambo mazuri kutoka Manispaa ya Tabora.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe Elias Masumbuko, aliwashukuru sana Waheshimiwa Madiwani Kutoka Manispaa ya Tabora kwa kuiona Shinyanga na hata wakaamua kwenda kujifunza, hivyo akawaomba kuwa huru kuuliza, kuhoji, kukosoa na kuboresha pale ambapo wanaona panafaa kwa kusudoo la kuleta tija na kuwahudumia wananchi wa Manispaa ya Shinyanga.

“Siyo kwamba tuu mmekuja kujifunza kutoka kwetu, hapana nasi pia kupitia ujio wenu tutajifunza mambo mengi yaliyomazuri zaidi ambayo mmekuja nayio na huenda sisis hatukuwa nayo pia, ndiyo maana nasema mkosoe, mshauri na mhojinkwa kadiri mtavyoona ili nasi tujikosoe pia,” alisema Meya Masumbuko.

Akifunga ziara hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora, Mhe. Ramadhani Kapela aliwashukuru sana wanaShinyanga kwa ukarimu wao waliowapatia tangu kufika kwao hapo, ushirikiano waliowaptaia kwenye ziara hiyo ya kujifunza mambo mbalimbali na kwamba akwaahidi wajumbe wote kuwa watakwenda kuyafanyia kazi yote yale waliyojifunza ili yakalete mabadiliko chanya zaidi kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora.

 Kukamilika kwa ziara hiyo ya siku mbili katika Manispaa ya Shinyanga, kunatoa fulsa sasa kwa wao Waheshimiwa Madiwani kwenda kuyachakata na kuyabadilisha yale yote waliyojifunza na kuyaona kwenye ziara hiyo ili yakaonekane kwenye madiliko ya vitendo na maisha ya wananchi wao wanaowaongoza kwenye maeneo yao, sambamba na kukuza pato la Manispaa, kuboresha huduma kwa jamii, kuibua na kusimamia mairadi yao wenyewe.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.