• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WAHESHIMIWA MADIWANI WA MANISAPAA YA TABORA WAKAMILISHA ZIARA YA SIKU MBILI KATIKA MANISPAA YA KAHAMA

Posted on: February 3rd, 2022

Na Paul Kasembo.

Waheshimiwa Madiwani kutoka Manispaa ya Tabora walifanya ziara ya siku mbili kwa ajili ya kujifunza namna bora na njia sahihi zenye lengo la kuongeza Ukusanyaji wa Mapato, kuona namna Miradi Mikubwa ya Kiuchumi na Uwezeshaji wa Viwanda katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.

Akizungumza wakati wa ukaribisho wa ziara hiyo, Naibu Meya wa Manispaa ya Kahama Mhe. Sindano Machumu aliwaeleza Waheshimiwa Madiwani kutoka Manispaa ya Tabora wawe huru kuuliza, kuhoji, kukosoa kushauri na kutoa mapendekezo yoyote kwa kadiri watakavyokuwa wameona kwenye ziara hiyo, ikiwa ni sehemu yao pia Kahama kujisahihisha na kujiweka veama zaidi.

“Pamoja na kwamba hapa Kahama tumekuwa tukipokea ugeni mwingi wenye dhamira ya kuja kujifunza mambo mbalimbali, lakini kwa Manispaa ya Tabora tunafurahia zaidi ujio wenu kwani ni jirani zatu, ndugu zetu na wamoja katika kuhudumia jamii zetu amabzo zimepakana, hivyo muwe huru zaidi na tupo tayari kupokea maoni yenu na kuyafanyia kazi tukijuwa nasi tutakuja kujifunza kwenu pia”, Mhe. Machumu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama Ndg Anderson Msumba, alimshukuru sana Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela kwa kwa kushirikiana na Waheshimiwa Madiwani kuichagua Kahama kuwa sehemu ya mafunzo yao, kwakuwa anaamini kuwa ziara hiyo itakuwa na tija kubwa kwao na kwa wananchi wao kwa muktadha mpana wa Manispaa ya Tabora, kisha akawakata kushiriki kikamilifu sasa kwenye ziara.

Pamoja na salamu hizo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama alipata wasaa wa kuelezea namna ambavyo wanatekeleza ukusanyaji wa mapato,uendeshaji wa miradi mikubwa na uwekezaji wa viwanda.

Manispaa ya Kahama imeweza kupiga hatua kubwa sana kwenye kuongeza ukusanyaji wa mapato kwa kuwawezesha kimiundombinu wafanyabiara wadogowadogo (CDT) kwa kuwatengenezea maeneo ya kibiashara bure ikiwa ni pamoja na kuanzisha kituo kidogo cha mabasi, kujenga mabanda ya wauza mitumba.

Kufanya matengenezo makubwa ya miundombinu ya barabara, umeme, maji na mitaro, na kisha kufanya maboresho kwa makubaliano na na wafanyabiashara hao ambao wanaendelea na ujenzi wa vibanda vya biashara kwa uataratibu wa JENGA, TUMIA HAMISHA (Build, Operate and Transfer) gaharama ambazo zinafanywa na mfanyabiarasha mwenyewe baada ya kuwa amewezeshwa na Manispaa kama ilivyoelezwa awali.

”Kwa kufanya hivi peke yake, Kahama inaweza sasa kukusanya mapato yake kwa wingi zaidi kwakuwa imewawezesha wafanyabiashara hao na wao hulipa bila hata tatizo tena kwa wakati bila shuruti yoyote”, alisema Anderson.

Kwa upande wa Miradi Mikubwa ya Kiuchumi na Viwanda, wametenga eneo maalumu (CHAPULWA) ambalo lipo pembezoni kabisa mwa Manispaa ya Kahama, likapimwa, likapatiwa HATI, kulipwa fidia wananchi wa eneo hilo na kisha kuwapatia wawekezaji wakubwa bure kabisa lenye ukubwa wa hekari mia saba.

Kisha Manispaa ikawezesha kupeleka miundombinu yote muhimu ikiwamo, barabara, maji, na baadae wanamalizia na nishati ya umeme, jambo ambalo limewezesha kupatikana kwa wawekezaji wakubwa wa viwanda vya usindikaji mafuta ya kula, utengenezaji wa mabati, mabomba ya maji, uunganishaji wa pikipiki nk.

“Hiyo peke yake kwa kuanzia kunaiwezesha Manispaa ya Kahama kukusanya Service Levy ya kutosha, kuongeza ajira kwa wananchi wa Kahama, kuboresha maisha kiuchumi, kuongeza mzunguuko wafedha ambapo sasa wanakusanya takribani asilimia 16.1 ya bajeti yote ya Manispaa ya Kahama”, alisisitiza Anderson.

Miradi mingine mikubwa ni uanzishwaji wa Eneo la Uwekezaji  Mwendakulima, eneo hilo lina ukubwa wa ekari 170, lipo umbali wa kilomita 6.3 kutoka katikati ya Mji wa Kahama ambapo wanaendesha shughuri za usafirishaji wa mizigo kwenda Tinde, Lusumo, Burundi, DRC Congo, Uganda na Sudani Kusini pamoja na kuanzisha Hotel na Shopping Mall.

Sambamba na hayo pia wanatarajia kuanzisha Soko la Kimataifa la Mazao Busoka am,bapo kutakuwa namashine kubwa za kisasa za kuchambua, kufunga na nafaka na mbogamboga ambapo wapo hatua ya upembuzi. Lengo la mradi huu mkubwa kuwezesha ununuzi wa mazao ya kilimo hasa nafaka mchele/mahindi kwa kujenga soko la ndani na nje hususani nchi za Mzaiwa Makuu  na Sudani Kusini.

Ambapo wataweza kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja, pato la Manispaa, kutoa ajira zaidi ya 6,000, kuwa na soko la uhakika kwa wananchi wao na kuchochea maendeleo ya Sekta zingine.

Akihitimisha ziara hiyo ya siku mbili, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda aliwapongeza sana Kahama kwa juhudi zao na maarifa wanayoyatumia kufanisha shughri za maendeleo, akawashukuru sana kwa ukarimu na ushirikiano waliuwapatia Waheshimiwa Madiwani na kwamba watakwenda kuyatekeleza yote waliyoyaona na kujifunza kutoka Kahama, na mwisho aliwakaribisha Manispaa ya Tabora na wao waje kujifunza.

Kukamilika kwa ziara hii ya siku mbili katika Manispaa ya Kahama kutaleta tija kubwa sana kwenye utekelezaji wa malengo ya Manispaa ya Tabora wenye dhamira ya kuipaisha kiuchumi, kuboresha maisha ya wananchi kwa kuwawezesha na kuongeza mapato kwa ujumla.

MWISHO


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.