• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

WAFANYABIASHARA MKOANI TABORA WAHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA UWEKEZAJI

Posted on: October 25th, 2022

Na Alex Siriyako,

Wafanyabiashara na Wajasiriamali walioko Manispaa ya Tabora na Tanzania kwa ujumla wamehimizwa kuwekeza kwenye fursa za kiuchumi zinazopatikana katika Manispaa ya Tabora. Miongoni mwa fursa za kiuchumi zilizoainishwa ni pamoja na Uwekezaji kwenye Viwanda vikubwa na vidogo, Ujenzi wa Hotel za Kisasa pamoja na Uwekezaji kwenye sekta ya Elimu na afya.

Ujumbe na hamasa hizi zimetolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhan Kapela, akimuwakilisha Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Paul Chacha katika Baraza la Biashara Manispaa ya Tabora. Baraza hili kimsingi huwakutanisha Sikta Binafsi na Sekta ya Umma na kujadili kwa Kina changamoto na fursa zilizopo na kuzipatia ufumbuzi ili kuharakisha maendeleo ya Watanzania.

Katika Baraza hili ambalo limefanyika ukumbi wa Manispaa ya Tabora, baadhi ya Changamoto zimebainishwa mathalani uhaba wa miundombinu kwenye masoko, uchakavu wa miundombinu kwenye machinjio ya Tabora, Bajaji na Bodaboda kutokuwa na vituo maalumu hivyo kuleta usumbufu kwa wateja, Wazabuni wa usafi kutowajibika ipasavyo pamoja na mikopo ya asilimia kumi kutotosheleza mahutahi ya  walengwa.

Mhe. Ramadhan Kapela ametoa ufafanuzi na maagizo kwa Menejimenti ya Manispaa ya Tabora katika kupata ufumbuzi wa changamoto hizo, miongoni mwa maagizo hayo ni pamoja na Watendaji Kata kusimamia ipasavyo Vikundi vya usafi na kukusanya ushuru wa taka ngumu, Jengo la Machinjio likarabatiwe ndani ya mwaka huu wa fedha, na amemtaka Afisa Biashara kuhakikisha miundombinu yote kwenye masoko inafanya kazi.

Aidha Bwana Festo Nashoni, Afisa Biashara wa Manispaa ya Tabora kwa nafasi yake ameeleza kwa kina fursa za uwekezaji katika Manispaa ya Tabora, fursa hizo zikiwa ni pamoja na uwekezaji wa Viwanda vikubwa na Vidogo, Ujenzi wa Hotel na Nyumba za kulala wageni na hii ikichangiwa na ongezeko la wageni wengi kutokana na ujenzi wa Miradi ya Kitaifa ya kimkakati kama Reli ya Kisasa kutoka Makutupora-Singida hadi Tabora.

Bwana Nashoni amedadavua kuwa Manispaa inatarajia vilevile kuwa na Miradi mikubwa ya kimkakati kama ujenzi wa Karakana ya reli ya mwendo kasi, ujenzi wa soko kuu la kisasa, ujenzi wa stendi kubwa ya mabasi , ujenzi wa Kitega Uchumi cha Halmashauri (ppp) pamoja na ujenzi wa Chuo Kikuu cha Teknolojia na Kilimo cha Mwalimu Julius Nyerere.

Aidha katika kuhitimisha, Wajumbe wa Baraza la Biashara waliomba Serikali ione namna ya kuipa Manispaa ya Tabora mahindi kutoka ghara la Taifa ili kupunguza kasi ya njaa  kama ambavyo miji mingine imepewa mahindi hayo.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.