• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

SERIKALI KUU YATUMIA ZAIDI YA ASILIMIA MIA MOJA KUJENGA MIRADI YA MAENDELEO MANISPAA YA TABORA

Posted on: August 14th, 2024

Na Alex Siriyako:

Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imetumia zaidi ya asilimia mia moja na nane katika kujenga miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Serikali Kuu ilitenga bajeti ya maendeleo ya bilioni kumi na mbili (12) katika Manispaa ya Tabora kwa mwaka huo wa fedha, na ikaleta bilioni kumi na tatu (13) ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia zaidi ya nane.

Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imetumia zaidi ya bilioni mbili kutekeleza miradi ya maendeleo kutoka kwenye mapato yake ya ndani, huku wafadhiri nao wakitoa zaidi ya milioni mia nane ambazo kimsingi ni kiwango cha chini ya ahadi zao.

Serikali Kuu imevunja rekodi yake yenyewe kwa kuleta fedha za miradi ya maendeleo kwa zaidi ya asilimia mia moja hasa kwa miaka ya hivi karibuni.

Taarifa hii ya mwaka wa fedha 2023/2024 imetolewa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndugu Elias M. Kayandabila leo Agosti 14,2024 katika kikao cha Baraza la Madiwani cha kufunga mwaka wa fedha 2023/2024, kikao ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora.

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, wameishukuru sana Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi makini wa Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuipendelea Manispaa ya Tabora kwa miradi mingi sana ya maendeleo katika sekta za Afya, Elimu, Kilimo na Mifugo, pamoja na Miundombinu ya Barabara.

Aidha, katika Baraza hili la kumaliza mwaka wa fedha 2023/2024, wajumbe wa baraza wamefanya uchaguzi wa kumpata Naibu Meya wa Manispaa ya Tabora pamoja na wenyeviti wa Kamati za Kudumu kwa mwaka wa fedha 2024/2025 ambapo Mhe. Adam Kalongo, Diwani wa Kata ya Kabila kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) ameibuka mshindi wa kiti cha Naibu Meya.

Aidha Mhe. Zinduna Kisamba, Diwani wa kata ya Tambukareli (CCM) amechaguliwa kuwa Mwenyekiti kamati ya Maadili, Mhe. Elias Ndelemba, Diwani wa Kata ya Tumbi (CCM) amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mipangomiji, Ujenzi na Mazingira, Mhe. Paulo Kananda, Diwani wa Kata ya Mbugani(CCM) amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhan Kapela ameishukuru sana Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa miradi kemkem ya maendeleo, aidha ameendelea kuipongeza Manispaa ya Tabora kwa kukusanya mapato kwa asilimia mia moja mwaka wa fedha 2023/2024, lakini pia amewashukuru Madiwani kwa uchaguzi mzuri, na zaidi ya yote, amewapongeza viongozi waliomaliza muda wao na waliochaguliwa kushika nafasi hizo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.