• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RC TABORA MHE. DKT PHILEMON SENGATI KUZINDUA MWONGOZO WA UWEKEZAJI WA MKOA IFIKAPO 08 MEI, 2021

Posted on: May 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Tabora MHE. DKT PHILEMON SENGATI anatarajiwa kuzindua kitabu cha mwongozo wa wa uwekezaji wa Mkoa wa Tabora tarehe 8 Mei. 2021 hafla ambayo itafanyika kwenye ukumbi wa Mtemi Isike Mwanakiyungi uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ambapo Mgeni rasmi wa tukio atakuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Geofrey Mwambe (MB).

Hayo ameyasema leo kwenye kikao na waandishi wa habari ambapo alikuwa akitoa taarifa kwa umma juu ya uwepo wa tukio hilo muhimu lenye muktadha wa uchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla  ili umma uweze kuelewa na kufuatilia tukio hilo hata kwa kupitia vyombo vya habari.

”Kwa kuwa ninyi ni wadau muhimu sana wa maendeleo katika Mkoa wetu, nimeona ni vema  niwaite hapa ili niwafahamishe kuhusu tukio hilo muhimu kwa uchu,I wa Mkoa wetu na Taifa kwa ujumla ili nanyi kwa kutumia taaluma yenu mtangaze na kuhamasisha wananchi wa Mkoa wa Tabora, na Watanzania wote kufuatilia kwa karibu tukio hilo katika vyombo vya habari,’’ alisema Dkt Sengati.

Dkt Sengati alisema kuwa, umuhimu wa Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa wa Tabora unaelezea fulsa muhimu zilizopo Tabora ili sasa kumrahisishia mwekezaji kufanya maamuzi ya kuwekeza Tabora. Pia itaweza kumsaidia mwananchi kufahamu jinsi ya kunufaika na uwekezaji tarajiwa.

Kwenye kitabu hicho kumeainisha maeneo muhimu ya kiuwekezaji ikiwa ni pamoja na;

  • Hali ya kijiografia, kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutawala ya Mkoa.
  • Sababu za kuweka Tabora.
  • Huduma wezeshi zilizopo kwa ajili ya wawekezaji wa ndani na nje ya Mkoa.
  • Maeneo ya kipaumbele ya kuwekeza katika Mkoa.
  • Miundo mbinu wezeshi iliyopo Tabora.
  • Orodha ya taasisi wezeshi zilizopo kwa ajili ya kurahisisha uwekezaji Tabora.
  • Orodha ya ukubwa wa Ardhi iliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji mbali mbali na uwepo wa Mawasiliano muhimu (simu na barua pepe) kwa ajili ya kutolea ufafanuzi kwa wawekezaji.

Aidha Sengati alikumbusha kwamba, mnamo tarehe 01 Julai, 2020 Tanzania iliingia katika uchumi wa kati ambao msingi wake mkuu ni viwanda , hivyo akawaomba wananchi wote wa ndani na nje yaTanzania kuchangamkia fursa hii ili waweze kujenga viwanda vya kuchakata na kuongeza thamani ya mazao yatokanayo na kilimo, mifugo,nyuki, madini na mazao ya maliasili.

‘’Hadi kufikia tarehe ya leo, maandalizi ya uzinduzi yanaendelea  vizuri, ambapo tumealika wawekezaji wakubwa wa ndani wakiwemo Mohamed Enterprises (MeTL), Azania Group, Bakhresa Group, Kahama Oil Mills na Jambo Group of Companies,” alisema Dkt Sengati.

Dkt. Sengati alitoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Tabora, Taifa na hata Nchi  jirani kujipatia nakala ya kitabu hicho cha mwongozo wa uwekezaji wa Mkoa ambacho kitapatikana bure katika tovuti ya Mkoa wa Tabora mara tu baada ya uzinduzi.

Huu ni muendelezo wa kongamano ambalo lilitangulia mwaka 2018, ambapo mwaka huu kauli mbiu ni ‘’Wekeza Tabora kwa Uchumi wa Kijani”.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.