• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RC TABORA DKT. BATILDA BURIAN AWATAKA WATANZANIA KUUENZI MUUNGANO KWA KUIMARISHA ZAIDI MAHUSIANO YA KIFAMILIA KATI YA WAZAZIBARI NA WATANGANYIKA

Posted on: April 26th, 2023

Na Alex Siriyako:

Dkt. Batilda ameyasema hayo leo Aprili 26, katika kilele cha maadhimisho ya siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo alikuwa Mgeni Rasmi  katika sherehe hizi  ambazo kwa Mkoa wa Tabora zimefanyika katika Viwanja vya Makao makuu ya Brigedi ya Faru, Tabora Mjini.

Dkt. Batilda ameongeza kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar unaimalika siku hadi siku kwani Serikali ya Tanzania katika awamu zote na zaidi katika awamu hii ya sita imechukua hatua nyingi sana muhimu kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye Muungano ambapo hadi sasa changamoto nyingi sana zimefanyiwa kazi.

Aidha Mkuu wa Mkoa amesema kuwa Watanzania ni wamoja na hili linadhihilika kwa muingiliano mkubwa wa kijamii hasa ndoa nyingi sana kati ya Wanzanzibar na Watanzania Bara. Mhe. Batilda ametanabaisha kuwa yeye mwenyewe ni mfano wa ndoa ya Mtanzania Bara na Mzanzibar, hivyo anasema tukiwa na ndoa nyingi sana za aina hii kutakuwa na msingi imara zaidi kwenye Muungano wetu kwani vizazi vya aina hii havina upande wowote zaidi ya kuitwa Watanzania.

Katika hotuba yake Mkuu wa Mkoa wa Tabora amemshukuru sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia S. Hassan kwa kuupatia Mkoa wa Tabora fedha nyingi sana za miradi ya maendeleo hasa katika sekta ya Elimu, Afya, Kilimo pamoja na Miundombinu ya Barabara na Reli.

Vilevile pamoja na mambo mengi aliyosisitiza, Mkuu wa Mkoa amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote Mkoa wa Tabora kuhakikisha kuwa wanaandaa program maalumu ya kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi wa shule kuanzia Awali mpaka Kidato cha Sita anakuwa na mti wake ambao ameupanda mwenyewe na kuutunza.

Maadhimisho ya Sherehe za Muungano katika Mkoa wa Tabora yamefana sana kwa kushuhudia michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, mpira wa wavu, kukimbiza kuku, Mashindano ya Nsha kwa Wanafunzi wa Sekondari, Mashindano ya Kwaya kwa Wanafunzi wa Msingi na Sekondari, Kuvuta Kamba pamoja na Ngoma za asili.

Katika kuhitimisha maadhimisho haya Wakazi wa Manispaa ya Tabora kupitia Mwakilishi wao ambaye ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhan Kapela wamemshukuru sana Mhe. Rais kwa kazi kubwa sana anayofanya kuwatumikia Watanzania na amesema Wanatabora wako naye hatua kwa hatua katika kupigania maendeleo ya Nchi yetu.


MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.