• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RC TABORA AZINDUA RASMI BARAZA LA MADIWANI LA MANISPAA YA TABORA NA KUSISITIZA FEDHA ZA UMMA ZITUMIKE KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA

Posted on: December 8th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt.Phillemon Sengati amezindua rasmi Baraza la Madiwani la Manispaa ya Tabora huku akiwataka kusimamia na kudhibiti matumizi ya fedha za umma ili ziweze kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa ya kuwasaidia ya kupeleka maendeleo kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora.

Alisema fedha zote ni lazima zitumike kwa kuzingatia mipango na bajeti za Halmashauri na Serikali kwa ujumla kupitia Sheria ya Bajeti na ile ya fedha za umma.

Dkt. Sengati alitoa kauli hiyo leo wakati wa uzinduzi wa Baraza jipya la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, baraza amabalo limeketi kwa mara ya kwanza tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2020 ambapo awali lilitanguliwa na uchaguzi wa Naibu Mstahiki Meya, Meya pamoja Wenyeviti wa Kamati za Kudumu.

Alisema Madiwani wanalo jukumu la kuhakikisha kuwa fedha zote zinazoletwa na Serikali kuu na zile walizokusanya zinatumika kwa usahihi na uwazi na kuzipeleka katika shughuli mbalimbali za wananchi.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema hatua hiyo itasaidia kuepuka matumizi yasiyokuwemo katika bajeti waliyopitisha ambayo yanarudisha nyuma maendeleo na kuwasononesha wananchi.

Dkt. Sengati alisema ili kudhibiti ufujaji wa makusanyo ya Halmashauri ni lazima fedha zote zikusanywe kwa kutumia mashine (POS) na kutoa stakabadhi kwa waliotoa fedha.

Aidha Dkt Sengati alipiga marufuku kwa watendaji waliopewa dhamana ya kukusanya mapato kutumia vitabu kuandika kwa mkono wakati wa makusanyo ya mapato ya Halmashauri kwa kuwa njia hiyo ndio inayotumika kuiba fedha za umma kwa kutoa taarifa zisizostahili za ukusanyaji wa fedha.

Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa Madiwani wanalo jukumu la kuhakikisha kuwa hakuna fedha inayotumika kabla ya kupelekwa benki.

Alisema utumiaji wa fedha ambazo hazipita Benki (fedha mbichi) unasababisha kuzalishwa kwa hoja za kiugazi na wakati watendaji wasio waadilifu kutumia nafasi hiyo kuiba fedha za umma.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Madiwani kuhakikisha wanasimamia na kuwahimiza watendaji katika maeneo yao kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato na kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuiwezesha Manispaa ya Tabora kuwa na fedha nyingi zitakasaidia katika shughuli za maendeleo ya wananchi.

Alisema ni lazima wajipange kuhakiksha kuwa ifikapo mwaka 2025 wanakuwa na mapato ambayo watakuwa tena hawategemei fedha za ruzuku kutoka Serikali kuu.

Katika hatua nyingine Madiwani wa Manispaa ya Tabora wamemchagua Diwani wa Kata ya Isevya Mhe. Ramadhani Shabani Kapela kuwa Mstahiki Meya, aidha Baraza lilimchagua Diwani wa Kata ya Chemchem Mhe. Alhaj Kasongo Amrani kuwa Naibu Meya.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.