• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RC AONGOZA WAKAZI WA KIJIJI CHA IGOMBE MANISPAA YA TABORA KUADHIMISHA MIAKA 59 YA UHURU KWA KUPANDA MITI ZAIDI YA 300

Posted on: December 9th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Phillemon Sengati amewaongoza wanakijiji cha Igombe Kata ya Ikomwa kilichopo Manispaa ya Tabora kupanda miti zaidi ya 300 ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 59 ya Uhuru wa Tanzania bara.

Zoezi hilo limefanyika katika eneo la Misitu ya Hifadhi ya Bwawa la Igombe ambacho ni miongoni mwa vyanzo vya maji ya Bwawa la Igombe ambalo litaoa huduma ya maji katika Manispaa ya Tabora.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Sengati ameongoza zoezi hilo leo ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 59 ya uhuru wa Tanzania bara kwa kushiriki shughuli mbalimbali za kijamii.

Akizungumza baada ya kupanda miti kwenye eneo hilo la Hifadhi ambalo limeathiriwa na shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo , uchomaji mkaa na ufugaji aliwataka viongozi wa Wilaya zote kuhakikisha wanafikisha lengo la Kitaifa la kupanda miti milioni 1.5 kila mwaka.

Alisema Ofisi yake itahakikisha inafuatilia ili kupata takwimu sahihi na ikibainika kuwa ipo Wilaya ambayo hakufikia lengo la Kitaifa , hatasita kuwachukulia hatua viongozi hao.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Wakala wa Mistu Tanzania kwa kushirikiana na Mamalaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Tabora (TUWASA), Halmashauri ya Manispaa ya Tabora , Bonde la Tanganyika, Wakala wa Misitu Tabora Mnaispa Manispaa pamoja  na wananchi katika kulinda na kuhakikisha usalama wa Hifadhi ya Mistu ya Igombe kwa ajili ya kuwahakikisha wakazi wa Manispaa ya Tabora uendelevu wa upatikanaji wa maji kutoka Chanzo cha Bwawa la Igombe.

Aliwataka wadau mbalimbali wanaosimamia uhifadhi wa Msitu huo kuendelea kutoa elimu kwa wakazi wanaozunguka maeneo ya Hifadhi ya Msitu huo kuendelea kuulinda na kuwaondoa wavamizi kwa kuzingatia misingi ya Sheria na taratibu.

Katika hatua nyingine Dkt. Sengati alisema wakati wa zoezi la upandaji wa miti ni vema wakapanda miti ya matunda kama vile miembe na mikorosho ili pamoja na kulinda mazingira waweze kupata kipato kutokana na uuzaji wa maembe na korosho.

Alisema mpango wa Mkoa ni kuanzisha mashamba makubwa ya miembe na mikorosha katika eneo la Tura wilayani uyui kwa ajili ya kuwavutia wawekezaji wa viwanda vya kushindika matunda kuchukua na kuanzisha viwanda mkoani Tabora.

Mhifadhi wa Mistu wa Mnaispaa ya Tabora Peter Kisanga alisema Msitu wa Hifadhi wa Bwawa la Igombe una ukubwa wa Hekta 7,501 ni chanzo maji katika Bwawa la Igombe ambalo ndio linatoa huduma kwa wakazi wa Manispaa ya Tabora.

Awali akisoma risala mbele ya Mkuu wa Mkoa, Mhifadhi Misitu Tabora Manispaa Ndg Peter Kisanga aliuomba Uongozi wa Mkoa na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Tabora kushirikiana nao katika kuwaondoa watu ambao wamekuwa wakihatarisha uendelevu wa msitu huo na Bwawa la Igombe kwa kuendelea kilimo katika maeneo ambayo hayatakiwi, uvuvi haramu na ukataji wa magogo na uchomaji wa mkaa.

 Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mazingira Maniispaa ya Tabora Ndg. William Mpangala alimshukuru sana Mkuu wa Mkoa kwa namna ambavyo amekuwa akiongoza , kuelekeza na kushirikikwenye mambo yote yanayohusu Mazingira na kwamba yeye kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mnaispaa ya Tabora watakwenda kuyatekeleza kwa vitendo

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.