• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RAIS SAMIA AFUNGUA RASMI BARABARA YA NYAHUA-CHAYA

Posted on: May 17th, 2022

Na Alex Siriyako,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amefungua rasmi barabara ya Nyahua mpaka Chaya Mkoani Tabora. Barabara hii yenye kiwango cha lami imegharimu zaidi ya Bilioni 123 ikiwan ni kipande kimojawapo katika barabara kuu inayotoka Mkoani Tabora kwenda mpaka Itigi Mkoani Singida. Barabara hii imeweza kujengwa kwa hisani ya Mfuko wa Maendeleo wa Nchi ya Kuwait.

Hafla ya uzinduzi wa barabara hii imeshuhudiwa na Viongozi mbalimbali, Wageni waalikwa pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Tabora hususani Kata ya Tura Wilayani Uyui ambapo zoezi la uzinduzi limefanyika. Miongoni mwa wageni na Viongozi waliohudhuria ni pamoja na Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso, Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait Ndg. Marwan A. Al-Ghanem, Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Tabora, Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Tabora, Wabunge wa Majimbo ya Mkoa wa Tabora, Viongozi wa Dini, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Tabora.

Mhe. Rais amewashukuru sana Wananchi wa Mkoa wa Tabora kwa mapokezi yao mazuri, hii ikiwa ni ziara yake ya kwanza Mkoani Tabora akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Amewashukuru Kuwait kwa mchango wao mkubwa kwa maendeleo ya Tanzania na amewapongeza wadau wote walioshiriki katika mradi huu pamoja na kuahidi kumaliza mapema sana miradi yote iliyoanzishwa Awamu ya Tano.

Mhe. Rais amepokea changamoto mbalimbali za Wilaya ya Uyui na Mkoa wa Tabora kwa Ujumla ikiwa ni pamoja na uhaba wa Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari, Changamoto ya malipo ya Tumbaku kwa Wakulima ambayo hayajalipwa,  Uhaba wa Matundu ya vyoo Mashuleni, Changamoto ya fidia kwa Wakazi ambao maeneo yao yametwaliwa katika ujenzi wa mradi wa kupeleka umeme Mkoani Kigoma kutokea Tabora na kwa ujumla wake ameagiza Mawaziri husika kuzifanyia kazi haraka iwezekanavyo changamoto hizo na pale watakapokwama wamuone.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani katika kutoa Salamu za Wanatabora pamoja na Utambulisho, amemshukuru Mhe. Rais kwa kutupatia fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa muda mfupi sana akiwa madarakani hususani fedha za UVIKO-19, ambapo zimefanikisha ujenzi wa madarasa mengi sana, umaliziaji wa Vyuo Vya VETA pamoja na  Ujenzi wa Miundombinu ya Maji. Mwisho amemhakikishia Mhe. Rais kwamba Tabora tunatambua jitihada zake na tunapambana sana kumuunga mkono katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya Nchi yetu.

Mkurugenzi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait Ndg. Marwan A. Al-Ghanem nae alipata wasaa wa kusalimia Wanatabora na amesema uhusiano kati ya Tanzania na Kuwait kwenye miradi ya maendeleo umeanza zamani sana toka mwaka 1975 na mpaka sasa Serikali ya Kuwait imefadhili  miradi yenye thamani zaidi ya Dola za Marekani Bilioni 285. Ameahidi kuendeleza ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait na amewashukuru wadau wote katika  ujenzi  wa barabara ya Nyahua-Chaya.

 Aidha katika kuhitimisha hotuba yake, Mhe. Rais ametoa maagizo kwa Mawaziri hususani Wziri wa Maji pamoja na TAMISEMI kuhakikisha kwamba tenda zilizobaki katika matumizi ya fedha za UVIKO-19 zimalizike haraka iwezekanavyo na kufika June mwaka huu wawe wamemaliza zoezi hilo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.