• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

RAIS SAMIA ANATAMBUA UMUHIMU WA MICHEZO NCHINI – MAJALIWA

Posted on: August 4th, 2022

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa, amesema Serikali ya Tanzania kupitia kwa Mhe. Rais Samia Sluhu Hassan inatambua umuhimu wa michezo nchini kama moja ya fursa za kiuchumi kwa wanamichezo.


Mhe. Kassim Majaliwa amesema hayo leo Agust 04, 2022 Mjini Tabora, wakati akizungumza katika ufunguzi rasmi wa mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA kwa mwaka 2022 yanayofanyika kitaifa Mkoani Tabora.


Katika hotuba yake Mhe. Waziri Mkuu ameeleza kuwa Rais Samia alikubali Mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA 2022 kufanyiaka kutokana na kutambua umuhimu wa michezo na wanamichezo nchini kwa kuzingatia kuwa michezo ni ajira.


“Rais anatambua na ameahidi kuendelea kuongeza ubora wa miundo mbinu ya michezo mashuleni ili kuzidi kutengeneza mazingira bora ya wanafunzi kushiriki michezo mbalimbali”


“Wanamichezo wameanza kuhamasika kushiriki michezo mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi, na hii yote inachangiwa na nia njema ya serikali katika kukuza na kutangaza michezo kuanzia katika ngazi ya chini” amesisitiza Waziri Mkuu Majaliwa.


Amesema kuwa michezo na sanaa ni ni moja ya stadi muhimu kwa wanafunzi, ndio maana serikali imekuwa ikiwekeza fedha nyingi katika mashindano ya UMITASHUMTA, UMISETA na mashindano ya vyuo vya ualimu ambayo hufanyika kila mwaka.


Ameongeza kuwa serikali itaendelea na mpango wake wa kuboresha michezo mashuleni kwa kuwaajiri waalimu wa michezo ambapo tayari jumla ya waalimu 83 wameshaajiriwa lengo ikiwa na kuzidi kuinua sekta ya michezo nchini.


Awali akimkaribisha Waziriki Mkuu, Naibu Waziri Ofisi ya Rais - TAMISEMI (Elimu) Ernest Silinde alieleza kuwa wanamichezo zaidi ya elfu tatu kutoka mikoa yote nchini wanashiriki katika mashindano ya UMITASHUMTA 2022 Tabora wakiwa wanawakilisha michezo mbalimbali.


Silinde amesema kuwa mipango ya serikali iliyoanza ya kuboresha miundo mbinu ya viwanja mbalimbali vya michezo nchini vikiwepo vile vya mashuleni, inaenda kuibua wanamichezo wengi mahiri watakaliwakilisha vema Taifa kimataifa.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batlida Buriani, ameishukuru Serikali kwa kuuchagua mkoa wa Tabora kuwa mwenyeji wa UMITASHUMTA na UMISSETA kwa mwaka 2022, jambo ambalo amesema limezidi limezidi kuuheshimisha mkoa huo.


Amemualeza Waziri Mkuu kuwa mashindano hayo yameuchangamsha mkoa wa Tabora kibiashara, na kusaidia uchumi wa watu mbalimbali kuongezeka kutoka na huduma zinazotolewa kwa wageni waliokuja kushiriki michezo.


Katika maombi yake kwa waziri Mkuu, Balozi Dkt. Batlida Buriani aliomba michezo hiyo iendelee kuandaliwa Tabora kwa mwaka unaofuata, ombi ambalo waziri mkuu wakati wa kuhitimisha hotuba yake, alisema limekubaliwa hivyo UMITASHUMTA na UMISSETA 2023 itafanyika tena Tabora.


Mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA 2022 yaliyofunguliwa rasmi leo Agust 4,2022 na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, yanasimamiwa na Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Utamaduni, Sanaana Michezo.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.