• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI MHE. ENG. KUNDO MATHEW AHIDI KUBORESHWA KWA MAWASILIANO YA SIMU

Posted on: February 24th, 2022

Na Paul Kasembo - TMC

Naibu Waziri wa Habari, Teknolojia na Mawasiliano Mhe. Eng. Kundo Mathew amefanya ziara katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora na kutoa ahadi ya kuboreshwa kwa huduma ya mawasiliano ya simu kwenye baadhi ya maeneo ambayo yamekuwa na tatizo hilo.

Kauli ya kuboreshwa huduma ilitolewa kwenye Kijiji cha Kipalapala Kata ya Itetemia ambapo pamoja na mmbo mengine, Mhe Kundo alisomewa juu ya kutokuwepo kabisa kwa mawasiliano jambo ambalo limekuwa likihatarisha hata usalama wa enoe hilo sambamba na kusababisha mkwamo kwenye utoaji wa huduma za kijamii.

Awali akifungua mkutano huo wa hadhara Diwani wa Kata ya Itetemia Mhe. Haruna Kulwa alimueleza Naibu Waziri kuwa, eneo hilo limekuwa na tatizo la kutopatikana kwa huduma ya mawasiliano ya simu kwa muda mrefu sana.

Jambo ambalo limepelekea kukosekana kabisa kwa baadhi ya huduma za kijamii na kuhatarisha hata usalama wa eneo lenyewe, hasa pale wanapokuwa na shida ya kuomba hata gari ya wagonjwa, kuomba msaada polisi au kupeana taarifa zozote zile zenye kusudia la tahadhari imekwa ni ngumu sana.

“Suala hili limekuwa la muda mrefu sana Mhe. Naibu Waziri, lakini ujio wako leo huenda kukafungua na kuleta faraja mpya kwa wakzzi wa maeneo haya n vinga vyake, kwakuwa wamesubiria kauli ya Serikali na sasa umefika, nina imani jambo hikli linakwenda kuisha sasa na wananchi watakuwa na amani juu uoatikanaji wa mawasilano”, alisema Diwani Kulwa.

Akimkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda alimueleza Naibu Waziri kuwa, Wilaya ya Tabora imejiweka kikamilifu na wapo tayari kwenye utekelezaji wa zoezi ala Anwani za Makazi.

Ambapo kwa Wilaya kuna Kata zote 29, Mitaa 134 na Vijiji 53 kwakuwa mpaka sasa tayari Wenyeviti wote wamepewa semina elekezi pamoja na Watendaji wao na sasa wanasubirira kuanza kwa kazi ambayo waliahidi kufanya kwa uzalendo mkubwa sana.

“Pamoja na shukurani za kuja kutatua kero ya mawasiliano hapa kwetu, pia nikuahidi Naibu Waziri kuwa sisi Wilaya ya Tabora, tumejipanga vizuri sana kwenda kulitekeleza zoezi hikli kwa usahihim kwa wakati na kwa uzalendo mkubwa ili tuweze kuwa wa mfano kwa Mkoa na Taifa pia”, alisema Dkt. Nawanda.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Ndg Robert Makungu alimshukuru sana Naibu Waziri kwa ujio wake hasa kipindi hiki ambapo kuna zoezi la Anwani za Makazi, na kwamba akamuambia kuwa kwa upande wa Mkoa wameelekeza kuanza kutambuliwa na kuwekwa Anwani za Makazi kwa nyumba za viongozi, na majengo yote ya Serikali na hicho ndiyo kipaumbele cha Serikali ya Mkoa.

Akihitimisha baada ya kutembelea Kata ya Itetemia, Ifucha na Kakola Mhe. Naibu Waziri Mhandisi Kundo aliwaahidi wananchi wa hao kuwa, Serikali ya Awamu ya Sita imekuja na suluhisho la tatizo la mawasiliano, ambapo kupitia yeye Naibu Waziri ameahidi kulifanyia kazi kwa haraka ili wananichi waondokane na shida hiyo iliyowakabiri kwa muda sasa.

 Aidha alitumia fulsa hiyo kuweleza wananchi hao kuwa, ni wakati wao sas kushiriki vema kwenye zoezi la Anwani za Makazi ili waweze pia kutambuliwa na iwe rahisi kwa Serikali kutatua kero changamoto zao na kuwaletea maendeleo.

Baada ya hili tujiandae sasa kuhesabiwa ili Serikali iweze kupanga mipango yake ya kuleta maendeleo  kwa kuzingatia idaidi ya watu wake ambao watakuwa wamehesabiwa, na hilo ndiyonlitakuwa jukumukubwa zaidi la Serikali baada ya ninyi wananchi kuwa mmeshiriki kikamilifu kwenye hayo mambo mawili muhimu.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.