• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MSTAHIKI MEYA, MKURUGENZI NA WADAU WAKUBALIANA MUDA NA MIKAKATI YA KUJENGA MADARASA 69

Posted on: October 5th, 2022

Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Maiga Nyanja akiambatana na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhan Shabani Kapela pamoja na wadau wa ujenzi wa vyumba vya madarasa 69 wamekutana na Wakuu wa Shule za Sekondari hususani Shule ambazo zimepata fedha za madarasa kutoka Serikali kuu kwa ajili ya kuweka mikakati ya kujenga vyumba vya madarasa 69 ya kidato cha kwanza vyenye thamani ya Tzs. 1,380,000,000/= (Bilioni Moja, na Milioni Mia tatu themanini tuu) ikiwa ni mgawo kwa Manispaa ya Tabora ambapo uwiano wa darasa moja kwa milioni ishirini.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa, ambapo kimejumuisha wadau wote  wa Ujenzi wakiwamo Mafundi ujenzi, Wazabuni, Watendaji Kata, Mafundi wa thamani, Wakuu wa Shule ,pamoja na Menejimenti ya Manispaa ya Tabora. Aidha Wadau wamekumbushwa kuwa kufikia January shule zinapofunguliwa watoto wa kidato cha kwanza wanatakiwa kutumia madarasa haya.

Aidha katika kikao kazi hiki, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela  kwa nafasi yake amesisitiza kuwa kila mradi uwe na fundi mmoja, na fundi mmoja asiwe na miradi miwili kwani kufanya hivo kutapunguza kasi ya utekelezaji wa mradi na kuchelewesha kazi.

Vilevile Mstahiki Meya amewataka Watendaji Kata hususani kwenye vikao vyao vya WDC wawahimize Wananchi kushiriki na kuweka nguvu zao kwenye miradi hii kazi ya kuchimba msingi na kuweka kifusi na mawe kwenye msingi iwe sehemu ya nguvu kazi zao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nyanja katika maelekezo yake amewataka Wakuu wa Shule waunde Kamati za ujenzi na ununuzi kwa kufuata miongozo inavyotaka na kusisitiza wanakamati hao pindi wanapopatikana wapewe mafunzo ya kuwawezesha ili wafanye shughuli zao kwa weledi mkubwa.

Dkt. Nyanja amewataka Wakuu wa Shule kuleta taarifa ya utekelezaji kwa kila hatua ya ujenzi kabla ya malipo kufanyika na kuongeza kuwa baada ya hapo atatuma timu yake ya ukaguzi kwenda kukagua ubora wa mradi kwa hatua hiyo lakini vilevile kupata thamani halisi ya malipo yanayoombwa.

Vilevile Mkurugenzi amewaomba Mawakala wa vifaa vya ujenzi wawe waadilifu na wazalendo, wasitumie mwanya huu kupandisha bei za vifaa vya ujenzi hususani saruji, nondo, bati nk ambavyo ndio vifaa muhimu sana kwa ujenzi wa madarasa. Aidha Mkurugenzi ametumia fursa hiyo kuwaomba wazabuni wa madini ya ujenzi kutopandisha bei ya madini hayo kwa kivuli cha ujio wa fedha hizi za madarasa.

Aidha Dkt.Nyanja amewataka mafundi ujenzi kuongeza ubunifu na jitihada katika kazi zao na amesema hategemei kukuta ukuta ama sakafu imepasuka kwa sababu yeyote ile ya kiufundi, huku akiongeza kuwa mafundi milango watumie Mbao kavu za miti migumu lakini vilevile milango na madawati vipigwe Vanishi na Msasa kabla ya kukabidhiwa.

 Katika kuhitimisha kikao kazi hiki, wajumbe wote waliohudhuria wamekubaliana kwa pamoja kuwa ujenzi uanze rasmi mnamo tarehe 16 mwezi October na ukamilike kufikia tarehe 15, mwezi Disemba mwaka huu 2022

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.