• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MKUU WA WILAYA AKUTANA NA WATUMISHI WA HALIMASHAURI NA KUKAGUA BAADHI YA MIRADI

Posted on: June 23rd, 2021

Mkuu wa wilaya ya Tabora, Mheshimiwa Dkt.Yahya Ismail Nawanda akiambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na  Meya wa Manispaa Tabora, amefanya kikao chake cha kwanza na watumishi wote wa Halimashauri ya Manispaa ya Tabora wakiwemo  Makatibu Tarafa.

Katika kikao hicho alipata fursa ya kuwafahamu watumishi waliohudhuria kikao hicho na vilevile Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora aliweza kutoa taaarifa fupi kwa Mkuu wa Wilaya yenye takwimu za idadi ya kata, vijiji, idadi ya wakazi pamoja na vijiji vya wilaya ya Tabora.

Aidha Mustahiki Meya wa Manispaa Tabora alipata fursa ya kuzungumza machache, alimkaribisha sana Mkuu wa Wilaya, na kumhakikishia ushirikiano wa kutosha na kwa muda wote ambao atakuwa anamuhitaji. Vilevile Mustahiki Meya alimuomba Mkuu wa Wilaya kwa nafasi yake atafute mbinu ya kumaliza na kutokomeza hoja ya hati chafu ya Mkaguzi wa hesabu za serikali kwa Manispaa ya Tabora.

Mkuu wa Wilaya ambae amewahi kuwa mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida na Mhadhiri katika chuo kikuu cha Sokoine(SUA), kwa nafasi yake aliwashukuru wenyeji wake kwa kumkaribisha, alimshukuru pia Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kumuamini na kuahidi kwamba hatomuangusha, atatekeleza majukumu yake kwaniaba ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na kutekeleza Ilani ya chama cha Mapinduzi.

Katika hotuba yake fupi, Dkt. Yahaya amewasihi watumishi wa Halimashauru ya Manispaa ya Tabora kuwa wamoja, watiifu, wenye hofu ya Mungu, wenye upendo baina yao na kwa wananchi, wafanye kazi kwa weledi na waogope fedha za umma. Amesisitiza pia kwamba kila mmoja katika jamii ana kipawa chake alichopewa na Mungu ataheshimu mawazo ya kila mtu. Lakini pia amehimiza miradi yote iliyoanzishwa itekelezwe na ikamilike.

Dkt.Yahaya alibainisha vipaumbeele vyake kwa ufupi kwa sasa ambavyo ni pamoja na kusimamia ukusanyaji wa mapato, amesema hawezi kukubaliana na hati chafu kwa Halimashauri anayoiongoza yeye na katika hilo ameahidi kufumua na kuunda upya Idara ya Fedha. Kipaumbele chake kingine ni kutatua kero za wananchi kwani ndio kazi kubwa ya viongozi na watumishi wengine wa umma. Amewataka vilevile kila mtumishi kuwa na mpango kazi wake kwa kila mwezi na wafuge kuku kwa niaba ya kuongeza vipato.

Aidha  Mheshimiwa mkuu wa Wilaya aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya pamoja na Mkurugenzi wa halimashauri ya Manispaa ya Tabora na kwenda kuutembelea na kukagua mradi wa Hospitali ya Wilaya ya Tabora. Alifika na kupewa maelezo mbalimbali ikiwemo thamani ya mradi ambayo utagharimu zaidi ya Bilioni moja na milioni mia nne za kitanzania, ambapo kwa sasa mradi ushatumia zaidi ya milioni mia saba. Vilevile alielezwa kwamba malengo ya Hospitali ni kufikia Mwezi wa nane mwaka huu Idara ya huduma ya wagonjwa wa nje (OPD) ianze kufanya kazi.

Mkuu wa Wilaya alimaliza kwa kumtaka  Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndg. Bosco Nduguru kufuatilia kwa ukaribu na kuhimiza ujenzi uende haraka kwani wananchi wanahitaji huduma na magojwa hayana subira.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.