• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MKUU WA MKOA WA TABORA AFUNGUA MAONESHO YA NANE NANE 2019

Posted on: August 5th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amefungua maonyesho ya nane nane leo tarehe 05-08-2019 kwa kanda ya Magharibi kwa kuwataka wakulima,wafugaji na wavuvi wa kanda ya Magharibi kuhakikisha bidhaa zao wanazoleta kwenye maonyesho hayo ya nane nane zina uhalisia kwa maana ya kwamba ni zile zinazozalishwa na wao wenyewe binafsi au kutoka kwenye vikundi vyao halisi na siyo kununua kutoka masokoni na kuletya hapo kwenye maonesho.

Akiongea kwenye uzinduzi huo mbele ya umati mkubwa uliofurika kwenye viwanja hivyo vya nane nane vilivyopewa jina la FATUMA MWASA vilivyopo Ipuli Manispaa ya Tabora Mkuu wa Mkoa alisema, kwenye maonesho hayo hakuna nafasi ya kudanganya kwamba unaenda kuleta bidhaa zilizozalishwa na watu wengine na kuja nazo ili kuzionyesha katika banda lako,hayo siyo makusudio ya ya maonyesho haya,alisema Mwanri.

Alibainisha kwamba , kama wakulima watafuata maelekezo yote yanayotolewa na wataalam wetu na kuzingatia mbinu za kisasa za kilimo, uvuvi na ufugaji utakuwa ni wenye tija sana na kwamba bidhaa zao zitapendwa sana na kila mtu atakayekuja kutembelea kwenye mabanda yao ataweza kununua na kujifunza pia.

Aidha alitoa agizo kwa maafisa kilimo, mifugo na uvuvi wa kanda ambayo inajumlisha Mikoa ya Kigoma na Tabora kufanya ukaguzi kwenye mabanda yote ili kujiridhisha kama bidhaa zilizopo eneo la maonyesho zinazalishwa na wahusika wenyewe na kuzifanyia tathimini ya kiwango cha ubora unaotakiwa.

Nae mwakilishi wa Wizara ya Kilimo kutoka Makao Makuu ndg Sospeter Wambura alisisitiza kuwa maonyesho ya nane nane mwaka huu yamepewa kauli mbiu inayotaka  Kilimo, Ufugaji na Uvuvi kuwa ni yenye kuleta tija na maendeleo kwa ukuaji wa UCHUMI WA NCHI.

Wambura akawataka wakulima, wafugaji na wavuvi kuwa wabunifu na wazingatie maelekezo ya wataalamu ili waweze kunufaika na utalaamu huo unaotolewa kwao, na waache ujanja ujanja kwenye shughuri zao za uzalishaji wa bidhaa ili waweze kukuza uchumi wao na kwa Taifa pia.

Awali kwenye ufunguzi huo wa maonyesho ya nane nane, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala amabe ndiyo mwenyeji wao alisema kuwa, ushauri na maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wameyachukua na watayafanyia kazi. Aidha aliwataka wakulima, wafugaji na wavuvi pamoja na washiriki wote kuzingatia ushauri unaotolewa na wataalamu ili waweze kunufaika na shughuri zao ili ziwaongezee uchumi wao na Taifa kwa ujumla.

Maonyesho ya nane nane yanayoendelea kwenye viwanja vya Fatuma Mwasa vilivyopo Ipuli Manispaa ya Tabora ambayo mkilele chake kitakuwa tarehe 8/8/2019, yatafungwa na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia mstaafu Emmanuel Maganga.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.