• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MKUU WA MKOA WA KIGOMA AFUNGA MAONESHO YA NANENANE AKIWATAKA MAAFISA KILIMO KWENDA KUTOA ELIMU NA SIYO KUKAA OFISINI

Posted on: August 8th, 2019

Maonesho ya nane nane kwa mwaka 2019 yamefungwa rasmi leo tarehe 8/8/2019 kwenye viwanja vya Fatuma Mwasa hapa Ipuli Manispaa ya Tabora na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Mstaafu Emanuel Maganga huku akiwataka Ofisa Kilimo wote kutokaa ofisini kwao, badala yake waende kutoa elimu kwa wakulima wa vijijini ili waweze kubadilika na kuwa wakulima wa kisasa.

Akizungumza jana wakati wa kufunga maonesho ya nane nane Kanda ya Magharibi yaliyofanyika hapa hapa Manispaa ya Tabora, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma alisema kuwa kutopata elimu ya kutosha kwa wakulima wetu kumechangia sana kutofanya vizuri hasa kwenye uzalishaji na hivyo kutokuwa na mazao yaliyo bora zaidi.

Kadiri muda unavyozidi kwenda ndivyo ubora wa mazao ya wakulima unazidi kuwa wa kiwango cha chini sana kwenye ubora na hata wingi wa mazao yenyewe pia hasa kwa wakulima ambao waliowengi wanapatikana kwenye vijiji vyetu.

Alisema kuwa, wakati wote serikali imekuwa ikisisitiza sana kuwa Kilimo ndio uti wa mgongo. Maana yake ni kwamba wataalamu sasa waisaidie serikali kwenda kutoa elimu kwa wakulima huko waliko vijijini, waondokane na tabia za kukaa ofisini wkahamasishe na kuelimisha matumizi sahihi ya kanuni za kilimo bora na matumizi sahihi ya pembejeo zikiwemo mbegu ili kufanya wakulima wapate mavuno yaliyo bora na mengi zaidi kwa wakati mmoja.

RC Maganga alishangaa kuendelea kuwaona Ofisa Ugani walio wengi wakiendelea kukaa ofisini licha ya serikali kuagiza waende kwenye mashamba ya wakulima kuwasaidia, agizo ambalo bado halijatekelezeka kwa ukamilifu zaidi. Utakuta wamelundikana ofisini tuu huku wakiwaacha wakulima peke yao huu ni uzembe, alisema Maganga.

Nawaagiza Ofisa kilimo wote waende wakakae na wakulima wao ili walete mabadiliko yenye ari mpya ya kilimo bora na chenye tija. Na yeyote atayekaidi agizo hili atachukuliwa hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake alisema Mkuu wa Mkoa huyo.

Aidha alisema kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada mbali mbali za kuboresha kilimo ikiwemo kuhamasisha kilimo cha mazao ya kimkakati zaidi ili kuifanya sekta hiyo iweze kuzalisha malighafi zitakazotumika viwandani na hivyo kuweza kulipatia mapato zaidi Taifa na kuwainua wakulima wote kiuchumi na dhamira ya serikali iweze kutimia kwa wananchi wake.

Hatuwezi kukaa kimya wakati wakulima wetu hawapati msaada wowote kutoka kwa Ofisa ugani, ni lazima hatua zichukuliwe ili kufanya maonesho yajayo yawe na mabadiliko makubwa na wakulima walete bidhaa zenye ubora wa hali ya juu zaidi.

Maonesho ya nane nane kwa Kanda ya Magharibi mwaka huu yalifanyika kwenye viwanja vya Fatuma Mwasa vilivyopo Manispaa ya Tabora yakiwa na kauli mbiu ya KILIMO,MIFUGO NA UFAGAJI KWA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.