• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MANISPAA YA TABORA YAMPONGEZA MTUMISHI WAKE KWA KUMPA TUZO YA NGAO NA FEDHA TZS MILIONI TATU

Posted on: May 21st, 2022

Na Paul Kasembo - TMC

Halmashauriya Manispaa ya Tabora imeungana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa kwa kumpongeza mtumishi wake Bi. Tumaini Mgaya ambaye ni Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kutambuliwa utendaji wake na Mhe. Bashungwa kwenye Kongamano la Uwekezaji na Biashara kwa Nchi zilizo jirani na Ziwa Tanganyika.

Mhe. Bashungwa alimtangaza Bi. Tumaini Mgaya kwa kutambua utendaji kazi wake ulio mzuri wenye ubunifu wakati alipokuwa akizungumza na Makundi Maalumu katika Ukumbi wa Chuo cha Uhazili uliopo Manispaa ya Tabora wakati wa Ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Katika hafla hiyo Mhe. Bashungwa aliagiza uongozi wa Mkoa na Manispaa kutambua pia mchango wake kwa kumpatia Tuzo ili sehemu ya hamasa na kumtia moyo zaidi yeye mwenyewe pamoja na kuhamasisha watumishi wengine wa Manispaa na Mikoa mingine kuiga mfano wake katika utendaji kazi.

Tukio hilo la utoaji wa Tuzo na Fedha liliongozwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela (Diwani) mbele ya Baraza la Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Tabora lilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano Manispaa.

“Sisi Waheshimiwa Madiwani, Mkurugenzi, Menejimenti na watumishi wote wa Manispaa ya Tabora kwa pamoja tunaungana na Waziri wa TAMISEMI Mhe. Innocent Bashungwa kwa kutambua ma kuthami ni utendaji kazi wa Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Manispaa ya Tabora Bi. Tumaini Mgaya na hivyo tunatekeleza agizo lake hilo kwa kumpatia zawadi ya Ngao na Fedha Tzs Milioni tatu (3) iwe ni motisha kwake na watumishi wengine kuiga mfano wake,” alisema Mstahiki Meya Kapela.

Aidha Mstahiki Meya Kapela alisema kuwa, pamoja na kumpongeza Tumaini haitakuwa vema kama pia hatutatambua mchango anaoupata kutoka kwa watumishi wenzie hasa anaofanya nao kazi kwenye Idara yake.

Hivyo akamuomba Mkurugenzi wa Manispaa kuangalia namna ambavyo anaweza kuwatambua na wao na ikimpendeza kuwapatia Vyeti na angalau kiasi chochote kidogo kwa walio chini ya Mgaya.

Hayo yalijiri kwenye KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA BIASHARA KWA NCHI ZILIZO JIRANI NA ZIWA TANGANYIKA baada ya Mhe. Bashungwa kutembelea Banda la Maonesho la Manispaa ya Tabora na kuona kazi za Wajasiliamali wa Manispaa Manispaa hao ambao walikuwa wakiongozwa na Tumaini Mgaya lililofanyika tarehe  9-13 Mei, 2022 Mkoani Kigoma.

Ambapo katika Kongamano hilo, ni Manispaa ya Tabora pekee ndiyo iligharamia na kupeleka wajasiliamali  wake kwenye maonesho hayo kulinganisha na Halmashauri zingine.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.