• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MANISPAA YA TABORA YAFANYA SEMINA YA ANWANI ZA MAKAZI KWA WENYEVITI WA MITAA, VIJIJI NA WATENDAJI

Posted on: February 18th, 2022

Na Paul Kasembo-TMC

Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imefanya Semina kwa Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Watendaji kwa lengo la kuwapa elimu juu ya ujio wa zoezi la Anwani za Makazi ili kuwawezesha kuwa na uelewa mkubwa zaidi wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Akifungua Semina hiyo Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nyanja aliwaeleza wajumbe juu ya dhamira ya Manispaa kuwaita hapo, kwamba Serikali inakusudia kuendesha zoezi la Anwani za Makazi kwa Nchi nzima.

Ambapo kwa Manispaa ya Tabora pia inatarajia kuanza utekelezaji hivi karibuni, na ndiyo sababu ya kuitwa kwa wajumbe hao ili kuweza kupeana uelewa wa jambo linalofuata.

“Tumeita hapa ili tuweze kuoeana uelewa wa jambo ambalo tunatarajia kwenda kulitekeleza sote kwa pamoja kwenye maeneo yetu ya kiutawala, na kwamba kwenye hili zoezi viongozi wangu niwaombe tukalitekeleze kwa kutanguliza uzalendo mkubwa zaidi, umakini, usahihi na kwa wakati zaidi ili tuweze kufika malengo ya Serikali ya kumtambua mtu alipo na kuwezesha huduma za kijamii kumfikia kirahisi”, alisisitiza Dkt. Nyanja.

Kando na utangulizi huo, pia Mkurugenzi wa Manispaa aliwataarifu Wenyeviti hao kuwa atakuwa na utaratibu wa kukutana nao angalau maea mbili kwa mwaka ili kuweza kujadili juu ya namna bora ya kuboresha huduma kwa wananchi huku akiwataka kutumia mikutano hiyo kujadili changamoto zinazo wakabili na namna ya kuzitatua kwa pamoja.

Kwa upande wake mgeni wa mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda, aliwashukuru sana Wote waliohudhuria huku akiwashukuru zaidi wenyeviti wote kwa namna ambavyo wamekuwa wamekuwa wakimpatia ushirikiano wakati wote.

Dtk. Nawanda aliwaeleza wajumbe kuwa, Serikali ya Wilaya imejipanga vyema kwenda kulitekeleza zoezi la Anwani za Makazi kwa wakati, kwa weledi, kwa ufanisi mkubwa sana na kwa umakini ili Wilaya ya Tabora iwe ya kwanza kwa kutekeleza kwa kuzingatia yote hayo na hatimae iwe ya kwanza ki-Mkoa na ki-Taifa pia.

“Viongozi wangu hamjawahi kuniangusha hata mara moja, nina imani kuwa hata kwenye hili tunakwenda kulitekeleza vizuri zaidi na tuatakuwa wa kwanza kwa kila kitu, sina shaka nanyi hata kidogo”, alisema Dkt. Nawanda.

Kukamilika kwa zoezi hili kunatajwa kuwa na tija sana, ambapo kutawezesha sasa kuwa na uwezo wa kupeleka maendeleo, miundombinu ya kijamii na kuweza kutambua wapi anapatikana na hivyo inakuwa rahisi zaidi kumfikia kwa ajili uokozi, kupeleka huduma, na hatimae kumfikia kirahisi na kwa wakati.

MWISHO.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.