• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MANISPAA YA TABORA YAELEZEA MAFANIKIO YA MWAKA MMOJA WA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

Posted on: March 16th, 2022

Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imeelezea mafanikio ya mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita ambayo yanaonekana waziwazi katika Manispaa ya Tabora ambayo yamekuwa na tija kubwa sana kulinganisha na kipindi kama hiki kwa awamu zilizopita.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nyanja alipokutana na waandishi wa vyombo vya habari mbalimbali kwenye ukumbi wa mikutano uliopo Ofisi ya Manispaa ya Tabora.

Dkt. Nyanja aliwaeleza waandishi wa habari kuwa, amewaita ili waweze kusaidia kuihabarisha umma na wa-Tanzania kwa ujumla waweze kujuwa kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na inayoendelea kutekelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa wananchi wa Manispaa ya Tabora.

“Kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Rais wetu, Mama yetu, Kiongozi wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan tumepokea fedha zote za ruzuku kama zilizvyotengwa kutoka Serikali Kuu kwenye eneo la LCDG, TOZO (Dev Foreign) na FEDHA ZA NJE (Dev Foreign), hii inakuwa kwa mara ya kwanza kwa Halmasahuri ya Manispaa ya Tabora kupokea fedha zote za ruzuku ya miradi ya maendeleo kutoka fedha za ndani zilizotengwa kwenye bajeti ukilinganisha na awamu zilizopita.” alisisitiza  Dkt. Nyanja.

Pia Halmashauri ya Manispaa ya Tabora inaishukuru sana Serikali ya Awamu Sita chini ya uongozi wa mahiri wa Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kipekee za kutafuta fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo.

“Moja kati ya mifano halisi ni huu wa fedha za UVIKO-19 ambapo kwa Manispaa ya Tabora tulipatiwa gawiwo la shilingi  1,573,485,741,91 fedha ambazo zilitumika kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa 60 kwa Sekondari, na vyumba vya madarasa 14 kwa Shule Shikizi ikiwa ni pamoja na uendeshaji wa Chanjo ya UVIKO-19” Dkt. Nyanja.

Kwa upande wa Utawala Bora, kwa kipindi cha mwaka mmoja wa utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan Manispaa ya Tabora imefanya zoezi la upandishwaji na ubadilishwaji vyeo kwa watumishi 653 kutoka Idara mbalimbali na wale waliobadilishiwa vyeo (recategorization) ni 99 na wameishabadilika vyeo vyao kwenye mfumo wa Lawson. Watumishi wote hao waliopandishwa vyeo walibadilishiwa mishahara yao ndani ya mwezi mmoja tuu na sasa wanaendelea kufurahia Serikali yao, kwakuwa hakunatena malimbikizo makubwa ya mishahara.

Pia Halmashauri ya Manispaa ya Tabora iliajiri watumishi 79 ikiwa ni ajira mpya kabisa kwa Idara ya Elimu Msingi, Elimu Sekondari, Afya, Ujenzi, na Idara ya Utawala na Utumishi.

Aidha Manispaa imeendelea kutekeleza agizo la uwezeshaji makundi maalum kama Serikali ilivyoelekeza, na kwamba kwa kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita Manispaa ya Tabora imeweza kutoa mikopo kwa vikundi 129 vya wanawake, vijana na wenye ulemavu na kwamba jumla ya shilingi 662,500,000/= imetolewa.

Ambapo wanawake vikundi 99 vilikopeshwa shilingi 516,000,000/=, vijana vikundi 15 sawa na shilingi 118,000,000/=, na watu wenye ulemavu ni vikundi 15 vimekopeshwa shilingi 28,500,000/= na jumla kuu inakuwa shilingi 662,500,000/=.

Utoaji wa taarifa za mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa ni sehemu ya utamaduni wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, sambamba na utoaji wa shukurani za dhati kwa Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuboresha na kuweka mazingira rafiki kwa wajasiliamali wadogo wadogo.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI ZA MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 20222 May 06, 2022
  • Usafi wa Mazingira kwa Wananchi Wote, Jumamosi ya mwisho kila Mwezi March 23, 2017
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA NNE 2021 January 15, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAIS SAMIA AFUNGUA RASMI BARABARA YA NYAHUA-CHAYA

    May 17, 2022
  • MAFUNZO YA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI (NaPA) YAFANYIKA

    March 30, 2022
  • HAKIELIMU WAKABIDHI MAJENGO YENYE THAMANI YA ZAIDI YA MIL. 140

    March 23, 2022
  • BARAZA LA MADIWANI LIMEPOKEA, KUJADILI NA KUPITISHA TAARIFA MBALIMBALI ROBO YA PILI 2021/2022

    March 17, 2022
  • Angalia Zote

Video

MSTAHIKI MEYA BW. RAMADHAN KAPELA - UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NA UWEKEZAJI KATIKA MANISPAA YA TABORA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA
  • Taarifa Mbalimbali
  • Fomu ya maombi ya Leseni
  • Jarida 2020
  • eMrejesho
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Manispaa Tabora - Barabara ya Boma

    Anwani ya Posta: S.L.P 174 Tabora

    Simu ya Ofisi: 026-2604315/6088

    Simu ya Mkononi: 0784705044

    Barua Pepe: md@taboramc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.