• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MANISPAA YA TABORA IMEKUSANYA MILIONI 884

Posted on: September 16th, 2021

NA PAUL KASEMBO

HALMASHAURI ya Manispaa ya Tabora imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi milioni 884 ambayo ni sawa na asilimia 18 ya makadirio ya kukusanya bilioni 4.6 ya mwaka wa fedha 2021/2022.

Takwimu hizo zimetolewa leo na Mkurugenzi  wa Manispaa ya Tabora Dkt. Peter Nyanja wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema makusanyo hayo ni miezi miwili ya robo ya kwanza ya mwaka wa fedha unaoendelea.

Dkt. Nyanja alisema lengo la Manispaa ni kuhakikisha kabla ya kumalizika kwa robo ya kwanza Halmashauri iwe imekusanya asilimia 25 ya makisio na kufikia bilioni 1.1.

Alisema mafanikio hayo yameanza kuonekana baada ya kubadilisha watumishi waliokuwa wakihusika na ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuongeza nguvu ya ukusanyaji kwa kubuni vyanzo vipya vingine.

Dkt. Nyanja aliongeza kuwa mwishoni mwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha huu Manispaa inatarajia kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ya kiasi cha milioni 100.

Aidha Dkt. Nyanja amevitaka vikundi vinavyokopeshwa fedha kuhakikisha vinazitumika katika kuimarisha mitaji yao ili wawaachie fursa watu wengine kunufaika na mikopo.

“Ifike wakati vikundi hivi vinavyokopeshwa viwe vinahitimu ili kutoa fulsa kwa vikundi vipya na vyenyewe kupatiwa mikopo hiyo na mwisho wa siku vikundi vyote viwe vimenufaika kama maelekezo ya fedha hizo zinavyoelekeza badala ya kuwa vinajirudia rudia tuu vikundi hivyo hivyo,” alisisitiza Dkt. Nyanja.

Katika hatua nyingine Dkt. Nyanja alielezea namna ambavyo Manispaa imejipanga kutekeleza Miradi ya maendelo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa Zahanati, vyumba vya madarasa, utengenezaji wa madawati na ukarabati wa baadhi ya majengo ya shule yaliyochakaa.

Ambapo alisema kuwa kutekelezwa kwa miradi hiyo kutatokana na makusanyo ya ndani ya Halmashauri jambo ambalo litapelekea utoaji wa huduma kwa wananchi na kuboresha miundombinu ya mji na hivyo kuufanya mji kuwa na muonekano bora na mzuri zaidi kuliko awali.

“Tumejipanga kuongeza juhudi za ukusanyaji wa mapato jambo ambalo litapelekea kuendeleza ujenzi wa Zahanati zetu, ujenzi wa vyumba vya madarasa, uongezaji wa madawati kwa wanafunzi, ukarabati wa majengo ya shule yaliyochaa na uboreshaji wa utoaji huduma kwa wananchi wetu jambo ambalo litaongeza ustawi wa wananchi wetu pia,” alisema Dkt. Nyanja.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.