• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MADIWANI WAPATA MAFUNZO YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Posted on: July 6th, 2021

Tume ya Haki Za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), imefanya semina ya siku mbili na Madiwani wa Halimashauri ya Manispaa ya Tabora ambayo ilihudhuriwa na Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Tabora, Ndg Rukia Manduta,Waheshimiwa Madiwani wa Halimashauri ya Manispaa ya Tabora na Wanahabari wa vyombo mbalimbali.Katika semina hiyo yenye mada ya “ Haki za Binadamu na Utawala Bora”, Madiwani wanatarajiwa kujengewa uwezo wa kuwa na weredi wa kutosha kuhusiana na haki za binadamu na utawala bora.

Miongoni mwa mada ndogo ndogo zilizowasilishwa ni pamoja na Historia ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora(THBUB). Hii iliwasilishwa na Ndugu Ayoub Msendo Mackanja, ambae alieleza kuwa THBUB ni Idara huru ya Serikali iliyoanzishwa kwa mujibu wa ibara 129(1) ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano ya mwaka 1977, kwa lengo la kukuza  na kulinda hifadhi ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora Nchini Tanzania.

Haki za Binadamu ni miongoni mwa mada zilizowasilishwa katika semina hii vile vile. Mada hii ikiwasilishwa na Ndugu Paul Sulle, alieleza kwamba kimsingi haki za binadamu ni  uhuru muhimu alionao binadamu kwa sababu tu yeye  ni binadamu. Ameeleza zaid kwamba duniani wimbi la haki za binadamu lilikuwa kubwa hususani baada ya vita kuu ya kwanza ya Dunia mwaka 1914-1918, lakin haki za binadamu zikajengeka zaid kidunia kwa mwogozo wa makubaliano ya mikataba miwili ambayo ni Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiraia na Kisiasa(ICCPR), na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamadunu(ICESCR) ambazo kwa pamoja zinaunda Hati ya Kimataifa ya Haki za Binadamu(International Bill of Rights).

Dhana ya Utawala Bora ni moja miongoni mwa mada zilizowasilishwa vilevile katika semina hiyo. Mada hii ikiwasilishwa na ndugu Mbwana Mussa Mbwana, ambaye alieleza maana halisi ya Utawala Bora kuwa ni zoezi la wenye madaraka katika maamuzi kuamua ni namna gani rasilimali za Taifa zitumike kwa ajili ya kuboresha maisha ya wananchi.

Ameeleza zaidi kwamba kimsingi Utawala Bora misingi yake ni uwazi, uwajibikaji, utawala wa sheria, ushirikishwaji,usawa, ufanisi na tija, mwitikio, maridhiano pamoja na uadilifu. Alifafanua zaidi kwamba katika hali ya kawaida sana, misingi hiyo ikitekelezwa, utawala bora umetekelezwa na hali kadhalika isipotekelezwa hakuna utawala bora.Utawala Bora huleta matumizi mazuri ya rasilimali za nchi, maendeleo endelevu, huduma bora za jamii na kuheshimiwa kwa haki za binadamu.

Mada ya Serikali za Mitaa ni moja ya hoja zilizowasilishwa katika semina hiyo, akiwasilisha mada hiyo Mwanasheria wa Halimashauri ya Manispaa yaTabora ndugu Deodoroth Chuwa,ambaye alieleza kwa mapana maana,historia na chimbuko la serikali za mitaa, alieleza nafasi za watendaji wa kata na madiwani katika kuleta maendeleo yenye tija kwa kata zao. Alifafanua majukumu ya Diwani na mipaka yake pamoja na Afisa mtendaji kata, na umuhiimu wa wao kuwa kitu kimoja katika kutekeleza utawala wa Sheria unaozingatia haki za raia.

Aidha Madiwani waliweza kuibua changamoto mbalimbali zikiwemo za ukiukwaji wa haki za binadamu katika meneo mengi ndani na nje ya Manispaa ya Tabora, changamoto za kiutendaji kwani wanadai mamlaka waliyonayo ni madogo , hawawezi kuwawajibisha kinidhamu papo kwa papo watendaji wa Serkali wanaotumi vibaya madaraka yao. Vilevile walieleza suala la wenyeviti wa vijiji kukosa posho wakati watendaji wa vijiji wana mishahara, hivyo ufanis wa wenyeviti na uaminifu unakuwa changamoto sana katika kuleta maendeleo endelevu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.