• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MADIWANI, WANASIASA NA WANANCHI WA MANISPAA YA TABORA WAASWA KUJIEPUSHA NA VITENDO VYA RUSHWA HASA KWENYE CHAGUZI ZINAZOKUJA HIVI KARIBUNI

Posted on: August 13th, 2024

Na Alex Siriyako

Bi. Happiness Madeghe, Mkuu wa Dawati la Uelimishaji Umma wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) Mkoa wa Tabora akiongea na Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Tabora katika kikao cha kawaida cha Baraza la Madiwani robo ya nne mwaka wa fedha 2023/2024 katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora amekumbusha kuwa kama Taifa tunaenda kwenye chaguzi mbalimbali kuanzia wenyeviti wa mitaa, vijiji na Vitongoji mwaka huu, pamoja na Uchaguzi Mkuu wa Madiwani, Wabunge na Rais mwakani, hivyo suala la rushwa limekuwa ni changamoto kubwa hasa ifikapo nyakati hizi za uchaguzi.

Bi. Madeghe amefafanua kuwa, rushwa iko katika mazingira tofauti tofauti sana, ikiwemo rushwa ya kutoa fedha taslimu, rushwa ya ngono, pamoja na rushwa ya kutoa zawadi ya aina yeyote ili tu mlengwa aweze kutimiza adhima yake, hivyo amesisitiza kuwa TAKUKURU iko kazini masaa ishirini na nne, na kwa kipindi hiki cha uchaguzi itaongeza nguvu zaidi, pia amewasihi sana Waheshimiwa waendelee kuwaelimisha Wananchi wao madhira yatokanayo na vitendo vya rushwa.

TAKUKURU, TUWASA, TANESCO pamoja na TARURA ni miongoni mwa taasisi za umma zinazotoa huduma katika Manispaa ya Tabora ambazo zimealikwa na kupata wasaa wa kutoa ufafanuzi, elimu pamoja na mpango mkakati wa kuendelea kumaliza changamoto za Wananchi hasa kwenye maji, umeme pamoja na barabara.

Kwa upande wao Waheshimiwa Madiwani,pamoja na mambo mengine, wamesisitiza hasa upande wa TARURA kuwa, taratibu za kuwapata wazabuni ziharakishwe, ili angalau vipande vilivyopata bajeti kwa mwaka huu wa fedha, viweze kuanza kujengwa kabla nvua hazijaanza kunyesha, lakini pia waendelee kufanya jitihada za kurekebisha barabara zilizosombwa na nvua nyingi msimu uliopita, kwani nazo barabara hizi kwa sasa hazipitiki kabisa.

Aidha, Waheshimiwa Madiwani wameendelea kuipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Manispaa ya Tabora fedha nyingi sana za miradi ya maendeleo hasa katika sekta mtambuka za Kilimo, Elimu, Afya pamoja na Miundombinu ya barabara.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mhe. Ramadhani Kapela kwa niaba ya Baraza ametoa pongezi za dhati kwa Menejimenti ya Manispaa ya Tabora chini ya Uongozi wa Mkurugenzi wa Manispaa hii Ndugu Elias M. Kayandabila kwa kukusanya mapato kwa asilimia mia moja kwa mwaka wa fedha 2023/2024, lakini pia kwa kupata hati safi ya ukaguzi wa CAG kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.