• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MADIWANI WA MANISPAA YA TABORA WAPONGEZWA KWA UMOJA WAO

Posted on: March 22nd, 2018

BAADHI ya Vyama vya Siasa MkoaniTabora vimelipongeza Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa kutokuwa na makundi na kuwa na mshikamano na umoja wakati wa uendeshaji vikao vyake.
Kauli hiyo imetolewa jana na viongozimbalimbali wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama cha Wananchi(CUF) walioalikwa kuhudhuria kikao maalumu cha Baraza hilo.

Katibu  wa CHADEMA Wilaya ya Tabora Msabaha Kambambovu alisema uendeshaji wa kikao cha Baraza la Madiwani wa Manispaaya Tabora na uchangiaji wa Madiwani umeonyesha kuwepo na umoja miongoni mwao licha ya viongozi hao kutoka Vyama tofauti vya kisiasa.

Alisema katika muda wote alipokuwa ndani ya ukumbi wa mikutano hakuona zomeazomea wala mjumbe kukatazwa kuchangia kwasababu ya utofauti wake wa kisiasa.
Kambambovu alisema ni vema waendeleze mshikamano huo kwa ajili ya maslahi mapana ya kuwasaidia wakazi wa Manispaa ya Tabora.

Naye Mwenyekiti wa CUF Wilaya yaTabora Mirambo Camil alisema kama ni mgeni wa Madiwani waliopo katika Barazahilo unaweza kudhani wanatoka Chama kimoja kwa jinsi walivyokuwa wakishirikiana katika uchangiaji wa hoja mbalimbali.

Alisema umoja huo utasaidia kuijengaTabora mpya ambayo itapeleka miradi ya maendeleo katika maeneo yote bila kujali Diwani wa Kata husika anatoka upinzani.

Naye Mtahiki Meya wa Manispaa yaTabora Mh. Leopold Chundu Ulaya aliwataka Madiwani wote kuendeleza Umoja na mshikamano ili waweze kusaidia katika kuwaletea maendeleo wakazi wa eneo hilo.

Alisema kuwa hata Mheshimiwa Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anasema maendeleo hayana Chama kwa hiyo ni vema wakaendeleza umoja ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Katika hatua nyingine Baraza laMadiwani la Manispaa ya Tabora limepitisha mapendekezo ya marekebisho ya bajeti ya ruzuku ya miradi ya maendeleo ya miundombinu (LGCDG) ya bilioni 1.3 kwa ajili ya mwaka huu wa fedha (2017/18).

Mapendekezo ya marekebisho ya bajeti hiyo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bosco Ndunguru katika kikao cha dharura cha Baraza hilo.

Alisema wameamua kufanyika marekebisho hayo kufuatia agizo la Waziri wa Nchi Ofisi yaRais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa za kuzitaka Halmashauri zote nchini kufanyia uchambuzi upya bajeti za miradi ili kuwa na miradi michache inayotekelezeka na kukamilika kwa wakati na kwa asilimia 100.

Mkurugenzi huyo Mtendaji alisema kuwa inalenga kuongeza wingi na ubora wa huduma za jamii na miundombinu pamoja na kuwezesha utawala bora.

Ndunguru alisema miradi itakayotekelezwa ni ile inayohusu sekta ya afya na elimu ambayo ujenzi wake umefikia katika mtambaa panya na miradi hiyo inatakiwa kukamilika kabla ya mwaka huu wa fedha kumalizika.

Aliongeza miradi mingine itatekelezwa katika Bajeti ya mwaka ujao wa fedha kulingana na upatikanaji wa fedha



Mwisho



Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.