Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

MADIWANI WA MANISPAA YA TABORA WAIPONGEZA MENEJIMENTI KWA MAKUSANYO YA ZAIDI YA BIL 3 MAPATO YA NDANI

Posted on: July 31st, 2019

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora wamempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa Bw. Bosco Ndunguru na Menejimenti yote kwa kukusanya mapato ya ndani zaidi ya sh bilioni 3 tofauti na miaka mingine iliyopita.

Wakiongea katika kikao cha baraza kilichoanza tarehe 29-31/ 07/2019, walisema kuwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 Manispaa ilikuwa na lengo la kukusanya kiasi chaTsh bilioni 4.2 lakini imeweza kukusanya Tsh bilioni 3.4 hadi sasa sawa na asilimia 81 ya lengo lake.

Katibu na msemaji wa Madiwani wa Chama Cha Mapinduzi ambae pia ni Diwani wa (CCM) kata ya Ndevelwa Mhe, Seleman Juma Maganga alisema kuwa mapato hayo ni ya kihistoria kwani tangu Halmashauri hiyo ianzishwe haijawahi kuvuna kiasi hicho cha fedha katika makusanyo yake ya ndani.

Alisema kuwa mapato ya mwaka huu yameonesha dhahiri kuwa kumbe Manispaa  inaweza kukusanya zaidi ya makadirio yake kama Ofisi ya Mkurugenzi itashirikiana ipasavyo na Wataalamu wake kama walivyofanya sasa, alisema Maganga.

Maganga alitoa mfano wa mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo Halmashauri hiyo ilikadiriwa kukusanya Tsh bil 3.6 lakini ikakusanya Tsh bilioni 2.5 sawa na asilimia 70 tu. Na kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ilikadiriwa kukusanya Tsh bilioni 3.8 lakini ikakusanya Tsh bilioni 2.2 sawa na asilimia 60 tu, lakini mwaka huu wamefanya vizuri zaidi.

Alifafanua kuwa mapato ndio uti wa mgongo wa Halmashauri yoyote na serikali yoyote duniani inategemea mapato ili kuleta maendeleo kwa wananchi wake. Hivyo hatua ya kupandisha zaidi makadirio hadi sh bil 4.2 na kufanikiwa kukusanya asilimia 81 ya kiasi hicho kumeiwezesha Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa wananchi wake.

Kwa uapnde wake Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora ambae pia ni diwani wa (CCM) kata ya Ipuli  Mhe, Leopold Ulaya alisema kuwa, kwa mwezi Juni pekee Halmashauri  imeweza kukusanya zaidi ya Tsh milioni 500 ambayo ni sawa na asilimia 156 ya lengo la makusanyo ya mwezi. Hivyo akatumia fulsa hiyo kuwasisitiza Menejimenti kuongeza kasi zaidi ili waweze kufanya vizuri zaidi na zaidi na kufikia lengo lililowekwa.

Aidha katika taarifa hiyo iliyosomwa na kwa niaba ya Madiwani wa CCM ilisema kuwa mafanikio hayo yamechochewa na kasi ya utendaji na maelekezo ya Mhe Rais John Pombe Magufuli, ambaye aliagiza kila Halmashauri kuongeza kasi zaidi ya ukusanyaji mapato.

Kwa namna ya kipekee, Madiwani walimpongeza sana Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala kwa weredi, ufanisi na ubunifu wake katika utendaji kazi wake na hivyo wakamuagiza Mkurugenzi wa Manispaa amuandikie barua ya pongezi.

Akiongea na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Manispaa,Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa Bw Ndunguru alikiri kuwa hiyo ni mara ya kwanza kwa halmashauri kukusanya mapato mengi namna hiyo. Aidha alisema kilichowasaidia sana kuwa ni ushirikiano wa wataalamu, madiwani, takwimu sahihi za vyanzo vya mapato ya walipa kodi wote na kutumia kikosi kazi maalumu/special task force kwenye kazi ya makusanyo.

Mkurugenzi litaja sababu nyingine kuwa ni utoaji elimu kwa walipa kodi wote, kazi amabayo ilifanywa na Halmashauri kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato (TRA) Tabora Manispaa na kudhibiti mapato na matumizi ya Halmashauri ikiwemo ushirikiano mzuri wa usimamizi,ushauri na fuatiliaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bw Aggrey Mwanri na Mkuu wa wilaya ya Tabora Manispaa Bw Komanya Kitwala.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.