• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KATIBU TAWALA WA WILAYA YA TABORA AMUAGIZA MKURUGENZI WA MANISPAA YA TABORA KUANDAA NA KURATIBU KONGAMANO KUBWA LA KUTANGAZA UTALII NA FURSA ZA KIUCHUMI ZILIZOPO WILAYA YA TABORA NA MKOA WA TABORA KWA UJUMLA

Posted on: November 28th, 2023

Na Alex Siriyako:

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora Bi. Asha Churu akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe.Louis Peter Bura katika kikao cha wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Tabora,ametoa maelekezo ya Serikali kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kuandaa na kuratibu Kongamano kubwa lenye malengo mahsusi ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Manispaa ya Tabora na Mkoa wa Tabora kwa ujumla.

Bi.Churu ametoa maelekezo haya leo Novemba 26,2023 katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora baada ya majadiliano ya kina na wadau wa maendeleo na kubainika kuwa utalii na fursa zake za kiuchumi katika Wilaya ya Tabora na Mkoa wa Tabora bado hazijatangazwa vya kutosha hivyo kuna sababu za msingi za kujipanga upya na kuzitangaza fursa hizo.

Wadau wa maendeleo wa Wilaya ya Tabora wamekutana leo katika ukumbi wa Manispaa ya Tabora huku wakiwa na ajenda kubwa ya kutangaza utalii wa Tabora, ambapo leo katika kikao hiki wamekutana na Balozi na Mdau mkubwa sana wa Utalii Tanzania Bi.Nangasu Werema ambae ameungana na wadau hawa leo katika kupeana uzoefu na mikakati inayoweza kutumika kutangaza Utalii na fursa zake za kiuchumi zinazopatikana Mkoa wa Tabora.

Bi.Werema ameeleza kuwa, kwasasa ana kampeni ya kutangaza Utalii wa Tanzania kwa jina la TALII NA MAMA SAMIA, kampeni yenye kauli mbiu isemayo UTALII NI UCHUMI. Ameendelea kufafanua kuwa kwasasa anatangaza vivutio vya Utalii kwa Mikoa ya Kanda ya Magharibi ambapo ameanza na Mkoa wa Tabora.

Miongoni mwa wadau waliohudhuria kikao hiki ni pamoja Mhifadhi Sefu Salumu ambae ni Afisa Maliasiri wa Manispaa ya Tabora na ameeleza kwa kina vivutio vya utalii katika Wilaya ya Tabora vikiwamo Tabora ZOO, Tembe la Dkt.Living Stone, Mnara wa Mwalimu Nyerere, Tabora School, pamoja na Njia Kuu ya Watumwa wakitokea Ujiji Kigoma hadi Bagamoyo.

Aidha Wawakilishi kutoka TANAPA Kanda ya Magharibi, TAWA Kanda ya Magharibi pamoja na TFS Wilaya ya Tabora walikuwepo na kila mmoja wao amepata nafasi ya kueleza vivutio pamoja na fursa za kiuchumi walizonazo mbele ya wadau waliohudhuria kiako hicho.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.