• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KATIBU TAWALA WA MKOA ATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA NA HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

Posted on: December 11th, 2021

NA ALEX SIRIYAKO

Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Bw. Musalika Makungu kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani, amefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Katibu Tawala pia aliambatana na Wataalamu mbalimbali kutoka Sekiretarieti ya Mkoa, miongoni mwa watalaamu hao ni pamoja na Jacob Mnyambwa (Mchumi), Jiame M.Mbati (Katibu Tawala Msaidizi), Shani Mangesho (Msimamizi wa Fedha, Serikali za Mitaa) pamoja na Rukia Manduta (Katibu Tawala Msaidizi). Hali kadhalika katika ziara hiyo, Katibu Tawala aliweza kuongozana na Watalaamu mbalimbali kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Tabora wakiongozwa na Mkurugenzi wa Manispaa Dkt. Peter M. Nyanja.

Katika ziara hiyo miongoni mwa miradi iliyopata fursa ya kutembelewa ni pamoja na; Ujenzi wa Madarasa mawili na Ofisi (UVIKO-19) pamoja na ukarabati wa Maabara ya PHYSICS shule ya Sekondari Cheyo, Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya, Ujenzi wa madarasa matano na Ofisi moja (UVIKO-19), Ujenzi wa madarasa matatu na Ofisi moja(Mapato ya Ndani) shule ya Sekondari Ipuli, Mradi wa Upimaji Viwanja 24 Kata ya Mapambano pamoja na Mradi wa kujenga Vibanda vya Machinga eneo la karibu na Standi kuu ya Mabasi kata ya Chemchem.

Katika ziara hiyo, Miradi yote imekaguliwa kwa kina na kwa ujumla Wataalamu wa Mkoa walilidhika na ubora wa miradi yote ikiwa ni sambamba na kasi ya utekelezaji ambapo kwa mfano Hospitali ya Wilaya muda sio mrefu itaanza kutumika, na madarasa yote yamekamilika kwa asilimia zaidi ya tisini na tano. Wataalamu vilevile walifurahishwa na namna upimaji wa viwanja ulivyozingatia matumizi tofauti tofauti hususani uwepo wa Viwanja vya Viwanda Vidogo vidogo, kwani Tabora inahitaji Viwanda sana kwa sasa. Hali kadhalika alihimiza ujenzi wa Vibanda vya Machinga uongeze kasi na mabanda hayo yapangwe kimkakati ili kuwe na mpangilio mzuri wa huduma katika soko hilo.

Aidha kulingana na changamoto ndogondogo zilizobainika, wataalamu wa Mkoa walitoa ushauri wao wa msingi sana ikiwa ni pamoja na kufuata Mwongozo wa PPRA katika kutekeleza Miradi hii inayojengwa kwa utaratibu wa Force Account, Bidhaa zote zinazonunuliwa na kupokelewa zionekane kwenye  Kitabu cha REJA, Taarifa zote za miradi ziwepo kwenye mafaili zikiwemo taarifa za Mikataba ya Mafundi pamoja na taarifa za manunuzi.

 Baada ya kumaliza kutembele miradi hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Bw. Musalika Makungu aliweza kuweka msisitizo kwenye maelekezo ya Wataalamu na ushauri wao,ikiwa ni pamoja na kufuata Mwongozo wa PPRA kwenye utekelezaji wa miradi yote inayojengwa kwa mfumo wa Force Account, lakini pia amesisitiza suala la Madawati yawepo kwenye madarasa yanayojengwa na zaidi kabisa akasisitiza kwamba uaminifu na uadilifu kwenye utekelezaji wa miradi ni wa razima. Mwisho kabisa amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri aendelee kusimamia kwa weredi mkubwa miradi yote ndani ya Manispaa ya Tabora.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.