• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KATA YA NG’AMBO NI MOJA KATI YA KATA MBILI ZA MAJARIBIO KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA MAJARIBIO WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KITAIFA

Posted on: November 20th, 2023

Na Alex Siriyako;

Kata ya Ng’ambo iliyopo Manispaa ya Tabora, katika Mkoa wa Tabora, ni miongoni mwa Kata mbili zilizoteuliwa kwa zoezi la Majaribio la kuboresha Daftari la Kudumu la Mpiga Kura huku Kata nyingine ikiwa ni Kata ya Ikoma iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Mkoani Mara.

Taarifa hizi zimebainishwa na Mhe. Balozi Omar Ramadhan Mapuri ambae ni Mjumbe wa TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI katika Mkutano wa Tume na Wadau wake ambao umefanyika leo Novemba 20, 2023 katika ukumbi wa Mwanakiyungi ,Mkoani Tabora, zoezi litakalo fanyika kuanzia Novemba 24 hadi 30,2023.

Mhe.Mapuri ameeleza kuwa, kwa mujibu wa sheria za Uchaguzi, ni jukumu la Tume kuboresha Daftari la kudumu la Mpiga Kura kabla ya Uchaguzi mwingine kufanyika, na katika kuboresha mifumo na tekinolojia ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga kura kuna majaribio ya kutosha yanafanyika ili kubaini changamoto zote zinazoweza kujitokeza mathalani ubora wa vifaa vinavyotumika, mtandao hafifu wa simu, ukosefu wa umeme na kadhalika, ili changamoto hizi ziweze kufanyiwa kazi kabla ya zoezi kuanza rasmi.

Aidha Mhe.Mapuri amefafanua kuwa uboreshaji wa majaribio utahusisha kuandikisha raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 18 au Zaidi, Raia atakae fikisha miaka 18 kabla au siku ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, Wapiga kura wanaoboresha taarifa zao ambao wamehama kutoka eneo moja la uchaguzi kwenda eneo jingine, Waliopoteza kadi zao za kupiga kura ama kuharibika, Wanaorekebisha taarifa zao, pamoja na kuondoa wapiga kura waliopoteza sifa za kuwemo kwenye Daftari.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria Tume ya Taifa ya Uchaguzi Ndugu Selemeni Mtibora akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI amefafanua kuwa Serikali imefanya maboresho makubwa sana katika teknolojia itakayotumika kuandikisha wapiga kura ikiwa ni pamoja na BVR Kits mpya zenye kilo 15 badala ya zile za zamani za kilo 35, lakini pia zikitumia program endeshi ya ANDROID badala ya WINDOW.

Katika kuhitimisha Mkutano huu, wadau wameridhishwa na nia thabiti ya Serikali ya kuwashirikisha katika kila hatua hii na wameomba Serikali iendelee na utaratibu huo. Aidha wameeleza kuwa wako tayari kutoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuwa zoezi la uboreshaji wa majaribio wa Daftari la Kudumu la Mpiga kura katika kata ya Ng’ambo linakwenda vizuri kama lilivyoratibiwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.