• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA SIASA YA MKOA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: January 11th, 2022

Na Alex Siriyako,

Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Tabora imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora. Kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Bw.Hassani Wakasuvi ambae aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dr. Batilda Burian pamoja na wajumbe wengine wa kamati wakiwemo; Maimuna Abbas, Lukas Sereli, Imani Matabula pamoja na Mwashamu Hashimu ambaye ni mjumbe wa Sekretarieti ya Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tabora.

 Vilevile Kamati hii iliambatana na Kamati ya Siasa ya Wilaya ya Tabora ikiongozwa na Mwenyekiti wake Bw. Mohamedi Katete, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Dkt. Yahaya Nawanda, Meya wa Manispaa ya Tabora Mh. Ramadhani Kapera , Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Bw. Seif Salum Seif, Wajumbe wa kamati pamoja na wataalamu wa Idara mbalimbali wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

Kamati hii imetembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 katika Manispaa ya Tabora ikiwa ni miradi inayotekelezwa kwa fedha kutoka vyanzo mbalimbali ikiwemo Mapato ya ndani ya Halmashauri, Fedha za tozo za Miamala ya simu, Fedha za Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 pamoja na fedha za maendeleo kutoka Serikali kuu.

Miongoni mwa miradi iliyopata fursa ya kutembelewa na kukaguliwa na Kamati ya Siasa ya Mkoa ni pamoja na Madarasa matano na Ofisi moja (Milioni mia moja kutoka mradi wa UVIKO-19), Umaliziaji wa Madarasa matatu na Ofisi moja (Milioni 25, fedha za TOZO), Ukamilishaji wa Maabara moja ya Sayansi (Milioni 30, Fedha kutoka Serikali Kuu), Miradi yote hii imetekelezwa katika Shule ya Sekondari Ipuli, Kata ya Ipuli. Kamati imekagua Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Tabora (Fedha za Maendeleo kutoka Serikali Kuu),  ambapo kuna majengo mengi yanayoendelea kujengwa kama jengo la Utawala, Jengo la Mama na Mtoto, Maabara,na OPD. Jengo la Huduma kwa Wagonjwa wa Nje(OPD) limekamilika na huduma zinatarajia kuanza kutolewa Janauri 15,2022.

Kamati imekagua vilevila ujenzi wa madarasa matatu na Ofisi moja Shule ya Msingi Kakola, Kata ya Kakora (Zaidi ya milioni 23, Mapato ya ndani) ambapo ujenzi uko hatua za umaliziaji. Kamati imekagua Madarasa mawili na Ofisi  Shule Shikizi ya Tumbi, Kata ya Misha (Milioni arobaini, UVIKO-19),= na Kamati imemaliza Ziara yake kwa kukagua Ujenzi wa Kituo cha Afya Misha (Milioni 250, fedha za TOZO) ambapo kwa awamu ya kwanza yanajengwa majengo matatu, Jengo la Huduma kwa Wagonjwa wa nje(OPD), Maabara na kichomea taka. Ujenzi wa mradi huu uko hatua ya kupandisha boma.

Mwenyeki wa Kamati Bw. Hassani Wakasuvi kwa niaba ya Kamati kwanza aliridhika na ubora na gharama za miradi pia alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada zake za dhati kabisa za kuwaletea maendeleo Watanzania hususani wakazi wa Manispaa ya Tabora kwa kuwapatia kiwango kikubwa cha fedha na kwa muda mchache sana kwenye miradi ya maendeleo katika sekta ya Elimu, Afya, Maji na Barabara. Vilevile amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Buriani, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Dkt. Yahaya Nawanda , Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Bw. Mohamedi Katete, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Tabora Mh. Ramadhani Kapela pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Bw.Seif Salum Seif kwa umoja wao wa kuunganisha nguvu na kuwa kitu kimoja katika usimamizi wa miradi hii ya maendeleo.

Bw. Hassani Wakasuvi pamoja na kuridhika na ubora wa miradi na namna fedha ilivyosimamiwa vizuri, alitoa maelekezo kwa Watendaji hususani Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora, miongoni mwa maelekezo ni kujenga uzio kuzunguka shule ya Sekondari Ipuli, Kuweka mpango wa kujenga uzio kuzunguka Hospitali ya Wilaya, Kuweka mipango ya Kibajeti ya kujenga nyumba za Watumishi katika Hospitali ya Wilaya na Kituo cha Afya Misha pamoja na Halmashauri kujipanga kuanza kufikiria kujenga madarasa ya ghorofa kwani ardhi haiongezeki na mji unakuwa.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora nae amempongeza Mama Samia Suruhu Hassan kwa moyo wake wa huruma na upendo kwa Watanzania hususani kwa Wakazi wa Wilaya ya Tabora kwani ameleta fedha nyingi sana za maendeleo ngazi ya Kata, Fedha ambazo pamoja na Ujenzi wa miradi lakini pia zimekuwa fursa kubwa kwa ajira kwa vijana wa Tabora na Wajasiriamali wengine. Vilevile amewashukuru Wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Tabora na kuahidi kusimamia maelekezo na ushauri walioutoa kwa ustawi wa Manispaa yetu na Mkoa wa Tabora kwa ujumla

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.