• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YATEMBELEA NA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO 7 TABORA MANISPAA

Posted on: July 24th, 2021

Na Alex Siriyako

Kamati ya Siasa ya Chama cha Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tabora leo imefanya ziara ya kutembelea na kukagua Miradi ya Maendeleo saba iliyopo hapa Tabora Manispaa na kuridhishwa nayo.

Akizungumza kwenye kikao cha majumuisho ya ziara Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Mhe. Mohamed Katete alisema kuwa, chama kimeridhishwa sana kwa namna ambavyo Halmashauri ya Manispaa ya Tabora inavyotekeleza Miradi hiyo.

 Katete alisema kuwa utekelezaji mzuri wa miradi hiyo unaleta faraja sana jambo ambalo wao kama viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na ndiyo wenye Ilani ya Chama ambacho kinaongoza Nchi wameona lina akisi na kwenenda na matarajio ya Chama katika kuisimamia Serikali.

“Sisi kama Chama kinachosimamia Serikali katika Ilani yetu tuliahidi mambo kadha wa kadha na hapa tumeona mnayatekeleza, hivyo tumeridhishwa sana na kwamba mnakwenda sambamba na matakwa ya Chama, hongereni sana kwa hili”, alisema Katete.

Siku ya kwanza  Kamati ilitembelea na kukagua miradi minne ikiwa ni Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Itulu Kata ya Ndevelwa wenye thamani ya zaidi ya Milioni 50 ambapo ujenzi wake unaendelea na umefikia hatua ya umaliziaji, ikafuatiwa na ukarabati wa majengo kwenye Shule ya Sekondari Tabora Wavula wenye thamani ya Milioni 500 fedha kutoka Serikali Kuu na kwamba ukarabati huo umekemilika.

Kamati pia iliendelea na ukaguzi kwenye mradi wa ujenzi wa Madarasa mawili (2) pamoja na matundu ya vyoo 12 Shule ya Sekondari Kanyenye iliyopo Kata ya Malolo vikiwa na thamani ya zaidi ya Milioni 50, ambapo ipo hatua ya upauaji, na baadae Kmati ya Siasa ilitembelea na kukagua ujenzi wa Madarasa 2 pamoja na matundu ya vyoo 12 kwenye Shule ya Msingi Mwinyi  ikiwa na thamani ya zaidi ya Milioni 50 ambapo ipo kwenye hatua ya Boma.

Siku ya pili Kamati ilipata wasaa wa kutembelea na kukagua miradi mingine mitatu ambapo ilianza kwa kukagua ujenzi wa Zahanati ya Ikomwa ambao utagaharimu zaidi ya Milioni 70 ikiwamo na nguvu za wananchi, ikafuatiwa na ukaguzi wa ujenzi wa Zahanati ya Misha iliyopo Kata ya Misha wenye thamani ya zaidi ya Milioni 50 na kwamba ujenzi kwa Zahanati zote mbili ujenzi badoo unaendele.

Kisha Kamati iliendelea na ukaguzi kwa Kituo cha Afya Tumbi kilichopo Kata ya Tumbi, mradi ambao umegharimu zaidi ya Milioni 200 kimekamilika  na kinatoa huduma tayari, na baadae kamati ilihitimisha ziara yake kwa kukagua Vikundi  4 vya Ujasiliamali kati ya hivyo vikundi 2 vimepata mkopo hivi karibuni na vingine 2 vilikwisha pata siku nyingi na vipo kwenye marejesho vikiwa na jumla ya Milioni 35.

Wakitoa maoni wajumbe wa Kamati ya Siasa walisema wameridhishwa sana kwa namna ambavyo Serikali ya Wilaya ya Tabora inavyotekeleza Ilani ya CCM kwa vitendo, na kwa kauli moja wajumbe wa kamati walimpongeza kwa dhati kabisa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Hassan Suluhu pamoja na Wizara zinazohusika katika miradi hiyo kwa namna ambavyo wameamua kutatua kero nyingi zinazowakabili wananchi hasa wa Wilaya ya Tabora.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mheshimiwa Dkt. Yahya Ismail Nawanda aliwashukuru wajumbe wote wa Kamati ya Siasa Wilaya kwa namna ambavyo wameweza kutembelea, kukagua, kushauri na kupongeza kwa miradi yote waliyopita. Na kwamba wao kama Serikali ya Wilaya wamepokea yote na kwamba ushauri wao wameupokea na kwamba wataufanyia kazi na kurekebisha penye kasoro.

Ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tabora ina lengo la kuwawezesha wajumbe wa Chama waweze kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo, kushauri na kupongeza inapobidi kwa minajiri ya kuboresha na kuisadia Serikali kwenye utekelezaji wa Ilani inayolenga kuwaondolea kero wananchi na kuwasogezea huduma karibu kama ilivyo dhamira njema ya Mhe. Rais na Chama pia.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.