• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA LAAC YAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UJENZI WA MIRADI MIZURI NA UTOAJI WA MIKOPO YA 10% YENYE TIJA

Posted on: March 17th, 2023

Na Alex Siriyako;

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imeipongeza Manispaa ya Tabora kwa utoaji wa Mikopo ya asilimia kumi (10%) kikamilifu na yenye tija kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu kupitia asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri. Aidha kamati imeipongeza Manispaa ya Tabora kwa ujenzi wa miradi mizuri kwa kuzingatia ubora na thamani ya fedha.

Haya yameelezwa leo tarehe 17 Machi 2023 wakati kamati hii ambayo imeongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Stanslaus Mabula (Mb), ambae ameambatana na Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt.Festo Dugange, kukagua miradi ya maendeleo pamoja na miradi ya vikundi vinavyonufaika na mikopo ya asilimia kumi.

Kamati imekagua Kituo cha Afya cha Tumbi, Ukarabati wa Bweni pamoja na ujenzi wa Viwanja vya Michezo Shule ya Tabora Wavulana, Kikundi cha Vijana cha Miombo Bee Keepers Initiative Group ambacho kinafuga nyuki pamoja na kusindika mazao ya nyuki kwa kuyaongezea thamani, pamoja na Kikundi cha Wanawake cha Holy Kitchen ambacho kinapika chakula (Catering), kinaoka keki, pamoja na kusindika  Maziwa ya Ng’ombe.

Wajumbe wa Kamati kwa ujumla wameridhika na ubora wa majengo ya Kituo cha Afya Tumbi kwani ujenzi ulifuata BOQ na thamani ya fedha zilizoletwa na Serikali takribani milioni 500 zinaonekana. Hata hivyo, Mwenyekiti na Wajumbe wameiagiza mamlaka ya maji safi na salama Mkoani Tabora (TUWASA) kuharakisha upatikanaji wa maji safi ,salama na yenye uhakika kituoni hapo. 

Wajumbe wa kamati wamekagua ukarabati wa bweni shule ya Sekondari ya Tabora Wavulana, ukarabati uliogharimu Zaidi ya milioni 500 ambapo wameridhika na ukarabati huo japo wameitaka Serikali kupitia Wizara ya TAMISEMI kuona umuhimu wa kutafuta fedha na kuzikarabati shule zote kongwe za Mkoa wa Tabora kwani hali ya miundombinu ya shule hizi haiendani na ukubwa wa majina ya shule hizi.Vilevile wajumbe wamekagua mwenendo wa ujenzi wa viwanja vipya vya michezo vinavyojengwa shule ya Tabora Wavulana kwa gharama ya takribani milioni 540, viwanja ambayo vinatarajia kuongeza ufanisi katika michuano ya UMITASHUMITA NA UMISETA , michezo ambayo ilifanyika mwaka jana na inatarajia kufanyika Manispaa ya Tabora  tena mwaka huu.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange amesema Serikali itaendelea kuzisimamia Halmashauri na kuhakikisha zinafanya vizuri  zaidi kwenye mikopo ya asilimia kumi, na kwa suala la ukarabati wa shule kongwe, kwa niaba ya TAMISEMI, amelichukua na kuahidi kwenda kulifanyia kazi.

Bi. Irene Malle, Mwenyekiti wa Kikundi cha Holy Kitchen, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mama Samia Suluhu Hassan kwa mkopo wa milioni hamsini kwenye kikundi hicho, na ameahidi kufanya vizuri Zaidi na kurejesha mkopo huo kwa wakati.


Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.