• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA FEDHA NA UTAWALA YAFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI

Posted on: August 13th, 2021

Na Alex Siriyako,

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Ndugu Ramadhani Kapela, ambae pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Fedha na Utawala, akiongozana na wajumbe wa kamati hiyo wa baraza la Madiwani, akiambatana vilevile na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora,Ndugu Sefu Salum, Katibu Tawala wa Manispaa ya Tabora,Ndugu Hamarskjold Yonaza, pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo, ameiongoza kamati hiyo kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika kata mbalimbali za Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

Kamati ya fedha ikiwa ni miongoni mwa kamati mbalimbali za Baraza la Madiwani, imefanya ziara ya siku mbili mfululizo kuanzia tarehe 12/08/2021 hadi leo hii tarehe 13/08/2021, ambapo kimsingi imefanya ziara hii kukagua baadhi ya miradi ya maendeleo katika kata mbalimbali za Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

Katika Sekta ya elimu, miradi iliyotembelewa na kukaguliwa katika ziara hii ni pamoja na Ujenzi wa matundu kumi na mawili katika shule ya msingi Igombe B, na ujenzi unaendelea vizuri. Aidha kamati ilikagua  vyumba vya madarasa viwili na ofisi ya walimu katika sekondari ya  Ipuli, kata ya Ipuli, Kamati ilikagua vilevile  vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu , matundu kumi na mawili ya vyoo katika shule ya Msingi Majengo kata ya Mpela.

Katika sekta ya Afya, Kamati ilikagua Hospitali ya Wilaya ya Tabora ambayo ujenzi wake unatekelezwa kwa nguvu ya serikali kuu pamoja na nguvu ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora. Ujenzi unaendelea na Jengo la Wagonjwa wa Nje (OPD),Kichomea taka(incinerator),  na Maabara yako kwenye hatua za umaliziaji. Huduma kwa wagonjwa wa nje zinatazamiwa kuanza hivi karibuni. Vilevile jengo la Mionzi(Radiology), Jengo la mama na motto (Maternity Ward),  Jengo la kufulia nguo( Laundry),  Jengo la Utawala na Stoo ya dawa ni miongoni mwa majengo yanayoendelea kujengwa.

Kamati ilipata kukagua umaliziaji wa Zahanati ya Itulu, ambayo inajengwa kwa nguvu za Serikali kuu, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora na nguvu za Wananchi wa kijiji cha Itulu. Zahanati hii inatazamiwa kugharimu zaidi ya milioni sabini mpaka kukamilika.

Zahanati ya Igombe ni miongoni mwa miradi iliyokaguliwa, zahanati hii inajengwa kwa nguvu kubwa ya pesa kutoka Serikali kuu pamoja na nguvu ya wadau wa maendeleo  na Wananchi wa kijiji cha Igombe. Utekelezaji wa mradi huu unatizamiwa kugharimu zaidi ya milioni sabini kwa mujibu wa tathimini ya kamati ya ujenzi. Kamati vilevile iliweza kukagua umaliziaji wa Zahanati ya Igosha, Zahanati ya Igosha  inajengwa kwa nguvu kubwa kutoka serikali kuu, Nguvu kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Tabora na nguvu za wananchi wa kijiji cha Igosha na mradi uko hatua za umaliziaji.

Kamati ilipata wasaa wa kukagua kikundi cha wajasiriamali cha SHANI YA MUNGU kilichopo kata ya Gongoni kikiwa ni miongoni mwa vikundi vinavyonufaika na mikopo itolewayo na Halmashauri na kimepata mkopo wa shilingi milioni tano. Hiki ni kikundi cha wanawake wajasiriamali wanaojishughulisha na ufugaji wa kuku, na vilevile kila mwanakikundi anakazi zake kama kuuza mkaa, kupika keki, kuuza nguo na kadhalika.

Katika majumuisho, wajumbe wa kamati walitoa maagizo kwa Wakuu wa Idara na Vitengo husika kufuatilia kwa umakini na kwa ukaribu zaidi ujenzi wa miradi kwani walibaini changamoto zinazojitokeza kati ya kamati ya ujenzi moja na nyingine, hivyo baadhi ya kamati zinahitaji kujengewa uwezo ili zifanye kazi kwa weledi na ufanisi zaidi na kuokoa fedha zaidi kama ilivyo malengo na madhumuni ya Serikali ya kutumia mfumo wa Force Account.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.