• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

KAMATI YA FEDHA NA UTAWALA IMEIPONGEZA MENEJIMENTI YA MANISPAA YA TABORA KWA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: May 3rd, 2023

Na Alex Siriyako:

Kamati ya Fedha na Utawala ya Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imeipongeza Menejimenti ya Manispaa kwa usimamizi mzuri wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika katika Kata mbalimbali za Manispaa hii.

Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Fedha na Utawala wametoa pongezi hizi leo Mei 3, 2023 katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo,ziara ambayo imefanyika kwa siku mbili mfululizo kwa maana ya tarehe mbili hadi tatu, Mei ,2023.

Kamati imeweza kukagua ujenzi wa Jengo jipya la Utawala la Manispaa ya Tabora, Ujenzi wa majengo manne ambayo ni Wodi ya Wanaume, Wodi ya Wanawake, Wodi ya Watoto pamoja na Mochwari  katika Hospitali ya Wilaya, Vyumba Viwili vya Madarasa na Ofisi moja katika Shule ya Msingi Bombamzinga , Kata ya Isevya, Ujenzi wa Zahanati ya Ng’ambo, Kata ya Kidongo Chekundu pamoja na Ujenzi wa Viwanja vya Mpira wa Miguu, mpira wa wavu, mpira wa kikapu katika Shule ya Tabora Wavulana, viwanja vinavyotarajiwa kutumika katika michezo ya UMISSETA na UMITASHUMITA mwaka huu kuanzia tarehe mbili, Juni.

Mhe. Nassir Mnenge, Naibu Meya wa Manispaa ya Tabora, kwa niaba ya wajumbe amemshukuru sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuipatia Manispaa ya Tabora fedha nyingi sana za miradi ya maendeleo na kuongeza kuwa Baraza la Madiwani kupitia Kamati zake za Kudumu litafanya kazi zake ipasavyo kuhakikisha kuwa miradi inajengwa kwa ubora uliuokusudiwa na thamani ya fedha katika miradi inaonekana.

Aidha pamoja na kuridhishwa na ubora wa majengo na thamani ya fedha iliyotumika, Wajumbe wameazimia fundi anayejenga Zahanati ya Ng’ambo iliyopo Kata ya Kidongio Chekundu asimamiwe kurekebisha makosa yaliyobainishwa na pindi akimaliza kurekebisha makosa hayo mkataba wake usitishwe mara moja kwani amekuwa mlevi wa kupindukia na kushindwa kumudu vema majukumu yake.

Katika kuhitimisha Ziara hii, Mhe. Nassir amewasihi sana Wataalamu wa Manispaa ya Tabora kuepuka kufanya kazi kwa mazoea na wajenge utamaduni wa kukubali kukosolewa na kupokea ushauri wa wadau mbalimbali hususani kwenye ujenzi wa miradi ya maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.