• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA KUTOA MILIONI TANO KWA KILA KATA KWA AJILI YA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Posted on: March 6th, 2020

Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kutoa kiasi cha Milioni Tano fedha za kitanzania kwa kila Kata ambapo zitaenda kusaidia urekebishaji wa miundombinu ya barabara.

Hayo yalisemawa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Bosco Ndunguru alipokuwa akitoa ufafanuzi wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa.

‘’Halmashauri ya Manispaa imetenga kiasi cha Milioni Tano (5) kwa kila Kata pesa ambazo zitaletwa kwenye Kata zenu kwa ajili ya kusaidia uboreshaji wa miundombinu hasa ya barabara, ambapo sasa kila Kata itaangalia vipaumbele kulingana na jiografia ya Kta yenyewe na viunga vyake ione kwamba ianze na barabra ipi angalau kuikwangua ili iweze kupitika au kuboresha mitaro kutegemea na ukubwa wa tatizo lenyewe,’’ alieleza Mkurugenzi Ndunguru.

Katika hatua nyingine Diwani wa Kata ya Mwinyi Mhe, Martin Daniel  alimueleza Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani kuwa Tarura Manispaa wanapaswa kuitazama Kata ya Mwinyi kwa jicho la tatu kwa kuwa jiografia yake ilivyo inapokea maji mengi sana yanayotiririka kutoka sehemu tofauti tofauti kama vile Ng’ambo, Kanyenye na kadharika.

Aidha Mhe, Martin alimuomba Mwenyekiti ili Baraza la Madiwani liwaombe Tarura waiangazie pia Kata ya Mpera ambayo pia imekuwa ikiathiriwa sana hasa pale ambapo mvua inakuwa imenyesha, kwa kuwa miundombinu yake haimudu wingi wa maji hivyo kupelekea maji kujaa barabarani na kwenye makazi ya wananchi. Tatizo hilo hupelekea hata watoto washule kushindwa kwenda shule na kuhatarisha maisha ya wakazi wanaoishi maeneo hayo.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Ikomwa Mhe, Salum Msamazi aliwapongeza sana Tarura kwa namna ambavyo wamekuwa wakitekeleza na kushughurikia kazi zao na matatizo ya kimiundombinu ya barabara, jambo ambalo hupelekea kuondoa kero wanazokabiliana nazo wananchi hasa wa Kata ya Ikomwa.

‘’Kwa upande wangu nawapongeza sana Tarura kwa namna ambavyo wamaekuwa wakishughurikia matatizo yanayowakuta wananchi hasa wa kata yangu kwenye suala zima la miundombinu, hata ukiwapigia simu Tarura wanafika kwa haraka na wanatatua tatizo husika kwa kweli napongeza sana, pia nampongeza zaidi Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora pamoja na Menejimenti yote kwa namna ambavyo wamekuwa wakishirikiana na uongozi wa Kata ya Ikomwa,’’ alisema Mhe Msamazi.

Naye Meneja wa Tarura Tabora Manispaa Mhandisi Edwin Kabwoto aliwaeleza wajumbe wa Mkutano wa Baraza la Madiwani kuwa, amepokea michango na maoni yote kutoka kwa wajumbe na kwamba naichukua na kwenda kuifanyia kazi. Aliongeza kusema kwamba Tarura Manispaa inafanya kazi kwa weredi na uwazi mkubwa sana na bila upendeleo wa Kata yoyote ile ,  aidha alisisitiza kuwa atakuwa akiwasilisha mpango kazi wa Tarura kwenye kila Mkutano wa Baraza ili kuweka uwazi zaidi na mwisho aliwaomba ushirikiano zaidi kutoka kwa Waheshimi wa Madiwani wote, Menejimenti ya Manispaa pamoja na wadau mbalimbali ili kuifanya Tarura kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na hatimaye kuifanya Tabora Manispaa kuwa sehemu bora na ya mfano zaidi kwa miundombinu.

 Mkutano wa pili wa Baraza la Madiwani Tabora Manispaa ulifanyika kwa siku mbili ulimalizika kwa wajumbe wote kupokea taarifa mbalimbali kutoka kwenye Kamati za Kudumu na kutoka kwenye kila Kata

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.