• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA YAPOKEA CHANJO 4030 ZA UVIKO-19

Posted on: August 3rd, 2021

Na Alex Siriyako,

Agosti 3,2021 imekuwa siku ya kihistoria katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, ni baada ya kupokea chanjo za Uviko-19 za awamu ya kwanza. Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ni miongoni mwa halmashuri saba zinazounda Mkoa wa Tabora ambapo zote hizi zimepata mgao huo wa chanjo,huku wilaya ya Tabora ikipata chanjo 4030.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora Dkt.Baraka Msumi amefafanua kuwa Wilaya ya Tabora imepata dozi za chanjo 4030 kwa awamu hii ya kwanza, na kipaumbele kwa sasa ni Watu wenye umri zaidi ya miaka hamsin(50), wenye magonjwa sugu na watumishi wa Idara ya Afya. Na akafafanua zaidi kwamba vituo vya chanjo kwa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kuwa ni Hospitali ya Rufaa Kitete, Kituo cha afya Maili Tano,kilichopo Ipuli, pamoja na Zahanati ya Town Clinic.

Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Dkt.Yahaya Nyawanda, wakati akiwaongoza wakazi wa Tabora kupata chanjo hizo, amemshukuru Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suruhu Hassani kwa kutupatia chanzo hizi 4030 watu wa Wilaya ya Tabora. Dkt.Nyawanda pia amewasihi wakazi wa wilaya ya Tabora kuja kupata chanjo hizi kwani ni tunu na fursa kubwa kwa wakazi wa Tabora manispaa. Amesisitiza kwamba chanjo ni bure na ni za hiari kwa wanaohitaji hususani wale wiliotajwa katika makundi yaliyopewa kipaumbele.

Katibu Tawala wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Ndugu Hamarksjold E.Yonaza ,nae alikuwa miongoni mwa watu wachache waliopata fursa ya kupata chanjo hii kwa siku ya leo, na aliweza kutoa nasaha zake kwa wakazi wa Tabora, amefafanua kuwa chanzo zimekuwepo sana, watu wamechanja chanjo za Polio, ndui na kadhalika. Amewasihi wakazi wa Tabora kujitokeza kwa wingi kuja kupata chanjo hii kwani ni bahati kubwa kuipata , kwamba kuna Watanzania wamesafiri kwenda mpaka nje ya nchi hii kufuata chanjo hii ya UVIKO-19.

Hali kadhalika, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Ndugu Sefu Salumu, nae alibahatika kuwa miongoni wa watu wachache waliopata fusa ya kupata chanjo hii kwa siku ya leo. Ndugu Sefu amewaasa wakazi wa Tabora kuachana na maneno ya mtaani na badala yake wawaone wataalamu wa Afya mahala popote pale wapate majibu sahihi juu ya chanjo hizi kwani kuna taarifa nyingi mtaani zisizo za kitaalam na wakazi wa Tabora wazipuuze ,waende kwa Wataalamu wa Afya kupata majibu sahihi ambayo ni ya kitaalamu zaidi.

Ndugu Mohamed Amdani almaarufu kwa Jina la Shakira, mwenye umri wa miaka 74, ni miongoni mwa wakazi wa Halimashauri ya Manispa ya Tabora waliopata fursa ya kupata chanjo hii na amewasihi wazee wenzake waje kuchanja, kwani chanjo ni kinga na anawasihi wasiogope.

Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Dkt. Yahaya Nyawanda aliwaongoza wakazi wa Manispaa ya Tabora kupata chanjo hii ya UVIKO-19 huku akiambatana na baadhi ya watumishi wa Halmashauri akiwemo Katibu Tawala, Kaimu Mkurugenzi na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, zoezi lililofanyika katika Kituo cha Afya Maili Tano,kata ya Ipili.

Mwisho.

Matangazo

  • ORODHA YA WAOMBAJI WALIOTEULIWA KATIKA AJIRA ZA MUDA ZA SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 July 28, 2022
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA TULI KATA YA IFUCHA - INALA July 25, 2022
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Usafi wa Mazingira kwa Wananchi Wote, Jumamosi ya mwisho kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI ROBO YA NNE KWA MWAKA 2021/2022 LAIPINGEZA MENEJIMENTI

    July 30, 2022
  • UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA USHIRIKA DUNIANI YAFANYIKA TABORA

    June 28, 2022
  • MANISPAA YA TABORA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA 2020/2021

    June 22, 2022
  • MKUU WA WILAYA AWAHAKIKISHIA USALAMA WATOTO WOTE WA MANISPAA YA TABORA

    June 16, 2022
  • Angalia Zote

Video

MSTAHIKI MEYA BW. RAMADHAN KAPELA - UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO NA UWEKEZAJI KATIKA MANISPAA YA TABORA
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • Mwongozo wa Matumizi ya TEHAMA
  • Taarifa Mbalimbali
  • Fomu ya maombi ya Leseni
  • Jarida 2020
  • eMrejesho
  • Fursa za Uwekezaji

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkurugenzi, Halmashauri ya Manispaa Tabora, 4 Barabara ya Kiwanja cha Ndege

    Anwani ya Posta: S.L.P 174, 45182 Tabora

    Simu ya Ofisi: 026-2604315/6088

    Simu ya Mkononi: 0784705044

    Barua Pepe: md@taboramc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.