• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

HAKIELIMU WAKABIDHI MAJENGO YENYE THAMANI YA ZAIDI YA MIL. 140

Posted on: March 23rd, 2022

Shirika lisilo la Kiserikali la Nchini Uingereza (HAKIELIMU) lenye Makao Makuu yake Jijini Dar es Salaam limekabidhi miundombinu ya majengo ya elimu yenye thamani ya zaidi ya Mil. 140 ikiwa ni matundu ya vyoo, vyumba maalumu vya wasichana kwa ajili ya kubadilishia pedi pamoja na bweni moja la wasichana.

Akitoa shukurani kwa niaba ya Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Balozi Dkt. Batilda Burian alisema analishukuru sana shirika la HAKIELIMU kwa kuweza kuchangia maendeleo ya Manispaa ya Tabora kwa kujenga miundombinu ya majengo ambayo yatachangia kwa kiwango kikubwa ukuwaji wa elimu kwa wanafunzi na kuongeza ufaulu hasa kwa watoto wa kike.

Mhe. Dkt. Batilda aliwaeleza HAKIELIMU kuwa watoto wa kike wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi sana ikiwamo mazingira ya umbali kutoka majumbani kwenda shule, hivyo uwepo wa bweni hilo la wasichana kutasaidia sana kuwaondolea changamoto walizokuwa wakikutana nazo njiani, na pale wanapokuwa kwenye hedhi jambo lilikuwa linawalazimu kutohudhuria masomo.

“Kipekee kabisa niwashukuru sana HAKIELIMU kwa kuwezesha miundombinu hii ya Elimu ili watoto wetu waweze kupata huduma hizi bora wakati huo wakiendelea na masomo yao bila kurudi nyumbani kwa ajili ya kubadilisha pedi,” alisema Mhe. Dkt. Batilda.

Mhe. Dkt. Batilda alitumia fulsa hiyo kuwaonya wanafunzi wote kujiepusha na uhusiano wa kimapenzi wakiwa shuleni, na pia kujiepusha kabisa na uhusiano wa jinsi moja jambo ambalo ni hatari sana kwa wanafunzi na kuwataka waalimu kulikemea kwa nguvu zote kwenye shule zao.

Aidha Mhe. Batilda aliwahakikishia HAKIELIMU kuwa miundombinu hiyo waliyopewa watailinda kwa nguvu zote ili ije kuwa na tija zaidi hata baadae ambapo na vizazi vijavyo vinufaike, kwakuwa elimu haina mwisho.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa HAKIELIMU Dkt. John Kalage aliwapongeza sana Manispaa ya Tabora kwa kuweza kupata miradi sita kutoka shirika lao la HAKIELIMU, na kwamba wameitendea haki kwakuwa kukamilika kwa miradi hiyo kunaenda kupunguza kabisa kama siyo kuondoa kabisa changamoto zilizokuwa zikiwakabili wanafunzi. Aidha Dkt. Kalage alimuahidi mgeni rasmi ambaye alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora kuwa shirika la HAKIELIMU litaendelea kushirikiana na uongozi wa Mkoa ili kwenye miradi ijayo pia waweze kuileta tena Tabora.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda aliwashukuru na kuwapongeza  pia HAKIELIMU kwa msaada huo wenye thamani ya zaidi Mil. 140 na kwamba miradi hiyo inaenda kuongeza tija kubwa kwa wanafunzi, wazazi na wadau wa elimu kwa ujumla.

“Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Tabora, tunawashukuru sana HAKIELIMU, tunawapongeza sana na mwisho tuna waahidi kuwa tutailinda miundombinu hii na kuitunza ili isaidie na watoto wetu wa baadae,” alisema Dkt. Nawanda.

Mhe. Dkt. Nawanda alitumia fulsa hiyo pia kuwaomba wazazi wa wanafunzi wa Itonjanda kufikia tarehe 31/3/2022 kuwa wameleta wanafunzi wao na kujaza nafasi zilizo wazi kwenye bweni, na baada ya hapo kama watashindwa basi atatoa nafasi hizo wazi kutoka kwenye shule nyingine.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.