• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

DKT. BATILDA AIPONGEZA TUWASA KWA KUFIKIA ASILIMIA 92 ZA UTOAJI HUDUMA YA MAJI KWA TABORA MANISPAA

Posted on: September 20th, 2021

Na Paul Kaembo-TMC.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Buriani ameipongeza Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Tabora –TUWASA kwa kuweza kufikia asilimia tisini na mbili (% 92) ya utoaji wa huduma ya maji safi kwa wananchi wa Halmashsauri ya Manispaa ya Tabora ambapo jumla ya Kata 24 kati ya Kata 29 zinapata huduma ya maji.

Pongezi hizo amezitoa wakati wa ziara yake ya kikazi alipotembelea TUWASA na kukagua vyanzo mbalimbali vya maji vilivyopo hapa Manispaa ya Tabora ikiwamo Bwawa la Igombe, Tanki la maji –Itumba na Tanki za maji zilizopo Filta baada ya Mkurugenzi wa TUWASA Mhandisi ……kusoma na kwasilisha taarifa ya Mamlaka kwake Dkt. Batilda.

“Niwapongeze sana TUWASA kwa namna ambavyo mmeweza kuongeza wigo wa utoaji huduma kwa wananchi wote hasa wa Manispaa ya Tabora ambapo mmefikia asilimia 92 sawa na Kata 24 kati ya Kata zote 29 zinazounda Halmashauri ya Manispaa ya Tabora jambo ambalo ni jema sana kwa muktadha wa TUWASA na wananchi wa Manispaa kwa ujumla kwenye hili mnastahili pongezi,” alisema Mhe. Dkt. Batilda.

Awali akiwasilisha taarifa yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhandisi …..  alisema kuwa pamoja na mafanikio ya kuweza kutoa huduma kwa asilimia 92, lakini pia wameweza kuunganisha mfumo wa maji taka kwa jumla ya wateja 482, kupatikana kwa huduma ya maji masaa 22 kwa siku, jumla ya tanki za maji saba zipo hapa Manispaa ya Tabora, na kubadilisha mtandao wa bomba za muda mrefu na kuweka mfumo wenye bomba za kisasa zaidi.

Kando na mafanikio hayo, Mamlaka inapitia changamoto kadhaa ikiwamo hujuma kwa miundombinu yake hasa ya mtandao wa bomba zilizochimbiwa chini ya ardhi ambapo mara nyingi hukatwa, gharama kubwa ya utoaji wa huduma ya maji kutoka Ziwa Victoria kulinganisha na maji yanayopatikana kwenye bwawa zilizopo hapa Manispaa ya Tabora. Matumizi ya kibinadamu kwenye vyanzo vya maji, uchafuzi wa mazingira, na kutolipa ankara kwa wakati kutoka kwa watumiaji wa huduma.

Aidha Mhandisi ….. alibainisha baadhi ya mikakati waliyonayo Mamlaka ili kuwafanya wateja wao waendelee kufarahia huduma yao ikiwa ni pamoja na kuhahaikisha kuwa wanapunguza gharama za uendeshaji huduma ya maji toka Ziwa Victoria, kudhibiti upotevu wa maji angalau ifikie asilimia 26 kati ya 36 zilizopo hivi sasa, kushirikisha wadau kwenye kazi na utekelezaji wa shughuri za Mamlaka ili kupata mtazamo wao namna ya kuboresha huduma, kuimarisha makusanyo na kuongeza wateja zaidi kwa kuwa hivi sasa maji ni mengi kulinganisha na awali.

Kwenye ziara hii Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Dkt. Batilda Buriani aliongozana na Katibu Tawala wa Mkoa Ndg Msalika Makungu, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mhe. Dkt. Yahaya Nawanda na baadhi ya watumishi wa Serikali.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 06, 2025
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Mazoezi kwa Wafanyakazi na Wananchi, Jumamosi ya Pili kila Mwezi March 23, 2017
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MEYA WA MANISPAA YA TABORA AELEZA KUWA KILA MFANYABIASHARA ANAO WAJIBU WA KULIPA TOZO NA USHURU WA HALMASHAURI

    May 20, 2025
  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.