• Lalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
TABORA MUNICIPAL COUNCIL
TABORA MUNICIPAL COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA MANISPAA YA TABORA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Usafi na Mazingira
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Fedha na Biashara
      • MIfugo na Uvuvi
    • Vitengo
      • Ugavi na Manunuzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
    • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utalii
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Malalamiko
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi , Elimu na Afya
      • Kamati ya Maadili
      • Ukimwi
    • Ratiba
      • Vikao vya Halmashauri
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu za maombi
    • Miongozo, Sera na Kanuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Picha

DC- KOMANYA AWATAKA WENYEVITI WA MITAA, VIJITI NA VITONGOJI KWENDA KUWATUMIKIA WANANCHI WAO

Posted on: December 3rd, 2019

Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mjini Komanya Kitwala amewaambia Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji kuwa wanao wajibu mkubwa wa kuwa karibu na kuwatumikia wananchi wao wote waliowachagua na ambao hawakuwachagua tena bila ubaguzi ili waweze kuwaletea maendeleo.

Hayo yamesemwa leo kwenye mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano uliopo Shule ya Sekondari ya Mihayo na kuliohudhuriwa na Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji wote waliochaguliwa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.

Kwenye Mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Tabora Komanya Kitwala aliwaekeza Wenyeviti hao kuwa wanatakiwa kwenda kuishi na kutekeleza yafuatayo; kwenda kusaidia kutatua migogoro hasa inayohusu Ardhi. Kumekuwa na migogoro mingi sana hasa inayohusu Ardhi  ambapo unakuta migogoro hiyo inachangiwa na Wenyeviti wenyewe na wengine hawashughuriki ipasavyo kuitatua kwa maslahi mapana ya wananchi.

‘’Saidieni kutatua migogoro hasa ya Ardhi kwenye maeneo yenu. Haiwezekani Viongozi wote wapo hapo, yaani  kuna Mtendaji wa Mtaa, Mwenyekiti yupo lakini bado kuna migogoro ya Ardhi mpaka inafikia wakati wanalazimika kuja Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au kwenye Ofisi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Tabora Mjini’’, alisema Komanya.

Matumizi mabaya ya madaraka: Mkuu huyo wa Wilaya aliendelea kuwaelekeza Wenyeviti hao kwenda kutumia vizuri madaraka waliyonayo na siyo vinginevyo. Viongozi wote mliochaguliwa mkienda kutumia madaraka vibaya mtachomolewa haraka sana, badala ya kwenda kutatua matatizo na kusaidia wananchi, wao wanaenda kuwanyonya wananchi na kutumia madaraka yao vibaya.

‘’Nafasi ya Mwenyekiti ni nafasi ya kuwatumikia wananchi na siyo sehemu ya kwenda kujilipa mamilioni ya pesa na kupora Ardhi za watu, muhuri wako, nafasi yako ukienda kuitumikia vibayatutaunda timu ikuchunguze na ukibainika tutakutoa na kuitisha uchaguzi mwingine, maana haufai’’, Komanya.

Kuchelewesha kutoa maamuzi yenye maslahi kwa umma na kusimamia uwajibikaji: Viongozi mnatakiwa kufanya maauzi yenye nia njema kwa umma, unakuta ukweli upo wazi na unaonekana kabisa lakini kunakuwa na ucheleweshwaji mkubwa wa kutoa maamuzi kwa wakati.

Ambapo alitaja baadhi ya maeneo yenye kuchelewesha utoaji wa maamuzi kama vile kata ya Mwinyi, Malolo,Mtendeni, Uyui na maeneo mengine. Hivyo aliwaasa sana Wenyeviti hao kwamba kuna kila sababu ya kutoa maamuzi kwa wakati, khivyo wakafanye maamuzi kwa maslahi mapana ya wananchi wao na wasiogope kutishiwa kwakuwa wanatenda haki.

Usimamizi wa Miradi ya Maendeleo: Kwenye hili aliwataka Wenyeviti wote kwenda kusimamia Miradi yote iliyopo kwenye maeneo yao kwa ajili ya maslahi makubwa ya Taifa letu ili mwisho wa siku kuwepo na mifano bora ya usimamizi huo. Komanya alitoa mifano ya sehemu zilizofanya vizuri ni kama vile Shule ya Msingi Kanyenye, Kwihara, Isike, Mpepo mnaweza kuona ni jinsi gani usimamizi unapokuwa mzuri na matokeo yake yanakuwa ni mazuri sana. ‘’Nendeni mkasimame kwenye nafasi zenu vizuri ili Manispaa yetu isonge mbele kwakuwa tunao mpango wa kujenga madarasa na tutaleta matofali, nendeni mkawasimamie ujenzi huo na muwahamasishe wananchi wenu yote inawezekana tukiamua’’, alisema Komanya.

Kwa upande Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Bosco Ndunguru alisema kwanza kule kuna kazi za Watendaji na zile za Wenyeviti hivyo mkashirikiane wote kutekeleza yote yaliyoelekezwa na viongozi wetu. Pili, mambo yote yanafuata kanuni, taratibu na sheria hivyo pale unapokwama na hauna uhakika ni vema ukaulizia sheria inasemaje ili usije kuonekana unayoyafanya yaonekane yapo kwa mujibu wa sheria na uzuri ni kwamba mawasiliano yapo.

La mwisho, kila unapofanya shughuri za utekelezaji kunahitaji mawasiliano, kitu gani kinachohitajika na bahati nzuri kuna ngazi mbali mbali hapo.

’’Sasa basi Wenyeviti kama ni wa Mtaa lazima umtaarifu Mtendaji wa Kata ili ifike huku, siyo kila kitu unakipiga huku juu na kama itakuwa hivyo basi mpe nakala wa eneo husika ili nay eye afahamu, mfano kuna mgogoro basi mpe nakala ili isionekane ni majungu tuu’’, alisema Ndunguru.

Mkutano huo wa Mkuu wa Wilaya na Wenyeviti wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji ulihudhuriwa pia na viongozi mbali mbali wakiwemo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Tabora Mjini Mohamed Katete, Katibu wa CCM Tabora Mjini Adam Makulilo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Tabora Mjini Rashid Ramadhani (Tall), Katibu Tawala Tabora Mjini H. Yonaza, Afisa Uchaguzi Msaidizi Tabora Manispaa pamoja na Waandishi wa habari mbali mbali.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFAZI ZA KAZI ZA MUDA MDH TABORA November 14, 2024
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2024 December 17, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA March 05, 2024
  • FOMATI ILIYOBORESHWA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI (PSLE) 2024 KUTOKA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA March 13, 2024
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADIWANI WA MANISPAA YA BUKOBA WAKOSHWA NA MANDHARI NZURI NA SAFI YA TABORA

    April 10, 2025
  • KAMATI YA SIASA WILAYA YA TABORA YARIDHISHWA NA MIRADI YA KIMKAKATI INAYOTEKELEZWA WILAYANI HAPA

    January 09, 2025
  • MIKOPO YA ZAIDI YA BILIONI 1.6 YATOLEWA NA MANISPAA YA TABORA

    January 04, 2025
  • MADIWANI WA KAHAMA WAIPONGEZA MANISPAA YA TABORA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI MIKUBWA YA KIMKAKATI

    December 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

MAKALA Ukuaji wa Kasi wa Mji wa Tabora ndani ya Miaka Miwili (2)
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Jarida la Halmashauri Julai - Septemba 2022
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri 2021/22 - 2025/26
  • Capital Investment Plan
  • Tabora Master Plan 2015 - 2035
  • eMrejesho ( Kutuma, kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi)
  • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Fursa za Uwekezaji
  • Kanuni za Maadili ya Utumishi wa Umma

Kurasa Zinazofanana

  • IKULU
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • Sekretarieti ya Ajira
  • Mkoa wa Tabora

Waliotembelea Tovuti

world map hits counter

Waliotembelea Tovuti

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.Haki zote zimehifadhiwa.